Madhehebu kuwakutanisha wanasiasa
Na Charles Misango
VIONGOZI wakuu wa dini
kutoka BAKWATA, CCT, TEC na Ofisi ya
Mufti Zanzibar, wanatarajia kuwakutanisha wanasiasa nchini wakiwamo wenyeviti
na makatibu wakuu wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu ili kujadili
amani na Uchaguzi Mkuu ujao.
Habari za kuaminika zilizolifikia
KIONGOZI, zimebainisha kuwa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Baraza
Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) na Ofisi
ya Mufti wa Zanzibar,
katika mkutano wao
uliofanyika Jumatano iliyopita kwenye Ukumbi wa Karimjee
Habari hizo za kuaminika
zilizothibitishwa na mmoja wa viongozi hao
waliohudhuria mkutano, zimesema taasisi hizo zinafanya maandalizi maalumu ya
mkutano huo ikiwa ni pamoja na kuwapa taarifa viongozi wa wa kisiasa ngazi ya
kitaifa, wanaotarajiwa kushiriki mkutano huo.
Kwa mujibu wa habari hizo, Mkutano
huo pia utawahusisha
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muuungano wa
Wengine ni
Wenyeviti wa Tume za Uchaguzi za Zanzibar (ZEC) na ile ya Tanzania Bara (NEC)
na wawakilishi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Waziri Kiongozi
Zanzibar.
Habari zimedai kuwa, mkutano wa
viongozi hao waandamizi wa siasa na dini, una lengo la kuangalia mambo muhimu
yanayopaswa kuzingatiwa na taifa ili kuhakikisha kuwa Uchaguzi Mkuu ujao wa
Rais na Wabunge pamoja na ule wa Rais wa Zanzibar na Wawakilishi, unaendeshwa
katika misingi ya haki, uhuru na amani.
Aidha, mkutano huo unatarajiwa
kuzungumzia namna viongozi wote wa dini watakavyoweza
kutumia nafasi zao kuchangia katika kufanikisha zoezi zima la uchaguzi.
Habari zimesema, uamuzi huo wa
viongozi wa dini, umetokana na utaratibu wao wa kukutana na viongozi wa siasa
kila mwaka na kwa namna ya pekee, mkutano huo wa mwaka huu utajadili mbinu bora
za kuendesha na kufanikisha Uchaguzi Mkuu ujao wa Rais na Wabunge wa mwaka
2005.
Historia inaonesha kuwa, kila baada
ya chaguzi kunakuwa na manung'uniko na migogoro ndani
ya vyama hali iliyofikia baadhi kufukuzana uanachanma na hata wakati mwingine,
kufikishana mahakamani.
Imekuwa ikidaiwa pia kuwa, katika
baadhi ya vyama vya siasa rushwa imekuwa ikitumika katika baadhi ya chaguzi ili kushinda.
Dosari nyingine ambayo imebainishwa
wazi na wananchi wengi katika chaguzi zilizopita, ni
baadhi ya wagombea kutumia ukabila, udini na hata ukanda
Uchunguzi zaidi wa Gazeti hili
umebaini kuwa, hadi sasa baadhi ya vyama vya siasa havina uhusiano mzuri baina
Wakati taifa likielekea
katika Uchaguzi Mkuu huu wa Tatu katika mfumo wa Siasa
wa Vyama vingi nchini, vyama vingine vya siasa vimekuwa vikitumia lugha za
vitisho na zinazohatarisha amani na usalama katika jamii.
‘Sheria ya Ugaidi ‘inasaliti’ Katiba’
Na Joseph Sabinus
Akitoa mada katika
semina hiyo, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Kitivo cha Sheria,
Dk. Sengodo Mvungi, alisema sheria hiyo
ambayo ni dhahiri imeundwa kwa shinikizo la Taifa la Marekani, ni hatari kwa
jamii kwa kuwa inawapa mamlaka watawala na vyombo vya dola kukiuka haki za
binadamu kama zinavyoelezwa katika Katiba.
Alisema miongoni mwa haki hizo, ni pamoja na uhuru wa kupokea na kutoa habari, haki ya
kuheshimika na kuchukuliwa kutokuwa na hatia hadi sheria itakapomthibitisha mtu
kuwa na hatia.
“Nyingine ni
haki ya kutembea, kuandamana, kukusanyika, kumiliki na hata haki ya mtu
kutoingiliwa faragha,” alisema.
