Wakatoliki
na Urais wa Marekani
l
Alianza Al Smith, Kennedy na sasa John Kerry
WAKATI
taifa kubwa kama Marekani linaaminiwa na walimwengu kwa kuwa na demokrasi ya
hali ya juu. Kuna ubaguzi wa kidini katika kuchagua marais. Moja ya madhehebu ya
dini ambayo yalibaguliwa kwa muda mrefu ni Wakatoliki. Ili kujua mtazamo wa
Wamarekani juu ya rais Mkatoliki fuatilia makala haya kama ilivyoandikwa na Erick Samba.
Wakati Seneta John F. Kennedy wa Massachusetts alipogombea
urais mwaka 1960, alikabiliana na mashambulizi ya maswali kutoka kwa
Waprotestanti, maswali kama, “Tunajuaje kwamba unaweza kutenganisha imani
yako ya Kikatoliki na wajibu wako wa kisiasa?”
Lakini
mgombea wa sasa, Seneta John F. Kerry pia wa Massachusetts mambo hayatakuwa
hivyo; ila yeye maswali yake yatatoka kwa Wakatoliki wenzake na huenda yakawa
kama: “Ni jambo gani linalokufanya udhani kwamba unaweza kutenganisha imani
yako ya Kikatoliki na majukumu yako ya kisiasa unapofika wakati wa kupigia kura
utoaji mimba?”
Mambo
mengi kuhusu maseneta hao wawili wa Massachusetts yanaweza kuwa sawa, ila hali
ya hewa ya kisiasa na kidini ya Kerry inafanana kidogo sana na ile
aliyokabiliana nayo Kennedy.
Kati
ya zama za Kennedy na Kerry kulitokea hukumu ya Mahakama Kuu kuhusu utoaji
mimba na kuongezeka kwa uangalizi wa baadhi ya watu katika kanisa kuhusu kura
za wanasiasa Wakatoliki bungeni.
Kerry
kama mgombea urais wa pili kutoka chama kikubwa akiwa Mkatoliki katika
historia, alichokabiliana nacho Kennedy kabla ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa
Vatican, ulikuwa ni umma wa Wamarekani ambao ulitaka kuhakikishiwa iwapo Baba
Mtakatifu asingekuwa anaongoza serikali ya Marekani.
Lakini
Kerry, kwa upande mwingine, ni Mkatoliki ambaye atatakiwa kutetea msimamo wake
kwa nini huwa hajali mafundisho ya Kanisa pale anapopiga kura katika bunge la
Seneti, hasa kuhusiana na kuunga kwake mkono utoaji mimba kuendelea kuwa halali
kisheria, wakati mafundisho ya kanisa yanapinga vikali.
Kabla
ya Kennedy kuwa mgombea urais wa Marekani na kushinda, kulikuwa na mgombea
mmoja tu Mkatoliki aliyekuwa amewahi kugombea kiti hicho. Huyo sio mwingine
bali ni Gavana wa New York wakati huo, Al Smith ambaye hata hivyo alishindwa
katika uchaguzi wa mwaka 1928.
Katika
hotuba yake kwenye bunge la Seneti hapo Januari 1928, Seneta Thomas Heflin wa
Alabama, alionya kwamba, Wakatoliki walikuwa wanajaribu kukiteka chama cha
Democratic ili kupinga “Ku Klux Klan” au utaratibu wa Kiprotestanti na
kwamba walikuwa wanajaribu kudhibiti magazeti ya kusini mwa Marekani ili
kumwimarisha mgombea wao wa urais, Gavana Smith.
Alisema,
“azimio la Kikatoliki limetolewa katika makala ya siri kwamba ‘Al Smith
atafanywa rais. Wataweka mkono mzito wa dola ya Kikatoliki juu yenu na
kufutilia mbali maisha yaliyotokana na Uprotestanti katika Marekani.”
Hali
hiyo ya wasiwasi na hofu juu ya Wakatoliki, iliibuka tena miaka 32 baadae,
wakati Seneta John Fitzgerald Kennedy wa Massachusetts alipoanza mbio za
kuelekea Ikulu ya Marekani mwaka 1960.
Kwa
mfano Kanisa la Kibaptisti la Kusini mwa Amerika, lilipitisha azimio la pamoja
kuelezea hofu yake iwapo Kennedy au Mkatoliki anapaswa kuwa rais wa Marekani.
Tamko
jingine lililosainiwa na wachungaji pamoja na walei 150 wa Kiprotestanti
wakiongozwa na Mchungaji Norman Vincent Peale, lilisema kwamba, rais Mkatoliki
angekuwa chini ya ushawishi mkubwa wa hairakia ya kanisa lake na kuoanisha sera
ya mambo ya nje ya Marekani na ile ya Vatican.
Hata
hivyo, Rais Harry Truman alilaani hali ya kutovumiliana kidini, ingawa mwanzoni
alikuwa amepinga uteuzi wa Kennedy kwa sababu ya kutoelewana na baba yake,
Joseph P. Kennedy aliyekuwa amewahi kuwa balozi nchini Uingereza.
Truman
alisema, “Siko kinyume na Baba Mtakatifu. Niko kinyume na Pap,” akimaanisha
Kennedy mkubwa.
Hata
hivyo, John F. Kennedy alitatua suala la Ukatoliki katika hotuba yake kwa njia
ya televisheni, Septemba 1960, aliposema ukomunisti, umaskini, elimu na sayansi
ya anga za juu, yalikuwa ndiyo mambo muhimu sana ya kujadili katika uchaguzi
lakini yalikuwa yamefunikwa na mjadala juu ya Ukatoliki.
Alieleza
imani yake katika Marekani, ambamo utengano kati ya kanisa na dola ni mkubwa. Hakuna askofu Mkatoliki anayeweza
kumwambia rais (iwapo ni Mkatoliki) namna ya kutenda na hakuna mchungaji wa
Kiprotestanti angeweza kuwaambia waamini wake ni nani wa kumpigia kura.
Kennedy
aliwataka wapiga kura kumhukumu kwa kufuata rekodi yake ya kisiasa, na sio
kufuata nukuu zilizochaguliwa kwa uangalifu kutoka kwenye kauli na taarifa za
viongozi wa kanisa.
Hata
hivyo, alikubali tamko la maaskofu Wakatoliki wa Marekani la 1948 ambalo
lilisisitiza utengano kati ya kanisa na dola.”
Alisema
kuwa yeye hakuwa mgombea urais kwa tiketi ya Wakatoliki. “Mimi ni mgombea urais
kwa tiketi ya Chama cha Democrat, ambaye pia nimetokea kuwa Mkatoliki. Siongei
kwa niaba ya kanisa langu katika masuala ya umma, na kanisa haliongei kwa niaba
yangu.”
Maneno
haya yalimsaidia Kennedy kushinda kwa tofauti ndogo. Majivuno ya Wakatoliki kwa
kuwa na rais ambaye alikuwa mmoja wao yaliashiria mwisho wa muda ambao
walijihisi kutengwa kisiasa.
Hakuna
wakati wowote ambao tungeweza kumwona mtu akisema, “Baba Mtakatifu atakuwa
akiongoza nchi,” alisema Clyde Wilcox profesa wa Chuo Kikuu cha Georgestown.
Hata
hivyo, jitihada za Kennedy kutenganisha dini yake na wajibu wake hazikujulikana
kwa Wakatoliki. Wala viongozi wa kanisa hawakuwa wakifurahishwa na upinzani
wake wa ajenda ya maaskofu, kama kumrudisha balozi wa Marekani katika Vatican.
Baada
ya Kennedy kuvunja mwiko, hatua ya kuwajumuisha Wakatoliki kama wagombea wa
umakamu wa rais lilikuwa jambo la mara nyingi japo halikufanikiwa, lilikuwa ni
mkakati wa vyama vyote viwili katika uchaguzi tangu mwaka 1964 mpaka 1972.
Kwa
upya, “suala la Ukatoliki” lililipuka upya mwaka 1984 juu ya wanachama wawili
wa Democrat kutoka New York, mwakilishi Geraldine Ferraro na Gavana Mario
Cuomo.
Tangu
siku yake ya kwanza ya kampeni kwa ajili ya nafasi ya makamu wa rais, kama
mgombea mwenza wa Walter Mondale wa Minnesota, Ferraro aliulizwa kwamba
anawezaje kuwa Mkatoliki safi na huku anapiga
kura kama alivyokuwa amefanya awali kuunga mkono uhalalishaji wa utoaji mimba.
Askofu
Mkuu wa New York, Mhashamu John J. O’Connor, ambaye baadae alikuwa kardinali,
alikwaruzana waziwazi na msimamo huo kuunga mkono serikali kufadhili utoaji
mimba, kwa maelezo yake kwamba anatenganisha mafundisho ya kanisa na wajibu
wake kwa umma.
Tangu
wakati huo wanasiasa Wakatoliki wamekuwa wakiegemea hoja kwamba: “Mimi binafsi
napinga utoaji mimba, lakini simaanishi kwamba ninapaswa kutunga sheria ya
imani yangu ili kufanya utoaji mimba kuwa halali katika nchi hii.”
Mwaka
1990, Kardinali O’Connor alisema kuwa, hoja za namna hiyo zitawafanya wanasiasa
Wakatoliki kutengwa, ingawa alisema yeye na maaskofu kama kundi, wanasisitiza
ushawishi kwa wanasiasa ili wabadili msimamo badala ya kuwatenga.
Muda
mfupi kabla ya kutajwa kama mkuu wa jimbo kuu la St. Louis Desemba iliyopita,
Askofu Mkuu Raymond L. Burke aliwaambia mapadre katika jimbo la La Crosse,
Wisconsin, kuwanyima Ekaristi wanasiasa Wakatoliki ambao hawafuati mafundisho
ya kanisa juu ya utoaji mimba na euthanasia (kifo cha huruma).
Askofu
Mkuu wa Boston, Mhashamu Sean P. O’Malley alisema kwamba wanasiasa Wakatoliki
wanaounga mkono utoaji mimba, wanapaswa kuacha kupokea komunyo kwa hiari,
ingawa alisema kanisa halinyimi sakramenti hiyo kwa watu wanaoijongea altare,
kwa kuamini kwamba wanafanya hivyo, “kwa imani safi.”
Mwaka
2003, nyaraka mbili zilizotolewa na Vatican ziliwataka wanasiasa Wakatoliki
kuwa na jukumu kubwa na wazi la kupinga sheria ambazo zinakiuka mafundisho ya
kanisa kuhusu haki ya uhai au ndoa za jinsia moja.
Kwa
wakati huu ambapo John Kerry anatarajiwa kuwa mgombea urais wa kwanza Mkatoliki
katika miaka 44, baadhi ya makundi ya kutetea uhai yanamshinikiza Askofu Mkuu
O’Malley na maaskofu wengine kumzuia kupokea komunyo takatifu kwa sababu
hafuati mwongozo wa kanisa juu ya utoaji mimba.
Katika
kitabu chake cha mwaka 2003, “Mwito kwenye Huduma,” Kerry alijieleza kama
“Mkatoliki anayeamini na kuishi imani yake.” Yeye pamoja na mkewe, Teresa Heinz
Kerry, mara nyingi huhudhuria misa Jumapili.
Kerry
ambaye aliachana na mkewe wa kwanza mwaka 1988, baadae alisema kwamba alikuwa
akitafuta ubatilisho wa ndoa yake. Lakini mpaka sasa haikujulikana kama
ubatilisho huo ulifikiwa na majimbo ya Kikatoliki huwa hayatangazi masuala hayo
hadharani.
Mke
wake wa sasa alibaki mjane baada ya kufiwa na mumewe Seneta John Heinz wa
Pennsylvania (Republican), alikufa katika ajali ya ndege mwaka 1991.
Katika
kura za hivi karibuni kwenye bunge la Seneti, Kerry alipinga miswada ya kupiga
marufuku utoaji mimba, akaunga mkono uondoaji wa marufuku ya utoaji mimba
katika maeneo ya jeshi la Marekani, nchi za nje na kuunga mkono azimio na
kudhibitisha kwamba hukumu ya kuhalalisha utoaji mimba. Misimamo yote hiyo ni
kinyume na ule wa kanisa lake.
Kuhusu
masuala mengine, misimamo ya Kerry karibu inafanana na misimamo inashawishiwa
na kanisa. Kwa mfano, huwa anapinga adhabu ya kifo isipokuwa kwa magaidi.
Mafundisho
ya kanisa ya hivi karibuni yanasisitiza kwamba, katika jamii ya kisasa hakuna mazingira
ambamo adhabu ya kifo ni lazima.
Majibu
ya Kerry juu ya shutuma dhidi yake kutokana na kupuuza mafundisho ya Kikatoliki
kuhusu utoaji mimba, yatajengeka katika mwenendo wa kampeni zake. Ingawa kauli
moja aliyoitoa mwaka jana inarudia kile alichosema Kennedy miongo kadhaa wakati
akijibu shutuma tofauti kabisa, lakini zenye msingi wa kidini.
Shirika
la habari la Associated Press lilimnukuu Kerry hapo Agosti mwaka jana
akitoa maoni yake kuhusiana na waraka uliotolewa na Vatican ambao uliwataka
wabunge Wakatoliki kupinga ndoa za jinsia moja.
“Ninaamini
katika kanisa na ninalijali sana. Ila nafikiri kwamba ni muhimu kanisa
kutowaelekeza wanasiasa nini cha kufanya. Huko ni kuvuka mpaka ambako sio sawa
nchini Marekani.”
Sababu kumi
za kuzaa mtoto
BAADHI ya watu wamekuwa wakiwaona watu
wengine hasa watoto wadogo na watoto ambao hawajazaliwa kama “magugu watu”
wanaokwaza ustawi wa watu wengine duniani hivyo, wanastahili kuondolewa kabisa
au kuzuiliwa wasizaliwe.
Watoto
wanaowekwa katika janga hilo, wanauawa ama wakiwa wamekwishazaliwa, au
hawajazaliwa kwa njia ya utoaji mimba. Watu wengine wanatumia juhudi kubwa
kuhakikisha kuwa, hawazai mtoto hata mmoja., ili wafaidi maisha. Lakini je,
wanajua vyema faida za kupata watoto? Ungana na MWANDISHI WETU katika makala
hii ujue sababu kumi za kupata mtoto. Wakati hayo yakiendelea, Makala hii
inazitaja sababu kumi, za kuzaa watoto.
Huku makala ikisisitizwa na Kanisa na jamii kuwa uzazi bora ni ule unaozingatia
idadi ya watoto ambao wazazi watamudu kuwalea na kuwapa huduma muhimu za
Kijamii hadi wanapojitegemea
Biblia Takatifu inatuambia kuwa
watoto ni baraka kutoka kwa Mungu na ndivyo walivyo.
Lakini, tunaishi katika ulimwengu unaochukia uzao. Utetezi wa
kifo umekengeusha thawabu ya uzazi wa mtoto na kuuona uzao kuwa ni chukizo la
mlipuko wa watu. Wazazi wa Kikristo mara kadhaa huhitaji kuhamasishwa ili
wakubali thawabu za ziada.
“Tazama wana ndio urithi wa Bwana Uzao wa tumbo ni
thawabu” (Zab 127: 3).
Sababu ya Kwanza
Pata mtoto ili uungane na Mungu katika kuumba.
Zaeni mkaongezeke
Wazazi wamepewa jukumu maalum na
Mungu la kusaidia kuumba roho isiyokufa. hata malaika hawajapatiwa neema hiyo.
Mtu mashuhuri duniani ni mama. Hawezi kujivuna kuwa amejenga
Kanisa Kuu pekee. Lazima awe amejenga kitu kingine cha fahari zaidi kuliko
Kanisa Kuu (Katedrali); makazi ya roho isiyokufa, mwili mkamilifu wa mtoto
wake.
Hata malaika hawajapatiwa neema hii. “Ni nini lililo tukufu
zaidi ya hili kuwa mama?”
Sababu ya pili
Hakuna furaha iliyo kubwa zaidi kama kumkaribisha mtoto mwingine katika
maisha yako.
Utashangazwa na jinsi mtoto wako alivyoumbika kwa ukamilifu
na jinsi utakavyompenda. Utafurahiwa na kila sehemu ya mwili wa mtoto wako.
Rangi ya nywele zake umbile la pua yake na tabasamu lake
lisilo kifani na utaongea juu ya upande wako au wa mumeo.
Katika hali ya shukrani, kuzaliwa kwa mtoto kutakufunga zaidi
kwa Mungu kuliko ilivyokuwa kwanza. “Ulikuwa muujiza wa ajabu uliowahi kutokea
katika maisha yangu,” aliwahi kuandika Whittaker Chambers kuhusu binti
yake katika kitabu cha Witness
na katika maisha ya wengi wetu.
“Nilifikiri kuwa siku moja nitakuwa msanii na kutengeneza
kazi maarufu sana, badala yake, Mungu amenifanya kuwa mama na watoto wangu;
ndio zao lake bora. Maumbo ya maisha yao yatadumu baada ya kifo changu.
Kilichopangwa mioyoni mwao kitadumu milele.” (mtu aliyeyasema haya,
hajulikani).
Sababu ya tatu
Pata mtoto ukue katika utakatifu na thawabu.
Kwa wale wanaoamini na kuwa na familia, Mungu huwapatia watoto
kama njia ya kuwakuza katika utakatifu na thawabu.
Watoto huwafundisha wazazi wao uvumilivu, subira, upendo na
unyenyekevu. Wanawapatia wazazi wao nafasi ya kutekeleza kwa matendo huruma ya kimwili na kiroho.
Watoto huzaliwa uchi nasi tunawavika, wenye njaa nasi
tunawalisha, wenye kiu nasi tunawapa maji ya kunywa. Matendo haya yote
tunapaswa kuyatenda kwa Mungu wa hawa “ndugu zetu wadogo” tunatenda kwanza kwa
watoto wetu.
Mtakatifu Katarina wa
Sienna alipata maono. Mungu alimwingiza kwenye chumba kilichojaa misalaba na
kumwambia achague mmoja.
Mtakatifu Katarina alichagua msalaba mkubwa na mzito zaidi,
lakini Mungu alimwambia huo haukuwa wake”; huo ulitengwa kwa ajili ya wazazi
wenye familia kubwa.
Sababu ya nne
Pata mtoto usaidie kumaliza janga la
utoaji mimba.
Mama Teresia wa Calcutta aliwahi kuulizwa juu ya njia bora ya
kuendelea na shughuli za utetezi wa uhai, alijibu kwa uhakika wote, “Kuwa na
familia kubwa na utii ndiyo njia bora ya kumaliza janga la utoaji mimba.” Sio
vigumu kuelewa kanuni hii inavyofanya kazi.
Kwa kadiri tunavyokabiliana na uhaba wa watoto kutokana na
matumizi ya vidhibiti mimba, kufunga kizazi na utoaji mimba, ndivyo jamii ya
watu inavyopoteza viungo vya furaha na matumaini ambayo huletwa na watoto tu.