Alisema kwa
mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Dk. Mvungi alisema kuwa, kwa kurithi mfumo wa Utawala wa Uingereza, hivi sasa Dola
inaichukulia Katiba ya nchi
Katika mfano wake, Dk. Mvungi
alisema Sheria hiyo ya Ugaidi katika Kifungu cha 9(1), inamzuia mwandishi wa habari kupokea wala kusambaza habari zozote za kigaidi.
Katika mada aliyoitoa kwenye semina
hiyo, Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na
Utawala Bora, Balozi Mohamed Ramia Abdiwawa, alisema Sheria ya Kuzuia Ugaidi
ilipaswa kulinda haki za binadamu na utawala bora na kwamba, ina mapungufu
makubwa kwa kuwa haielezi tafsiri ya ugaidi.
Balozi Ramia alisema badala yake,
sheria inazungumzia vitendo vya kigaidi na kwamba,
bila kuwapo kwa muafaka na tafsiri ya wazi, itakuwa vigumu kwa dunia kupambana
na ugaidi.
Katika kuchangia, wajumbe walisema
ukosefu wa tafsiri halisi ya ugaidi unasababishwa na
ukweli kuwa, baadhi ya mataifa yanayoshinikiza vita na sheria dhidi ya ugaidi
yakiongozwa na Marekani, yanashiriki kwa namna nyingi katika kufanikisha na
kuendeleza ugaidi.
“Mara nyingine
utata huo umesababisha ugaidi kufananishwa na upiganiaji wa uhuru,” alisema.
Katika semina hiyo, Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Helen Kijo-Bisimba,
alisema miongoni mwa mapungufu na ukiukwaji wa haki za binadamu uliopo katika
sheria hiyo, ni kutotajwa kwa muda wa kumalizika kesi huku mtuhumiwa akiwa
mikononi mwa dola.
“Sheria hii pia, haitaji
Naye Mwenyekiti wa Muungano wa Asasi
zisizo za Kiserikali nchini Tanzania (TANGO), Marie Shaba, alisema wakati
akifunga semina hiyo kuwa, jamii haina budi kuungana ili kupinga mambo
yote yanayokwenda kinyume na haki za binadamu.
“Bila watu wote kuungana tangu
makanisa, misikiti, wanaharakati na NGOs, tutafika
mahali pabaya ambapo sasa sheria mbaya
Semina hiyo
iliazimia kuendesha kampeni maalumu kuhakikisha kuwa, sheria hiyo inabadilika.
Maazimio
mengine yaliyofikiwa ni juhudi za makusudi za
kuwaelimisha Watanzania kuhusu sheria hiyo kwani watu wengi wakiwamo baadhi ya
viongozi Serikali, vyama na dini hawaijui kwa kuwa hawakushirikishwa katika
kuandaa muswada.
Chini ya Sheria ya Ugaidi, ni marufuku kusoma au kusambaza habari za kigaidi.
Sheria hii inazuia
mtu anayedhaniwa kuwa gaidi, kuhutubia wala kusikilizwa akihutubia mkutano.
Katika Kifungu cha
29, Sheria inatoa nguvu zaidi za upekuzi kwa polisi.
Chini ya Sheria hii, bila kulazimika kupata waranti, afisa wa
polisi chini ya cheo cha Assistant Superintendent of Police, anaweza
kuingia na kufanya upekuzi mahali popote.
…Wanaochanganya dini, siasa wavurugaji Zanzibar- Sheikh
Na Joachim Mushi
HALI ya machafuko ya amani yanayotokea
Visiwani Zanzibar kila mara, inachangiwa kwa kiwango
kikubwa na baadhi ya watu wanaochanganya dini na mambo ya siasa; Imesema
Ofisi ya Mufti wa
Mwakilishi
kutoka Idara ya Mufti Zanzibar, Sheikh Said Nassoro Seif alisema hayo katika
mahojiano na waandishi wa habari, nje ya ukumbi wa
Karimjee
Alisema mambo mengi
yanayolalamikiwa na baadhi ya Waislamu Visiwani humo,
yana mtazamo wa kisiasa zaidi kuliko wa kidini.
“Hali hiyo imeharibu sifa na heshima ya Uislamu katika macho ya watu wengine duniani,”
alisema.
Sheikh Said alisema malalamiko juu
ya Serikali kuingilia masuala yanayowagusa Waislamu moja kwa
moja
Alisema awali, kulikuwa na vyombo kadhaa vilivyokuwa vinamilikiwa na Waislamu, huku
vikisimamiwa na serikali, na hakukuwa na malalamiko yoyote kwa muda wote.
“Sasa iweje leo
hii kuwepo na shutuma kali dhidi ya Serikali, wakati sio jambo geni?” alisema.
Akifafanua zaidi, Sheikh Said
alisema, Chuo Kikuu cha Kiislamu Zanzibar na Mahakama
Kuu ya Kiislamu ni baadhi ya taasisi nyeti zinazomilikiwa moja kwa moja na
Waislamu, huku zikiongozwa kwa muda mrefu na Serikali bila matatizo.
“Hata mapendekezo ya majina ya watu
wanaofaa kuwa Mufti wa
Alisema ingekuwa vyema kwa Waislamu wenye mapenzi ya siasa kuendesha shughuli hiyo
bila kuhusisha upande wa pili wa dini. “Huwezi kutumikia watu
wawili kwa wakati mmoja hata siku moja.
Kauli ya Mwakilishi huyo wa Mufti inatokana na malalamiko ya siku nyingi, yanayotolewa
na baadhi ya Waislamu Visiwani humo, wakidai kuingiliwa na vyombo vya Serikali
katika masuala yanayaohusiana na Dini ya Kiislamu.
Katika
Mkutano huo, Askofu Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT),
Elinaza Sendero, alisema jamii haina budi kuunganisha nguvu zake pamoja ili
kuwadhibiti watu wanaofanya majaribio ya kuvuruga amani nchini.
‘Tusikubali kuwa watumwa wa wafadhili’
Na Lilian Timbuka
Askofu wa
Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Dar es Salaam, Valentino Mokiwa, amesema Umasikini
ni mchezo wa utandawazi unaompumbaza mwananchi ajione mnyonge na
asiyejiweza, ingawa baadhi ya viongozi wanaushabikia utandawazi huo.
Aliyasema hayo juma lililopita wakati akifungua warsha ya
siku mbili iliyoandaliwa kwa pamoja na Jumuiya za Kikristo
Warsha hiyo ililenga kujadili Mkakati wa
Pili wa Kuondoa Umasikini uliofanyika katika ukumbi wa mkutano TEC, jijini
Alisema ingawa jamii inaendesha mijadala mingi juu ya suala
la kuondoa umaskini, lakini haina matunda kwa kuwa
wafadhili wa semina na warsha juu ya umaskini, hushinikiza wapate maazimio
ambayo mataifa wahisani huyatumia kubuni mbinu nyingine za ukandamizaji wa
wanyonge.
Askofu Mokiwa alisema vita dhidi ya umaskini haina budi kutoa
kipaumbele pia katika kupambana na ujinga kwa kuwa
matatizo haya, huambatana.
“Wakati mwingine utaona kuwa hizi semina zinazofadhiliwa na mataifa ni mbinu za
matajiri kuwatuma masikini wajadili hali zao, na kisha wawaambie wafikiri nini
ili wajiondoe kwenye umasikini.”
Akaongeza kuwa,“Kwa kuwarudisha
kule, basi hukaa na kusema, hivi ndivyo masikini wanavyozungumza; wamesema
wanataka kufanya hivi, sasa sisi tunafanya hivi kuwadhibiti.”
Alidokeza kuwa ndio maana mara nyingi
wafadhili hutaka ripoti za semina hizo, kabla nchi husika haijatoa maamuzi.
Askofu Mokiwa aliyalaumu mashirika ya fedha ya kimataifa, IMF
na Benki ya Dunia akisema kuwa, yamekuwa yakitoa fedha
kwa ajili ya kupanga mikakati ya kupambana na umasikini wakati huo huo
yanazibana nchi masikini katika kuondokana na umasikini.
Alisema iwapo Mashirika hayo yana
nia ya kuinua uchumi na utajiri kwa nchi masikini, basi yafute madeni
“Ninyi mjijue wazi
kuwa ni sauti ya watu wasio na sauti, fanyeni juhudi
mumkomboe mwananchi aliye kwenye mahangaiko,” alisisitiza.
Alisema Watanzania si masikini kwa
kiasi kikubwa
Alibainisha kuwa, maono hafifu, sera za ubabaishaji za
mdomoni na zisizotekeleza, zinachangia kwa kiasi
kikubwa Mtanzania kujiona masikini.
Akitolea mfano wa mto Rufiji, Askofu Mokiwa alisema kuwa, mto
huo umekuwa ukitiririsha maji mabilioni ya lita kwenda baharini kwa siku, hali watu hawana
maji ya kutumia.
“Tunasubiri Wahisani waje watujengee
malambo ya kuhifadhi maji ya mto ule.”