Katika hali ya namna hii, vidhibiti mimba na utoaji mimba, vinajilisha vyenyewe
kwa kadiri hao wachache wanavyozidi kupunguzwa. Kwa kuwa na mtoto unaonesha
tena kuwa, mtoto ni zawadi kuu ya Mungu.
“Watoto hujenga maisha ya familia na jamii” kama ambayo Baba
Mtakatifu Yohane Paulo II aliwahi kusema, “Mtoto anakuwa zawadi kwa kaka na
dada zake, wazazi wake na familia yote.”
Uhai wake wote huwa ni zawadi kwa watu wote ambao walikuwa
watoaji wa uhai na ambao walilazimika kuonja uwepo wake, ushiriki wake katika
maisha yao na mchango wake katika mambo mema na kwa jumuiya ya wanafamilia.”
Kwa kadiri jamii hii inavyokuwa ya watu wengi, ndivyo hivyo jamii hii inavyokuwa ya watu watetea
uhai, na ndiyo itakavyokuwa rahisi kupigana vita dhidi ya maovu na utoaji
mimba.
“Nazishuhudia mbingu
na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka
na laana basi chagua uzima ili uwe hai wewe na uzao wako(Kumb 30:19)
Sababu ya tano
Pata mtoto ili watoto wako
wa kiume na wa kike wapate wadogo zao.
Watoto wenye wadogo zao wanajifunza kushirikiana mapema
katika maisha yao. Wanajifunza kutenda kwa zamu na kujali mahitaji ya wengine
kabla yao wenyewe.
Undugu unaojengwa kati ya ndugu hawa ambao ni kaka na dada,
ni wa kudumu, wa maisha na ni imara kulinganisha na ule wa marafiki “Tazama
jinsi ilivyo vema na kupendeza ndugu wakae pamoja, kwa umoja.”
“Ni kama mafuta mazuri kichwani yashukayo mpaka upindo wa
mavazi yake” (Zab 133:1-2). Wavulana wenye dada zao wanajifunza
kuwatendea wasichana na wanawake kwa heshima kama ambavyo wangependa dada
kutendewa.
Wasichana wenye kaka wanajifunza kutambua ukamilisho wa
wanaume na wanawake wote wakiwa wameumbwa kwa mfano wa Mungu.
Sababu ya sita
Pata mtoto ili wewe na wazazi msibaki wapweke uzeeni
Watu wenye watoto hawahitaji kuwategemea watu wasiowajua
katika uzee wao. Watoto pia watakuwa wazazi wa wajukuu wako. Wajukuu huleta
furaha uchangamfu na kicheko wakati huo huo, wanakupatia nafasi ya usingizi
mzuri. “Wana wa wana ndio taji ya wazee, na utukufu wa watoto ni baba zao” (Mith
17:6).
Sababu ya saba
Pata mtoto kwa vile watu ndio
rasilimali kuu.
Binadamu wamejaliwa zawadi ya akili na utashi. Binadamu anao
uwezo wa kupata majibu kwa matatizo mbalimbali yanayotokea. Watu wasiokuwa na
watoto lazima wakumbuke kuwa daktari aliyetokana na wazazi wengine, ndiye
atakayeweza kusalimisha maisha yao wanapohitaji matibabu.
Ni wazazi wa watoto wengi ndio watakaoweza kuzima moto nyumba
yao inapoungua. Mhandisi wa reli atatoka katika familia ya watoto wengi.
Sababu ya nane
Pata mtoto achangie uchumi.
Familia zenye watoto ni kama mafuta kwa uchumi, ununuzi wa
nyumba, magari na wanachuo wa vyuo mbalimbali. Bila vijana kuingia katika
ajira, mifumo ya usalama na huduma za jamii huanguka.
Bila watoto wa kusoma, walimu hawana kazi, viwanda vingi
hutegemea watu kuviendesha. Bila watu, hatimaye uchumi huanguka. “Mkeo atakuwa
kama mzabibu uzaao nyumbani mwa nyumba yako, wanao kama miche ya mizeituni
wakiizunguka meza yako. Tazama, atabarikiwa hivyo yule amchaye Bwana” Zab
128:3-4.
Sababu
ya tisa
Pata mtoto ili kukabiliana na ukame wa watu duniani
Yeyote aliyesafiri kutoka Pwani hadi Pwani ya Marekani na
kuona mapori yasiyokuwa watu atagundua kuwa nchi hiyo haina mrundikano wa watu.
Na kwa kweli watu wote wa dunia wangeweza kuishi katika Jimbo la Texas, katika
vyumba vya familia ya wastani, wakawa na sehemu za mapumziko mbele na nyuma ya
nyumba…viwango vya vizazi vinaporomoka kote duniani watu wa dunia hawataweza
tena kujizalisha kwa mara mbili.
Kama viwango vya kizazi
vitabaki vilivyo, idadi ya watu itafikia kilele katikati ya mwaka karne hii na
kisha, kuanza kupunguka bila uwezekano wa kuzuia. Tatizo letu la muda mrefu sio
watu wengi, bali watoto wachache. Kuwa na mtoto mwingine kutasaidia kuondaa
tatizo la uhaba wa watu.
Sababu ya kumi.
Pata mtoto usaidie kuwa na watakatifu wengi mbinguni.
Mtoto ambaye wewe na mwenzi wako mmempokea kwa mikono miwili
kutoka kwa Mungu, ameumbwa ili arudi kwake Mungu baada ya maisha ya hapa
duniani, aishi milele mbinguni na Mungu.
Bwana wetu alisema, zipo nafasi tele kwa roho zetu huko
mbinguni. Hakuna tatizo la msongamano wa watu huko mbinguni.
Kaka na dada zake, wazazi wake na familia yote. Uhai wake
wote huwa zawadi kwa watu wote ambao watoaji wa uhai na ambao wanalazimika kuonja
uwepo wake, ushiriki wake katika maisha yao na mchango wake katika mema na kwa
jumuiya ya wanafamilia’.
Kwa kadiri jamii inavyokuwa na watoto wengi, ndivyo hivyo
jamii hii inavyokuwa ya watu wateteao uhai na ndivyo itakavyokuwa rahisi kupiga
vita dhidi ya uovu wa utoaji mimba.
*Makala hii imetafsiriwa kutoka
kipeperushi cha POPURATION RESEARCH ISTITUTE (PRI)
Shirika hili, PRI lilianzishwa mwaka
1989 na Steven Mosher, akateuliwa kuwa Rais wake mwaka 1995.
Malengo makuu ya kuanzisha shirika hili yalikuwa ni pamoja na
kupigania watu, kukanusha nadharia kuwa, idadi ya watu inakwenda kasi kuliko
uwezo wa kiuchumi na kufichua ukiukwaji wa haki za binadamu katika programu za
uzazi wa mpango.
Mengine ni kudumisha mitazamo ya utetezi wa watoto na familia
kimataifa, kulinda familia na kuongea juu ya haki za watoto katika nafasi
yoyote ipatikanayo pamoja na kuziua ueneaji wa utoaji mimba, vidhibiti mimba na
kufunga kizazi kunakofanywa na Serikali kwa dhana ya udhibiti wa idadi ya watu,
badala yake, kusemea programu zinazofanya wanyonge wawe vichocheo vya maendeleo
yao.
Kanisa Katoliki lapania kuleta maendeleo Zanzibar
Lilian Timbuka na Peter Dominic
PAMOJA na ugumu uliopo katika mustakabari na mchakato
mzima wa Uinjilishaji wa Kanisa Katoliki visiwani Zazibar bila kujali itikadi,
juhudi na mikakati ya kanisa hilo inaashiria nyota njema ya ukombozi wa maisha
ya kiroho na kijamii kwa wananchi wa visiwani humo.
Kanisa
hilo hilo ambalo limekuwa shabaha ya hujuma zinazofanywa na watu wanaotaka
kutekeleza matakwa yao kiimani na kisiasa, limekuwa na uhusiano mzuri kwa watu
wote.
Pamoja
na hujuma hizo, kanisa linasimamia na kuendesha miradi mbalimbali ya maendeleo
ikiwa ni pamoja na afya, elimu na malezi ya jamii, ambayo inawalenga watu wote
bila kujali itikadi ya mtu.
“Walio
mbali na Zanzibar, wanajua sisi tuna hali mbaya sana kimahusiano na kiusalama.
Ukweli ni kwamba si watu wote wana nia
mbaya na Kanisa, kuna watu wachache ambao wanatufanyia hujuma, hawa wanaendesha
mihadhara na kukashfu ukristo. Lakini kwa ujumla wazanzibar ni watu wazuri
mno,” anasema Askofu wa Jimbo Katoliki la Zanzibar Mhashamu Agustino Shao.
Miradi
ya kijamii inayoendeshwa na kanisa, ni kielelezo tosha cha dhamira ya kanisa
kuwasaidia na kuleta maendeleo kwa wananchi wa Zanzibar.
Moja
ya huduma za kijamii zitolewazo na Kanisa visiwani humo, ni kituo cha wazee
wasiojiweza kilichopo eneo la Welezo, ambacho kinaendeshwa na Masista wa
Shirika la Damu Takatifu ya Yesu kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi
Zanzibar.
Kituo
hicho chenye majengo manane, kinapambwa na wazee ambao huketi barazani
wakibadilishana mawazo, wakati vikongwe wenye nguvu bado hukaa wakisuka mikeka
ingawa wenye umri mkubwa zaidi husikika wakikohoa wakiwa vyumbani mwao.