Alisema katika nchi ya
Alisema hivi sasa utajiri wa nchi
umekabidhiwa kwa wageni wenye mitaji mikubwa, huku Mtanzania akikejeliwa kuwa
ni masikini na mtaji wake ni mdogo.
“Utajiri tumewakabidhi wageni ambao hivi sasa wanaondoka nao
mpaka makontena ya mchanga, lakini hatuulizi wanapeleka wapi huo mchanga na una nini ndani yake,” alisema.
Akaongeza, “Iko haja hivi sasa, wakati mkakati wa kujadili mchakato wa kuondoa umasikini unavyoendelea,
kutafuta na kuzibaini hali za umasikini tulizo nazo na kuzifanyia kazi kabla ya
kuwapelekea hao wanaojiita wafadhili wa kuondoa umasikini.”
Akitoa mada juu ya Uhusiano wa
Jinsia, Rasilimali na Ushiriki wa Wananchi katika PRSP, Bibi Mary Mwingira
alisema kuwa, muktadha wa uchambuzi wa sera za umasikini wa
Alisema kuwa hivi sasa
imeonesha kuwa, Watanzania walio wengi wana umasikini wa
akili na kufikiri na si rasilimali
Bibi Mwingira alisema
kuwa Mkakati wa kwanza wa uchambuzi wa umasikini
unaonesha kuwa, upande wa uwekezaji umepiga hatua japo serikali na bunge
wamekuwa wakitoa muongozo wa uwekezaji katika njia zisizo sahihi.
Hata hivyo Bibi Mwingira
alibainisha kuwa, umasikini wa Mtanzania unalemazwa na
utegemezi uliojengeka akili mwao, kwa kufikiri kila jambo watafanyiwa na
wafadhili.
“Hebu
tujiulize kwanza,
Wakichangia mada
washiriki wa warsha hiyo, waliwalaumu wafadhiri kwa
njia zao wanazotumia kusamehe madeni ya nchi masikini,
Warsha hiyo ya siku mbili, iliwashirikisha washiriki kutoka Jumuiya
za Kikristo Tanzania (CCT), Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na BAKWATA.
Milioni 200/= zahitajika kujenga Kanisa Kimara
Na Joseph Chewale
JUMLA ya shilingi milioni 200
zinahitajika kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa kubwa na la
kisasa la Parokia mpya ya Kimara, Jimbo Kuu Katoliki la
Paroko wa Parokia hiyo, Padre John
Frances ameliambia KIONGOZI kwamba, fedha hizo zinategemewa kupatikana kutoka
kwa waamini wa parokia hiyo ambao wamejizatiti kuhakikisha kuwa, wanafanikisha
upatikanaji wa fedha hizo mapema iwezekanavyo.
Padre
Alisema Kamati ya Ujenzi na Ardhi
imeundwa kusimamia ujenzi wa Kanisahilo linalotazamiwa kuchukua waaini 1,500
kwa wakati mmoja.
Alisema kuwa, mbali na michango ya
waamini parokiani hapo, waamini wengine na Watanzania wote wenye mapenzi mema,
wanakaribishwa kutoa chochote kitakachosaidia katika ujenzi huo.
“Tunategemea kufanya michango na mbinu
nyingine zitakazotusaidia kupata pesa. Lakini vilevile,
tunawaomba waamini wengine na Watanzania wenzetu wenye
mapenzi mema watusaidie,” alisema.
Waamini wa parokia hiyo
wanaokadiriwa kufikia 5140 kwa sasa, wanatumia banda la miti wakati wa ibada kwa
vile Kanisa lililojengwa likiwa kigango, ni dogo na linaloweza kuchukua waamini
200 tu.
Parokia hiyo iliyomegwa kutoka Parokia ya Ubungo Msewe, hadi
sasa ina vigango viwili vya King’ong’o na Korogwe. Ni
parokia inayokua kwa kasi kwa kuwa na ongezeko kubwa
la waamini. Ikiwa na vyama tisa vya kitume, Parokia ya
Kimara inazo Jumuiya Ndogondogo 49 zilizogawanywa katika kanda nane.
Wakati huo huo: Padre
Amesema, shule za Mavurunza na
Korongwe ndizo tu zilizopo katika parokia yake na kwamba hali hiyo, inawafanya
watoto wengi kusoma shule za mbali. Amedai kuwa, watoto wengi wanapata taabu ya
kusafiri umbali mrefu na kukabiliana na kero za
daladala ambazo zingelikwisha tu, iwapo kungekuwa na shule nyingi zaidi katika
eneo
Hata hivyo, Padre huyo amesema wananchi pia wanaowajibu
kutumia nguvu zao ili kuionesha Serikali kuwa, na nia
ya maendeleo isipokuwa, wamekwama sehemu fulani.
Alisema huu ni wakati muafaka
kutambua kuwa, ili kupata maendeleo ya kweli na ya haraka, kila mwanajamii hana
budi kutambua kuwa anawajibika kuchangia upatikanaji wa maendeleo hayo na
kuondoa kero mbalimbali.
Mabaharia wabadili jina kuondoa mfumo dume
Lilian
Nyenza na Wema Figao
CHAMA Cha Mabaharia
Nchini (TASU), kina mpango wa
kubadili jina la chama hicho ili kuondokana na lile la sasa
linaloashiria mfumo dume.
Katibu Mkuu wa
TASU Taifa, Bw. Nicholas Mgaya,
amesema wanachama wengi wanalalamikia jina la sasa la Tanzania Seamen
Union (TASU), kuwa linaelekeza watu kuamini kuwa chama hicho ni cha
mabaharia wanaume tu, wakati wapo wanawake wanaofanya kazi hiyo.
Amesema ili kuondoa dhana hiyo, chama hicho kitaitwa Tanzania Seafarers
Union, jina ambalo wanaamini litakuwa limekidhi na kubeba jinsia zote
za wanachama wa chama chake.
Katibu Mkuu huyo amesema hadi sasa, chama
chake kina mabaharia wanawake 40, kati ya 900 waliopo.
Kuhusu mikakati ya
chama chao, Bw. Mgaya amesema
wanatarajia kufungua tawi
Hivi karibuni, chama hicho kilifanya uchaguzi wake kitaifa
ambapo Bw. Abeid Sheremu alichaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya kwa kupata kura
21. Bw. Nicholas Mgaya
aliibuka kuwa Katibu Mkuu Taifa kwa kupata
kura 23 na kumbwaga mpinzani wake Ahmedi Chakoma aliyeambulia kura tisa.
Viongozi
pambaneni kuiokoa jamii - Askofu
Charles
Hililla, Kahama
VIONGOZI wa Kanisa nchini, wametakiwa kuwa makini, wavumilivu na
shupavu katika kupambana na kasoro mbalimbali zinazovuruga mwenendo na mfumo
bora wa maisha katika jamii.
Rai hiyo ilitolewa hivi karibuni na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki
Mhashamu Niwemugizi ambaye ni Askofu wa Jimbo la Rulenge, alisema
kumekuwapo na kasoro mbalimbali katika mfumo mzima wa maisha ya Watanzania
ikiwa ni pamoja na rushwa, ambayo imekithiri kwa wakubwa wengi hapa nchini na
vita dhidi ya tatizo hilo, imekuwa ikipigwa kwa wadogo.
Aliongeza kuwa, Serikali haina budi
kuweka mkakati wa makusudi kupambana na rushwa
Aidha, Mhashamu NiweMugizi alisema
kuwa, kukithiri kwa vitendo hivyo vya rushwa hapa
nchini, ambavyo vinachangia kwa kiasi kikubwa taifa na jamii kuonekana
masikini, kwa kukosa maendeleo.
Alisema vitendo hivyo kwa sasa vinajificha ndani ya kivuli cha uwekezaji, ambao
unatafsiriwa na jamii kuwa ni unyang’anyi na wizi wa mchana unaofanywa na
wakubwa, huku jamii ikikosa huduma muhimu.
Alifafanua kuwa, hali hiyo kwa kiasi kikubwa inachangia kuwapo kwa tishio la kuvurugika
kwa amani nchini.
“Ni aibu kwa wananchi wa
wilaya ya Kahama kukabiliwa na umaskini kwa kukosa huduma, wakati wilaya yao
ina mgodi mkubwa wa dhahabu uliopo Bulyanhulu ambao hutoa madini, “
alisema na kuongeza “… halafu madini
hayo yanapitishwa mbele ya macho yao na kupelekwa kwa wakubwa ambao ndio wanaofaidi
matunda yanayotokana na utajiri wao huku wao wanabakia masikini ndani ya ardhi
iliyojaliwa utajiri.”