Wazee
hao hususani wasio na ndugu wa kuwahudumia, wanapata mahitaji muhimu ya
kumalizia kipindi kilichosalia cha uwapo wao hapa duniani kabla ya kuitwa na
Mwenyezi Mungu, wakiwa salama na matumaini.
Kwa
Mujibu wa msimamizi Mkuu wa Kituo cha Welezo Sista Mary Theresina Ndoro (C.R.S)
wa Shirika la Masista wa Damu Takatifu ya Yesu, anasema kituo hicho chenye idadi ya wazee 66 ambapo
wanaume wako 49 na wanawake 17, kinaendeshwa kwa ushirikiano wa Shirika lake na
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Sisita
Theresina anasema, wamekuwa wakitunza wazee wenye umri mkubwa, ambapo alisema,
mzee ambaye ana umri mkubwa zaidi ana miaka 112, na mwenye umri mdogo ni yule
aliye na umri wa miaka 70 hivi sasa.
kihistoria
kituo hicho kilianzishwa na Kanisa Katoliki Mwaka 1911 na Wamisonari wa Shirika
la White Fathers, kikikusudia kuwahudumia watu waliokuwa na ugonjwa wa ukoma.
Hata
hivyo kituo hicho kilitaifishwa na Serikali mara baada ya mapinduzi ya Zanzibar
kutokea, na kuwafanya wamisionari waliokuwa wakikisimamia kuondoka na kukiacha
mikononi mwa serikali. Mwaka 1982
serikali ilikiteua kuwa kituo cha kulelea wazee wasiojiweza.
Sisita
Theresina anasema kuwa, serikali ya mapinduzi iliendelea kuwahudumia wazee
wasiojiweza kupitia kitengo cha Ustawi wa Jamii. Hata hivyo anasema tofauti na
hali ilivyokuwa awali, serikali haikuweza kumudu mazingira ya kuwahudumia wazee
hao hali iliyochangia kuwaweka wazee
katika hali mbaya.
Anasema
hali hiyo ilichangiwa na kuchakaa kwa majengo, kukosekana kwa wafanyakazi wa
kutosha baada ya serikali kushindwa kuwalipa mishahara, ukosefu huduma muhimu
ikiwa ni pamoja na maji, umeme na vifaa vya kutosha kuwahudumia hali
iliyowafanya wazee wasioge kwa muda mrefu.
Serikali
iliamua kurejesha kituo hicho kwa Kanisa Katoliki katika miaka ya 1990 ili
kuboresha huduma za kituo. Shirika la Damu
Takatifu ya Yesu lilianza utaratibu wa
kukarabati na kuboresha huduma kwa makubaliano maalum ya mkataba wa
miaka miwili miwili.
“Kila baada ya miaka miwili tulitiliana saini ya kuanza mkataba mpya na
serikali, kwa vile tulihofia kushindwa kutokana na gharama kubwa za
uendeshaji,” alibainisha Sista Theresina.
Sista
Theresina anabainisha kuwa, makubaliano yaliyopo kati ya Kanisa Katoliki
Zanzibar na serikali kwa hivi sasa, ni kwa serikali kuendelea kulipa mishahara ya wafanyakazi ambao idadi yao
inafikia 66, walinzi 14 na wahudumu wa kawaida pamoja na Muuguzi mmoja ambaye
huwahudumia wazee kwa matibabu kwa kushirikiana na Sista Theresina ambaye pia kitaaluma ni muunguzi.
Anasema
kuwa, Daktari mmoja kutoka serikalini hufika na kuwahudumia wagonjwa na wale
wanaoshindikana hupelekwa katika hospitali ya Rufaa ya serikali ya Mnazi
Mmoja. Akielezea namna kituo hicho
kinavyopokea wazee, alifafanua kuwa, serikali ya Zanzibar huwatumia Masheha kuwakusanya wazee
wasiojiweza katika maeneo yao wakizingatia wasio na ndugu kisha huwaleta
kituoni hapo.
Akizungumzia
gharama za uendeshaji, anasema kuwa awali serikali ilikuwa ikitoa posho kwa
wazee ikiwa ni jumla ya shilingi 500,000
kwa mwezi, ingawa baadaye ilionekana isingeweza kukidhi mahitaji ya kila
mzee.
Hata
hivyo anasema, kulingana na kupanda kwa gharama za mahitaji, hivi sasa serikali
inatoa kiasi cha shilingi Milioni 2 kwa mwezi ingawa bado kiwango hicho ni
kidogo.
Kuwepo
kwa masista wa shirika hilo, imeonekana ni faraja kwa wazee hao kama
wanavyobainisha. “Najisikia faraja kuwepo hapa, tunafurahia huduma zinazotolewa
na masisita najisikia nipo na ndugu zangu,” alisema Mzee Omari Mtiro (70). Naye
Mzee Juma Bakari ambaye hakukumbuka umri wake, alisema, “mwili ulikuwa
ukitetemeka, sasa najisikia afadhari, tatizo langu macho, lakini ninaimani hawa
ndugu zangu watanisaidia tu, wana moyo sana Mungu awabariki sana.”
Mzee
Raphael Daima (70) na Mzee Musa Almas (87) wameshukuru huduma zinazotolewa na
kituo hicho tangu kuwepo kwa uongozi wa Shirika la Damu Takatifu ya Yesu. Sisita
Theresina alisema kuwa, umri walionao wazee kama hao, wanahitaji kuhudumiwa
kama watoto wadogo.
Sisita
Theresina alisema pamoja na wingi huo wa wazee hakuna tishio la vifo ambapo
wastani unaonesha kwamba vinaweza kutokea vifo 12 kwa mwaka.
Akiongelea
suala la Elimu na Mikakati ya Jimbo Katoliki la Zanzibar Mhashamu Shao
aliwaambia Waandishi wa makala haya kuwa, hivi sasa Kanisa linamkakati wa
kueneza elimu bora zaidi kwa jamii.
Alisema
tayari kanisa limekwisha jenga shule za msingi na sekondari ambazo kwa hivi
sasa zinachukua wanafunzi kama kawaida.
Shule
ya msingi ambayo hivi sasa inaonekana kuwa ni shule ya kisasa zaidi kuliko
shule zingine mjini Unguja, ni ile ya Mtakatifu Fransis Maria Libermann iliyo
katika Kitongoji cha Tomondo, inayochukua wanafunzi toka wale wa darasa la
awali, mpaka darasa la saba, shule hiyo ina uwezo wa kuchukua wanafunzi 600 kwa
sasa.
Katika
uchunguzi uliofanywa na waandishi, imebainika kuwa karibu asilimia 80 ya
wanafunzi wanaosoma shuleni hapo, ni wa dini ya kiislamu, hali ambayo inaonesha
wazi kuwa Kanisa limedhamiria kutoa huduma za jamii kwa watu bila kubagua.
Shule
hiyo ya Mtakatifu Fransis Maria Libermann, ilianzishwa mnamo mwaka 1997,
ikiwa ni shule ya chekechea, ambapo
watoto walikuwa wakisomea chini ya Mwembe na kukalia vipande vya magogo ya
minazi kama madawati. Shule ilianzishwa
kwa msaada wa Askofu Mstaafu wa Jimbo la Zanzibar wakati huo, Mhashamu Bernard
Nganviliyao.
Majengo
yaliyopo hivi sasa, yamejengwa chini ya Uongozi wa Mhashamu Agustino Shao, kwa
kushirikiana na wafadhiri mbalimbali wa nje na ndani, akiwamo Askofu Donald
Wuerl.
Shule
hiyo ambayo ni ya kutwa na bweni, tayari ina wanafunzi 24 wa bweni. Shule
inauwezo wa kulaza wanafunzi 50 hivi sasa.
Akijibu
swali juu ya shule kuwa na wanafunzi wengi wa Kiislamu kuliko Wakristo Mhashamu
Shao alisema;
“Lengo
la Kanisa ni kutoa huduma kwa watu na si kwa kuangalia huyu ni muamini wa dini
ipi, au mkazi wa wapi. Kazi yetu kubwa ni kueneza Injili kimwili na kiroho, na
ikiwa ni pamoja na kutoa huduma muhimu kwa jamii kama hii ya Elimu.”
Pia
Mhashamu Shao alibainisha kuwa, Wakristo wengi waishio visiwani humo wamekuwa
wakishindwa kuwapeleka watoto wao shule, kwa kuwa na matumaini ya kurudi
Tanzania Bara muda wowote.
“Hapa
visiwani Waamini wengi wa Kikristo ni wale ambao wamekuja kutoka bara, kwa hiyo
ukimwambia mpeleke mtoto shule, atakwambia mimi sikai sana hapa, nimekuja
kutafuta maisha kwa muda tu, nikifanikiwa narudi kwetu Shinyanga au Tabora”
alifafanua Mhashamu Shao.
Hata
hivyo Mhashamu Shao alibainisha pia kipato kidogo walichonacho Wakristo
kinachangia kwa kiasi kikubwa kushindwa kusomesha watoto, kutokana na kukosa
ada.
Pamoja
na machungu ya kupigwa mabomu kwa mali za Kanisa na watu wasiotaka maendeleo
visiwani humo, ikiwa ni pamoja na kulipuliwa kwa basi la Shule la Mtakatifu
Fransis Maria Libermann na Kanisa, kulikofanyika hivi karibuni, bado Kanisa
Katoliki halijakata tamaa ya kutafuta maendeleo ya wananchi wake visiwani humo.
Jimbo
la Zanzibar hivi sasa linaendelea na ujenzi wa shule ya Sekondari katika kijiji
cha Cheju kilicho nje kidogo ya mji wa
Zanzibar, ambayo inatarajia kuanza kufundisha masomo kamili ya sekondari katika
siku chache zijazo.
Shule
hiyo ambayo ilianzishwa rasmi mnamo April 1999, kwa sasa inajulikana kwa jina
la Cheju Wisdom Centre, ikiwa ni kituo cha malezi ya Vijana shule hiyo
imekamilisha baadhi ya majengo, na inachukua wanafunzi wanaojiandaa kwa masomo
ya sekondari wa kike na wa kiume.
Akizungumza
shuleni hapo, Mkuu wa Shule hiyo, Padre Damas
Mrina alisema kuwa, shule hiyo ambayo ina jumla ya wanafunzi 46,
wasichana 32 na wakiume 14, hivi sasa inawaandaa vijana kwa muda wa mwaka mmoja
kabla ya kuwatawanya katika shule za sekondari zilizoko Tanzania Bara, zikiwamo
zile za Kiraeni, Kifungiro, Marangu, Kibosho,
Sila na shule ya Mtakatifu Fansis ya Mbeya.
“Shule
yetu mpaka hivi sasa iko katika ule mtindo wa chuo cha malezi, vyuo ambavyo
hata wenzetu waislamu wanavyo,” alisema Padre Mrina.
Hivyo
aliainisha kuwa, kwa sasa shule inawafundisha wanafunzi masomo ya Kiingereza na
Hisabati ambayo wameyafanya kama masomo ya msingi. “Tunafundisha pia masomo
mengine ikiwemo Jiografia, Elimu ya Biblia, Siasa, sayansi na Afya,” alisema
Padre Mrina.
Alisema
masomo yote hayo hufundishwa kwa kutumia lugha ya kiingereza na Kiswahili.
Aliongeza kuwa, lengo kuu la shule hiyo hivi sasa ni kuwajengea uwezo wanafunzi
wa kuweza kuyamudu masomo ya sekondari ambayo huyasoma baada ya kutoka hapo.
Shule
hiyo ambayo iko umbali wa kilomita 30 toka katikati ya Mji wa Zanzibar,
huchukua wanafunzi kutoka Tanzania Bara na Visiwani. Na hivi sasa iko katika kampeni ya kutaka
kuiwezesha kuwa sekondari kamili ya bweni. Na maandalizi ya ujenzi wa mabweni
unaendelea.
Mbali
ya masomo ya darasani, shule hiyo pia inafundisha elimu ya kujitegemea. Tayari
shuleni hapo kuna miradi ya ufugaji wa ng’ombe wa maziwa, mbuzi, na nguruwe
wapatao 63.
Padre
Mrina alisema mradi wa nguruwe huingiza kiasi cha shilingi Laki 5 kwa mwaka, na
nguruwe hao huwauza katika Hoteli za kitalii zilizomo visiwani humo.
“Hawa
nguruwe wanatuingizia kipato, hasa katika sikukuu za mwaka, kama zile za Pasaka
na Krismasi,” alisema Padre Mrina.
Shule
hiyo pia inamiliki shule ya awali, iliyopo ndani ya majengo ya shule.
Kanisa
katoliki visiwani linajishughulisha pia na utoaji wa elimu ya UKIMWI kwa
kuanzia ngazi ya vitongoji mpaka mkoa.
Akizungumzia
utoaji wa elimu hiyo, Mhashamu Shao alisema Zanzibar hivi sasa hakuna NGO
yoyote inayotoa elimu ya UKIMWI kwa kina kama Kanisa Katoliki.
Alisema
Kanisa hivi sasa limekuwa mstari wa mbele na tayari wafadhiri wa mfuko wa Global
Fund, wamelitambua hilo.
Mhashamu
Shao anasema tayari Jimbo lake limekwisha jenga vituo kadhaa vya Afya,
vinavyoendelea kutoa huduma ya afya kwa hivi sasa, ikiwa ni pamoja na
kuwahudumia wagonjwa walioathirika na virusi vya ukimwi.
Alisema
kisiwani Pemba jimbo limejenga zahanati Tatu, na Hospitali moja ambayo hutoa
huduma ya ukunga kwa wanawake wajawazito.
“Cheju
tayari tumejenga Zahanati, lakini bado haijaanza kufanya kazi kutokana na
ukosefu wa wafanyakazi wenye sifa,” Mhashamu Shao alisema.
Alisema
lengo la Kanisa ni kutoa huduma zenye ubora na si za kubahatisha,
japoakuwa walipoanza kujenga zahanati
hizo, walipata kipindi kigumu toka kwa waamini wenye itikadi tofauti na ya
wakristo, kwa madai ya kuwa kamwe wasingeweza kutibiwa katika zahanati hizo
ambazo walidai sindano zitumikazo zina nguruwe.
“Lakini
taratibu sasa wameelewa, sasa hivi ukitaka kufanya sensa ya wagonjwa wanotibiwa
katika zahanati zetu kwa asilimia kubwa ni wale waliokuwa wanatupiga vita hapo
awali,” alibainisha Mhashamu Shao.
Akizungumza
na KIONGOZI katika Zahanati ya Mtakatifu Camillius Mission, iliyo katika
Kitongoji cha Tomondo Zanzibar, Muuguzi Mkuu
Sista Imelda Nafun N.O wa Shirika la Evangelising Sister’s,
alisema kuwa, kituo hicho kinapokea wagonjwa wa aina mbalimbali ambao hupata
huduma kila siku.
Sista
Imelda aliongeza kuwa, zahanati hiyo inawatibu pia watu wanaoishi na virusi vya
UKIMWI kutoka kundi la (ZAFA+), ambapo aliainisha kuwa wagonjwa hao hupatiwa
dawa na gharama za matibabu hulipwa na ofisi ya Askofu wa Jimbo la Zanzibar.
Aliongeza
kuwa, kwa hivi sasa zahanati yake haina vipimo vya maradhi ya UKIMWI, bali
vipimo vyote hufanyika katika Hospitali ya Serikali ya Mnazi Mmoja.
Zahanati
hiyo ambayo iko ndani ya eneo la shule ya Mtakatifu Fransis Maria Libermann,
mbali ya kuwahudumia waathirika, pia
imekuwa ikitoa huduma za vipimo vya maabara, kliniki kwa akina mama wajawazito
na watoto, na hutibu maradhi ya kawaida kwa jamii ya eneo hilo, na wanafunzi wa
shule ya Mtakatifu Fransis, kwa gharama za shule.
Tofauti
na Tanzania Bara, waathirika wa ugonjwa wa ukimwi, wamekuwa wakitengwa na
kubaguliwa na jamaa zao. Huduma zinazotolewa na kanisa zimekuwa faraja kwa
waathirika hao ambao sasa wanaishi kwa matumaini.
Pamoja
na misukosuko inayoendelea kuliandama Kanisa Visiwani humo hivi sasa kwa
kuharibiwa mali zake ambazo ziko kwa faida ya jamii ya watu wa visiwani,
Mhashamu Shao alisema kamwe hawatakata tamaa katika kutafuta maendeleo.
“Pamoja
na kuwa wanatutukana lakini wanapoona kuwa kuna dini nyingine pia ambayo inafanya mambo mazuri, basi wanaelewa
maendeleo ni nini,” alisema.
Alisema
suala la baadhi ya watu wanaodai
wakristo waondoke Zanzibar, eti hawana kazi, wanakosea, alisema
“Wakristo wana kazi kubwa na moja wapo ni kama hii ya kutafuta maendeleo ya
visiwa hivi.”
Hata hivyo katika kutafuta maendeleo ya kweli ya visiwa hivyo, jumuiya ya Zanzibar kwa hivi sasa, haina budi kuonesha hali ya mshikamano, upendo na umoja, ili kujenga na kuendeleza amani kwa maendeleo ya wananchi wake, badala ya kurudi nyuma kwa kufanya uharibifu kwa kile kilichotengenezwa kwa faida ya kizazi kijacho.
Vita dhidi ya mila potofu ihusishe jamii za wahamiaji
Na Edna Ndejembi
MIAKA zaidi ya 10 iliyopita, nilishuhudia kioja kwenye
Hospitali ya Serikali ya Mkoa wa Dodoma ambapo, mama mmoja mjamzito alishindwa
kujifungua kwa vile sehemu yake za siri zilikuwa zimeshonwa.
Muuguzi
Mkuu kwa wakati huo, Ruth Kalanje, alilazimika kuwasihi mama na ndugu wa
mjamzito huyo, kumfumua mara moja mgonjwa wao ili aweze kujifungua salama
lakini, hawakumsikiliza.
Tulielezwa
kuwa, mjamzito huyo mwenye asili ya Kisomali alikuwa amefanyiwa ukeketaji na
kisha, kuzibwa sehemu za siri, (INFIBULATION).
Aina
hii ya ukeketaji inayosababisha maumivu makali, ni maarufu sana katika nchi za
Sudan, Somalia na Djibouti
Mama
yake ambaye hatimaye alimfumua binti yake baada ya kutishwa kuwa angepelekwa
polisi, alitueleza kuwa binti yake huyo alikeketwa alipokuwa na umri wa miaka
minane na kuzibwa kwa kushonwa sehemu zake za siri.
Anasema,
alipofikisha miaka 16, aliolewa na hivyo kufumuliwa ili kumwezesha mumewe
kumwingilia.
Hata
hivyo, msichana huyo alilazimika kushonwa tena kwa vile mumewe aliyekuwa dereva
wa magari makubwa, alikuwa anasafiri kwa muda mrefu na kwamba, hadi muda huo
hakuwa amepata ujauzito.
Njia
hiyo inadaiwa kuwa, ilikuwa inasaidia kumfanya mwanamke aliyeolewa asiweze
kutoka nje ya ndoa yake, hali inayoweza kumsababisha kupata ujauzito
Mama
huyo anasema, kilichomfanya akatae kumfumua tena binti yake, ni woga aliokuwa
nao kwa vile angeshindwa kumjibu mkwewe ni kwa jinsi gani mwanae kapata
ujauzito, wakati ameshonwa.
Akadai
kwamba, binti huyo licha ya kuzibwa sehemu za siri, ajabu ni kwamba binti yake
alitembea na mwanaume mwingine na kwa namna ya ajabu, akapata mimba.
Aina
nyingine ya ukeketaji, ni ile inayohusisha ukataji wa sehemu kubwa bila ya
kuziba. Hii hufanyika nchini Ethiopia, wakati aina ya tatu inayofanywa kwenye
nchi nyingi zaidi ikiwemo Tanzania, inahusisha ukataki wa ncha tu (excision).
Huko
Ulaya ambako ukeketaji ulikuwa unaruhusiwa kisheria hadi mwaka 1985 kabla ya
kuzuiwa, ulifanyika kwa lengo la kuzuia michezo ya usuguaji hasa miongoni mwa
watoto.
Wazazi
walikuwa huru kuwapeleka watoto wao hospitalini na kufanyiwa ukeketaji aina ya excision
kama tiba dhdi ya usuguaji.
Lakini
pamoja na Bara hilo la Ulaya kupiga vita kitendo hicho, hivi majuzi Waziri wa
Mambo ya Ndani wa Uingereza, David Blunkett, ametangaza sheria mpya dhidi ya
ukeketaji, baada ya vitendo hivyo kushamiri nchini humo.
Amesema
sheria hiyo itawawabana wazazi wanaowapeleka watoto wao nje ya Uingereza ili
kuwakeketa.
“Kwetu
hakuna mila, matibabu au sababu yoyote inatakayoweza kuhalalisha ukeketaji
ambao unawasababishia maumivu makali mabinti zetu,” alisema Blunkett na
kuongeza kuwa, inakadiriwa kuwa wanawake 74,000 waliohamia Uingereza kutoka
Afrika, wamekeketwa.
Jitihada
za vita dhidi ya ukeketaji pamoja na mila potofu ambazo ni za unyanyasaji dhidi
ya mwanamke, zinazofanywa na mashirika yasiyo ya kiserikali hapa nchini, hazina
budi kusambazwa kwenye jamii zote, badala ya kuhusisha tu, wananchi walioko
vijijini.
Kama
inavyoeleweka, jamii za Kisomali hazikubali kuacha vitendo vya ukeketaji kwa
kuwa ni mila inayotukuzwa sana, na ndio maana kwa kuogopa kujulikana wakiwa
nchi zilizopitisha sheria kali kama Uingereza, hudiriki kuwapeleka mabinti zao
kukeketwa nchi za nje.
Vita
dhidi ya ukeketaji na mila nyingine potofu kama ndoa za utotoni katika nchi
yoyote ile, haiwezi kufanikiwa endapo jamii zote husika hazitashirikishwa.
Ukeketaji
una madhara mengi na kubwa zaidi, ni kumsababishia maumivu na kuvuja damu
nyingi endapo kovu litatanuka na kuchanika hasa wakati wa kujifungua, au
kusababisha mtoto ashindwe kutoka hadi hapo upasuaji unapofanyika.
Jamii
sharti ijue hilo na isiuone ukeketaji kama njia ya kujipatia kipato au basi
kwamba, ni ufahari kama asemavyo Mama Shufaa Mahfudh (61); ngariba wa Kisomali
ambaye amekuwa akifanya kazi ya ukeketaji kwa miaka mingi.
“Mimi
silipwi pesa, wala sitaki kulipwa chochote; jamii yetu imenipa heshima kubwa
sana ambayo ninajivunia kwani sio kila mwanamke anaweza kuruhusiwa kufanya
kitendo hiki ambacho kinawaweka wasichana kwenye hali inayokubalika,” anasema
Bibi Shufaa.
Bibi
Mahfudh, mkazi wa eneo la Makola, linalokaliwa na jamii kubwa ya Kisomali
Manispaa ya Dodoma anasema kuwa, huwakeketa watoto wa kike wanapofikisha umri
wa kuanzia miaka 5 hadi 6 na kwamba, baada ya kuvunja ungo, hushonwa hadi pale
watakapoolewa.
Ushonaji
huo kwa mujibu wa Bibi Mahfudh, hufanywa ili kuwazuia wasichana kutojamiiana
kabla ya kuolewa, na kwa wale walioolewa, huwazuia wasitoke nje ya ndoa pindi
waume zao wanapokuwa mbali nao.
Nilipomuuliza
kuhusu wasichana au wanawake walioshonwa kubeba mimba, Bibi Mahfudh alisema
kuwa, kitendo hicho huweza kutokea iwapo mshonaji hatakuwa ameziba nafasi zote.
Hata
hivyo uchunguzi uliofanywa kwenye jamii hiyo umeonesha kuwa, licha ya kushonwa,
bado wanawake na wasichana wengi hujihusisha na ngono kama kawaida.
Aidha,
ndoa za utotoni ni jambo la kawaida kwenye jamii hiyo na kwamba, watoto
huhamishwa kutoka wilaya na hata mkoa mmoja hadi mwingine kwa lengo la kuolewa.
“Watoto
watatu wamepelekwa nchi jirani mwaka huu kwenda kuolewa. Hivi sasa wote
wanaweza kuwa wamekwishabeba mimba,” Bibi Mahfudh alieleza na kuongeza kuwa,
watoto hao ambao hawakuwahi kusoma, walikuwa na umri wa chini miaka 15.
Vita
dhidi ya mila potofu inapaswa kuhusisha watu wote waishio ndani ya mipaka ya
nchi yetu, bila ya kubagua wala kuogopa jamii wanazotoka, ili mradi wako nchini
Tanzania ambapo mikakati na sheria dhidi ya vitendo hivyo zinatekelezwa.
Hivi
karibni mtandao dhidi ya mila potofu – AFNET, ulitaarifu kuwa unafanya mpango
wa kuwawezesha kiuchumi mangariba mkoani Dodoma waachane na vitendo hivyo,
kuangalia njia itakayowafanya mangariba kama Bibi Mahfudh ambao hawafanyi
shughuli hiyo kwa malipo kuachana na vitendo hivyo.
KONA YA SHERIA
Ijue sheria
ya ugaidi
Na Dotto Shashi
Matukio ya ugaidi yamekithiri sana hivi sasa. Ni ukweli usiopingika
kuwa amani ya Dunia haipo tena, kwani limekuwa ni jambo la kawaida kila kukicha
kusikia matukio ya mauaji ambayo ni ya kujitoa mhanga au hata bila kujitoa
muhanga, lakini matukio yote hayo yamekuwa yakiwalenga watu, na mbaya zaidi
waathirika wengi ni watu ambao hawana hatia yeyote kwa Mwenyezi Mungu na hata
kwa magaidi wenyewe.
Katika
mada ya toleo hili, tutaiangalia sheria ya kuzuia ugaidi iliyopitishwa na Bunge
la Tanzania mwaka 2002.
kwa
kuwa sheria hii ya ugaidi ina mambo mengi sana yaliyowekwa kisheria, na kwamba
watu wengi sasa kwa kiasi kikubwa tayari wana upeo wa kutosha wa kuuelewa
ugaidi ni nini, toleo hili tutaitazama sheria hii katika eneo linalohusu watu
ambao wanatabia ya kuficha magaidi au taarifa zozote, ambazo zinaweza kusaidia kupatikana
kwa watuhumiwa wa ugaidi.
Sheria
ya kuzuia ugaidi namba 21 ya 2002, yaani ‘The prevention of Terrorism
Act, 2002’, imeweka vifungu vya sheria vinavyomfanya mtu kuwa na wajibu wa
kutoa taarifa inayohusu ugaidi.
Sehemu
ya nane ya sheria hiyo, yaani ‘Part Viii’, vimeorodheshwa vifungu
ambavyo vinazungumzia suala zima la wajibu wa mtu katika kutoa taarifa ya
ugaidi.
Kifungu
namba 40 kifungu kidogo cha kwanza (1) kinaeleza kuwa, kila mtu
ambaye ana taarifa ambayo inaweza kusaidia; (a) Kuzuia kitendo chochote cha
ugaidi ambacho kinaweza kufanywa na mtu au (b) Kusaidia kukamatwa kwa mtu au
mashitaka yake chini ya sheria hii.
Atatakiwa
mara moja kutoa taarifa hiyo kwa Askari polisi ambaye ana cheo kisicho kuwa
chini ya cheo cha Mrakibu msaidizi wa
Polisi, (Assistant Superintendent of Police) au mkuu wa kituo cha
Polisi.
Katika
kifungu kidogo cha pili (2) imeelezwa kwamba, hakuna kitu chochote
katika kifungu kidogo cha kwanza ambacho kinataka utoaji wa habari ambazo zina
kinga (Information protected by privilege).
Kifungu
kidogo cha tatu (3) kinasema, “mtu yeyote hawezi kushitakiwa aidha kwa
kesi ya jinai au kesi ya madai kwa kutoa taarifa yoyote kwa nia nzuri au katika
mazingira kama inavyoelezwa katika kifungu kidogo cha kwanza(1).”
Kifungu
kidogo cha nne (4) kinasema kuwa, mtu yeyote ambaye itathibitika kushindwa
kutekeleza matakwa au wajibu wake kama ilivyoelekezwa katika kifungu kidogo cha
kwanza, atakuwa amefanya kosa la jinai, na hivyo akitiwa hatiani atatakiwa
kwenda kutumikia kifungo jela cha miaka isiyopungua miwili na au isiyozidi
mitano (Tafsiri ya kifungu hiki ni ya mwandishi mwenyewe).
Tunaona
katika adhabu iliyotolewa na sheria hii, kuwa kosa la kushindwa kutoa taarifa, halina
adhabu ya faini kama ilivyozoeleka kwa wengi katika makosa mengi ya jinai,
hivyo mtu akipatikana na hatia katika kosa hili ajue yeye ni mtu wa kifungo.
Baada
ya kuona kosa la mtu kushindwa kuwajibika katika kutoa taarifa za ugaidi kama
anavyotakiwa katika kifungu namba 40(1).
Tuangalie
kifungu kingine ambacho kina mtaka mtu kuwa na wajibu wa kutoa taarifa kwa
Polisi inayohusu mali za gaidi au mali zinazomilikiwa kwa niaba ya gaidi au
kundi la magaidi ambazo zimetumika kwa kutendea kosa la ugaidi.
Kifungu
namba 41 kifungu kidogo cha kwanza (1), kinaeleza kwamba; kila mtu
atalazimika kutoa taarifa mbele ya Afisa wa Polisi mara moja ya;
(a) Umiliki wake au
kukabidhiwa kwake mali yoyote ambayo kwa ufahamu wake ni mali ambao ni ya gaidi
, au inayotunzwa kwa niaba ya kundi la magaidi.
(b) Mipango ya utekelezaji
au inayokusudiwa kutekelezwa kuhusiana na mali yoyote kama ilivyoelezwa katika
kipengele cha (a) hapo juu.
Neno
Afisa wa Polisi kama lilivyotumika katika kifungu cha 41 lina maana, isipokuwa
kama itaelezwa vinginevyo na Afisa wa Polisi mwenye cheo cha Mrakibu Msaidizi
wa Polisi, hii ni kwa mujibu wa kifungu namba 3 cha sheria hii ya Ugaidi.
Tukiendelea
na kifungu cha 41, tunaona kuwa katika
kifungu kidogo cha pili (2), Taasisi za Fedha nchini zimetakiwa kutoa ripoti
kila baada ya miezi mitatu, mbele ya Afisa wa Polisi au mtu yeyote ambaye
amepewa mamlaka kisheria ya kusimamia na kurekebisha shughuli za Taasisi hiyo
ili kuona endapo Taasisi hiyo;
(a)
Haimiliki au kuwa na Amri juu ya mali yeyote ya kundi la magaidi au;
(b)
Ina miliki na kuwa na Amri juu ya mali ya magaidi, maelezo kuhusu watu
(magaidi), Hesabu za Fedha, na mipangilio inayohusiana na mali hiyo ikiwa ni
pamoja na thamani ya jumla ya mali hiyo.
Kifungu
kidogo cha tatu (3) kinaeleza kuwa, kwa nyongeza ya matakwa ya kifungu kidogo
cha pili hapo juu kila Taasisi ya Fedha italazimika kutoa taarifa mbele ya
Afisa wa Polisi ya kila hatua ya shughuli ambazo wana kila sababu ya kuhisi
kuwa hatua hizo shughuli zao zina mwelekeo au zinahusiana na magaidi.
Kifungu
kidogo cha Nne(4) kinasema kuwa, mtu yeyote hawezi kushitakiwa kwa kosa
la jinai au madai kwa kutoa ripoti kwa nia njema, kama inavyotakiwa katika
vifungu vidogo vya (1), (2) au (3).
Mwisho
katika kifungu kidogo cha tano(5), inatolewa adhabu kwa mtu ambaye
atashindwa kutii matakwa ya vifungu vidogo vya (1), (2) na (3).
Na
kwamba adhabu ya kosa hilo ni kifungo cha miezi isiyopungua kumi na mbili jela
(12).
Kwa kumalizia mada hii, ni matumiani yangu kuwa sote tumeona
umuhimu wa kutii sheria hii ya kuzuia ugaidi (Prevention of Terrorism
Act, 2002), kwani bila kufanya hivyo tutakabiliwa na adhabu kali, kama
inavyoelezwa katika sheria hii.
SHERIA ZA KANISA
SAKRAMENTI
YA NDOA: Kan. 1055 – 1165.(17)
Katika Toleo lililopita tuliishia katika kipengele
kinachotaja DARAJA TAKATIFU kama moja ya vizuizi vya Sakramenti ya Ndoa. Kabla
ya kuendelea na mjadala juu ya kizuizi hiki, hebu kwanza tujikumbushe historia
fupi kuhusu sheria ya useja. Endelea
Mafundisho kuhusu useja yanakutwa katika mapokeo ya
Kanisa kama vile, maandishi ya Mababa wa Kanisa: Mt Yohana Christostom,
Tertulliano, Origen, Jerome, Clement wa Alexandria, Eusebiowa Caesarea, Sirilo
wa Yerusalemu, na Gregori wa Nazianzen. Lakini, mafundisho ya kisheria kuhusu
useja wa ki-kanisa yanakutwa katika mafundisho ya Kanisa (magisterium) na basa
ya Kanisa Katoliki ya Magharibi. Kwa namna ya pekee, hatuwezi kusahau mchango
wa mkutano wa Elvira (hispania) wa 306.
Uliwakataza wote waliopokea madaraja makubwa kuendelea
na maisha ya ndoa (DZ 119). Ingawa mkutano huo ulikuwa na baadhi ya majimbo ya
Hispania, majimbo mengine yalifurahishwa na msimamo huo. Yakaidhinisha maazimio
yake, kama vile mkutano wa Arles (314) wa Ancyra (314) wa Roma (386). Hata
Mababa Watakatifu Damaso, Siricio na Innocent waliwataka makrelo kuishi hivyo.
Mikutano mingine ya Kanisa iliyofuata iliyoyakubali
maamuzi hayo ni pamja na Mkutano wa Karthage- Africa (390), Orange Ufaransa
(441) wa Tours-Ufaransa (461), na Turino - Italia (398). Aidha maaskofu katika
majimbo yao waliwahimiza watu wao, kuishi maisha ya useja. Hatuwezi kusahau
mchango wa Gregori VII aliyeishi karne ya 11 ambapo kulikuwa na uozo
wakimaadili na kiroho.
Watawa walikuwa wameacha monasteri na kuoa au kuolewa.
Makleri waliacha huduma za Kanisa na kuoa.
Aliandika barua nyingi na kuwatuma wawakilishi sehemu
mbalimbali za dunia ili kuhimiza suala la useja wa kiKanisa (Delhaye P.,
History of Celibacy, katika, New Catholic Encyclopedia, Vol. III, Jack Heraty
& Associates, Washington, 1967, uk. 369). Alifanikiwa kiasi kikubwa. Mababa
Watakatifu waliofuata walifuata nyayo zake: Urbano II na Callisto II. Mitaguso
ya Kanisa iliendeleza utaratibu huo: Laterano I (1123), Laterano II (1139),
Trenti karne ya 16, Vatikano I (1869-1870) na Vatikano II (PO, 16; PC, 12; LG,
42; OT, 10).
Kumbe, ni kutokana na juhudi hizo zote kwamba
sheria imeweka kanuni zinazohusu useja wa kiKanisa (kan. 227; 1037; 1042 na
1087).
Wajibu
wa kuishi useja unawahusu wale wote wanaoshiriki madaraja matakatifu, yaani,
maaskofu na mashemasi-waseja. Wakivunja sheria hiyo na kufunga ndoa, ndoa hiyo
ni batili (kan. 1087). Zaidi ya hayo, yeyote atakayefunga ndoa hata kama ni ya
kiserikali atavuliwa madaraka yote ya Kanisa (kan. 194) na kusimamishwa kama
ilivyo kawaida (kan. 1394).
Lakini
kwa sababu kubwa sana Baba Mtakatifu peke yake anaweza kumwondolea mtu wajibu
wa kuishi maisha ya useja (kan. 1078, 291) na kuruhusiwa kuoa. Ordinari mahalia
hawezi kumwondolea mklero, hasa padre au askofu, wajibu wa useja (kan. 291).
Wajibu wa useja wa mapadre au maaskofu au mashemasi unaondolewa na Baba
Mtakatifu tu. Kwa maaskofu na mapadre, matayarisho na kesi nzima vinapitia kwa
Idara ya Mafundisho ya Imani na yale ya ushemasi yanapitia kwa Idara ya
Sakramenti. Wakati wa hatari ya kifo, ordinari mahalia anaweza kumwondolea
shemasi wa kudumu wajibu huo.
Nadhiri ya usafi wa moyo shirikani:
kan. 1088.
Sheria
ya Kanisa inasema waziwazi kuwa wale walioweka hadharani nadhiri ya daima ya
usafi wa moyo katika shirika la kitawa hufunga ndoa batili (kan. 1088). Ili ndoa
iweze kuwa batili lazima masharti manne yatimizwe, yaani: nadhiri iwe ya usafi
wa moyo, iwe ya daima, iwekwe hadharani na iwekwe katika shirika la kitawa.
Kizuizi
hiki hakiwahusu wale wanaoweka nadhiri ya muda ya usafi wa moyo au nadhiri ya
binafsi au wanaoweka ahadi ya kutunza usafi wa moyo katika mashirika mengine ya
Kanisa yasiyo ya kitawa. Pamoja na kufunga ndoa batili mtawa anajifukuza
mwenyewe kutoka shirikani (kan. 694;1394) na kuacha huduma zote za Kanisa (kan.
194).
Kizuizi
hiki kinaweza kuondolewa na mamlaka halali ya Kanisa. Ikiwa nadhiri imewekwa
katika shirika la kitawa la kipapa, mamlaka ya kuondoa kizuizi hiki ni Kiti cha
Kitume, yaani, idara inayoshughulikia watawa na mashirika mengine ya Kanisa
(kan. 1078). Uongozi wa Jimbo unaweza kuondoa kizuizi hiki wakati wa hatari ya
kifo tu.
Iwapo
mawasiliano na Uongozi wa Jimbo ni magumu sana na kuna hatari ya kifo, padre
yeyote anayeruhusiwa kufungisha ndoa anaweza kuondoa kizuizi hiki. Hii ni
pamoja na shemasi anayeruhusiwa kufungisha ndoa (kan. 1079 na 1116). Padre
mwungamishi anaweza kuondoa kizuizi hiki wakati wa hatari ya kifo na wakati
akiadhimisha Sakramenti ya Upatanisho na ikiwa kizuizi hiki ni cha siri, yaani,
hakijulikani kwa watu.
Kwa mtawa wa shirika la kitawa la kijimbo, ni Uongozi wa Jimbo unaoondoa kizuizi hiki. Inapotokea sababu maalum (kan. 1079 na 1080) na ikiwa mawasiliano na Uongozi wa Jimbo ni magumu, mapadre au mashemasi walioruhusiwa kufungisha ndoa wanaweza kuondoa kizuizi hiki.
Adhabu ya
kunyonga si suluhisho
Na Charles Misango.
TAIFA hivi karibuni, liliambiwa kuwa watanzania
350 wanasubiri kuuawa kwa kunyongwa, baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya
mauaji na uhaini, kati yao 11 wakiwa ni wanawake.
Ingawa takwimu hizi hazikubainisha idadi ya
watu wanaosubiriwa kunyongwa kutokana na kosa la uhaini na lini walitenda kosa
hilo, dhahiri wengi wao watakuwa wanakabiliwa na makosa ya mauaji.
Takwimu hizi zimedhihirisha kuwepo kwa
ongezeko la mauaji hapa nchini. Nalazimika kuamini kuwa wapo wengine
walioua zaidi ya hawa waliotajwa
bungeni, kwa sababu kesi zao bado hazijaamuliwa na mahakama.
Katika miaka ya hivi karibuni, taifa
limeshuhudia taarifa nyingi za mauaji hasa ya ujambazi. Huko mkoani Mbeya,
matukio ya mauaji yanayoandamana na uchunaji ngozi za watu yalivuma sana ndani
ya miaka miwili iliyopita.
Sote tunatambua uchungu walionao na ambao
wataendelea kuwa nao, wale ambao ndugu zao waliuawa na mmoja wa watu hawa
wanaosubiri kuuawa pia.
Waliouawa katika matukio yanayopelekea
kunyongwa kwa wahusika hawa walikuwa baba zetu, kaka ama dada zetu ambao
walikuwa tegemeo kubwa katika familia zetu.
NIONAVYO MIMI, msingi wa kuwepo
kwa sheria hii ya kunyonga, ni kuhakikisha kuwa raia wanalindwa kikamilifu na hata kuzuia matukio ya mauaji hususani ya
kukusudia.
Hata hivyo, sidhani na sikubaliani kabisa
kuwa kuwanyonga wafungwa wa makosa ya mauaji ni njia sahihi na bora ya
kupunguza ama kukomesha kabisa, matukio ya mauaji nchini.
Ninazo sababu kubwa, na nyingi za msingi
kuthibitisha haya nisemayo; Mosi, itakumbukwa kwamba wakati fulani ujambazi
ulizuka kwa kiwango kikubwa sana katika Jiji la Dar es Salaam.
Wakazi wake wengi baada ya kuchoshwa na
vitendo hivyo na hasa pale ilipodhaniwa kwamba jeshi la polisi lilikuwa
limeshindwa kabisa kudhibiti vitendo hivyo, waliamua kuwachoma moto palepale
wale wote waliokamatwa wakifanya ujambazi.
Wakazi hawa walifanya hivyo wakitambua kuwa
kwa kuwauwa kwa njia hiyo, bila kujali kama jambazi alikuwa amesababisha kifo,
wangewatia woga na kuwakomesha kabisa majambazi hao.
Lakini hadi wakati huu unaposoma makala
hii, vitendo vya ujambazi havijaisha na ndio kwanza vinaongezeka kwa kasi.
Majambazi na hata vibaka wamekuwa hawasubiri
tena giza liingie, bali hufanya uharamia huo, mchana wa jua kali. Kibaya sana,
ujambazi sasa unafanyika hata katika nyumba za ibada. Sio tu kwamba sasa watu
hawaogopi macho ya watu, bali hata hawaheshimu nyumba za ibada.
Sababu ya pili inayonifanya niamini kuwa
adhabu hii haisaidii kukidhi haja yake, ni matukio ya ajali za barabarani. Kwa
watu wa vijijini, pengine sababu hii haitawaingia kikamilifu.
Lakini kwa wale tunaoishi mijini tunafahamu
na kutambua kikamilifu kwamba, dereva yeyote anayeendesha gari kwa uzembe na kumgonga mtu, dereva huyo hupigwa hadi
kufa na gari lake kuharibiwa vibaya hata kama aliyegongwa atakuwa hajafa.
Kama vile ilivyokuwa katika suala la
kuwachoma vibaka, ilitegemewa kuwa ajali za kugonga watu, hasa wale waendao kwa
miguu, zingepungua sana. Kinyume chake sasa, ajali zimeongezeka mno tena hata
katika sehemu ambazo usingetegemea zitokee.
Wakazi wengi wa mijini, watakubaliana nami
jinsi ambavyo watembea kwa miguu wanavyogongwa kila siku wanapovuka barabara
kwenye eneo la zebra (alama za pundamilia) ambako ni haki yao.
Je
ile adhabu ya kuwapiga na kuwaua iliyokuwa ikitolewa kwa madereva wa aina hii
imesaidia kukomesha vitendo hivyo?
NIONAVYO MIMI, jibu
litakalopatikana katika swali hili, ni wazi kuwa litakuwa likisema kuwa bado
vitendo hivyo havijasaidia kitu, isipokuwa kasi ya ajali inaongezeka kila
kukicha.
NIONAVYO MIMI, mbali na
kutosaidia lolote, adhabu ya kuwanyonga wahalifu, haina manufaa kwa waathirika
wa ndugu wa kwanza aliyeuawa. Mtu aliyeuawa na jambazi ama yeyote iwe kwa
makusudi ama kwa bahati mbaya, huacha nyuma yake familia yenye simanzi na
mateso.
Anaacha familia yenye chuki, visasi na
uhasama mkubwa baina yake na familia ya aliyeuwa.
Kwa kumnyonga muuaji, familia ya awali
haitakuwa imeepuka msiba mzima wa kuondokewa na mzazi ama ndugu yao. Familia
haitakuwa imenufaika kifedha ama kwa mali, na wala haitakuwa imesaidia kuondoa
chuki baina ya familia hizo mbili, eti tu kwa kuwa adui yao nae kauawa.
NIONAVYO MIMI, kwa kumnyonga
mhalifu wa mauaji, serikali na jamii kwa jumla itakuwa imewaadhibu watu wengine
zaidi ya yule mhalifu wa mauaji.
Kama familia 350 za wahalifu wa mauaji
zimebaki yatima, kwa kuwanyonga wahalifu hao, serikali na jamii itazalisha
kiasi kama hicho cha yatima na kufanya jumla kuwa 700!
Je serikali inaweka mpango gani basi,
kuhakikisha kwamba adhabu wampayo mtu huyu haitawaathiri kwa kiwango cha
kuwaingiza katika matendo mabaya watoto wa mzazi aliyehukumiwa kunyongwa?
Inawasaidia kwa jambo gani kuboresha iwe ni maisha ya watoto wa marehemu wa kwanza,
achilia mbali yule wa pili?
NIONAVYO MIMI, badala ya
kuwanyoga, serikali ingeliwahukumu wafungwa hawa kifungo cha maisha. Huko basi,
wangetumika kufanya kazi za uzalishaji mali kama vile uchimbaji wa migodi ya
dhahabu, ujenzi na kazi nyingine za uzalishaji mali.
Kwa kufanya hivyo, taifa lingepata faida
nyingi kwa sababu gharama za uzalishaji kwa kuwatumia watu wasiostahili
mshahara na marupurupu makubwa, zingekuwa ndogo sana.
Aidha, serikali ingeliweza kuweka utaratibu wa kutoa sehemu kidogo ya
faida ipatikanayo kutokana na kazi za uzalishaji mali wa mfungwa huyo,
kuisaidia ile familia ya mtu aliyeuawa na mfungwa.
Natambua kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, ndiye pekee mwenye uwezo wa kuamua juu ya hatima ya mfungwa mwenye hukumu ya kifo, akishauriwa na kamati
maalum ijulikanayo kama “Kamati ya Huruma.”
NIONAVYO
MIMI, kwa msingi
huo, ningeshauri wana kamati, taasisi mbalimbali na vyama vya kutetea uhai wa
binadamu, kushauri kwa umakini njia mbadala ya adhabu ya kifo. Kwa kweli
haisaidii, sio kwa serikali tu, bali hata kwa jamii nzima.