Alisema kuwa, viongozi wa Kanisa wanao wajibu mkubwa kushirikiana na viongozi
wengine serikalini katika kupambana na changamoto za utandawazi wa kimaendeleo,
ili kuondoa kasoro zinazojitokeza na watu wamtumikie Bwana kwa moyo
Mhashamu NiweMugizi aliongeza kuwa,
kinyume na hali ilivyo sasa, watu wengi wamekuwa
wakitenda maovu kwa kisingizio cha hali mbaya ya maisha, huku UKIMWI nao
ukichukua nafasi inayowaacha vijana wakikosa mwenendo mzuri wa kimaadili kwa
kufundishwa masomo ya UKIMWI shuleni.
Alisema masomo hayo yanayofundishwa kwa kivuli cha stadi za maisha, yamekuwa yakiendeleza
mmomonyoko wa maadili kwa jamii.
Kanisa Shinyanga kutafutia wakulima soko Ulaya, Asia
Na Peter Dominic
JIMBO
Katoliki la Shinyanga lipo hatua za mwisho katika kukamilisha mpango wa kuwawezesha wakulima kuuza mazao
Mkurugenzi wa Mpango wa
Mradi wa Kilimo na Mifugo jimboni humo, Padre Zengo Mikomangwa, ameliambia KIONGOZI
mwanzoni mwa juma lililopita kuwa, Jimbo hilo limefikia uamuzi huo ili
kuwasaidia wakulima ambao wamekuwa na tatizo la ukosefu wa soko la mazao yao
licha ya uzalishaji kuwa mzuri.
Alisema, tatizo la
ukosefu wa soko la uhakika, limesababisha wakulima wa
mazao mbalimbali walazimike kuuza, mazao
Alisema katika kutafuta
njia sahihi ya kumsaidia mkulima ili auze mazao yake
kwa faida, waliamua kufanya utafiti wa mazao yanayohimili ukame ambayo pia soko
Padre Mikomangwa alisema
katika utafiti huo, wameshirikiana na Kituo cha
Utafiti cha Ukiligulu na Shirika la Wakatoliki la Marekani na Shirika la
Utafiti wa mazao ya mikunde na mazao yanayohimili ukame la International
ICRISAT ambalo makao makuu yake yapo
Wengine kwa mujibu wa Padre Mikomangwa, ni shirika moja
linalojihusisha na utoaji wa huduma za kijamii (C.R.S).
Alisema utafiti huo
uliochukua miaka mitatu, pia umehusisha wakulima wenyewe pamoja na halmashauri za wilaya ambapo mazao yaliyopewa kipaombele
ni dengu, karanga, mbaazi na mazao mengine
“Kilimo hiki kilikuwepo
muda mrefu, sisi tunatafiti na kutafuta soko linahitaji mazao gani, Baada ya
utafiti, tuliwapelekea wakulima mbegu tisa wakachagua nne, tuliamua
kushirikiana na Shirika la
(Techno Serve). Hawa ni wataalamu wa
masoko. Tumefanikiwa kupata soko katika nchi za
Hata hivyo alisema,
kabla ya kufikia uamuzi ya kutafuta masoko, Jimbo
“Mpango huu umewezesha
kuundwa kwa vikundi vinane na vinne kati
Padre Mikomangwa
alisema, vikundi hivyo vilivyopo katika Wilaya za Shinyanga na
Maswa vimeanza uzalishaji na huenda vikaanza kuuza mazao yake katika soko la
nje mwaka huu.
Mradi hiyo inafadhiriwa na Catholic
Relies Services (CRS) “Lengo la Jimbo ni kuwasaidia wakulima kuuza mazao
Hospitali binafsi zabeza gharama za Muhimbili
Na Kizitto
Joseph
BAADHI ya wagonjwa
waliokuwa wakipata matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,
wamekimbilia katika hospitali binafsi za jijini
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na
KIONGOZI, madaktari wa hospitali za Hindu Mandal, Regent na Aga
Khan zote za jijini, walisema kuwa hospitali zao zimeanza kupokea wagonjwa
wengi waliokuwa wakipata matibabu kutoka Hospitali ya Muhimbili tangu
ilipoongeza gharama za matibabu.
“Watu wameanza
kufurika katika hospitali za watu binafsi. Mtanzania gani ataweza kumudu
gharama za Muhimbili,” alihoji Dk. Sharrif Patel wa
Hospitali ya Hindu Mandal.
Alisema wengi wa
wagonjwa waliokuwa wanaitumia Hospitali ya Muhimbili, wameanza kubadili
mwelekeo kutokana na kushindwa kumudu gharama hiyo mpya kwa sababu za kiuchumi.
Pamoja na
kufurahia kuongezeka kwa wagonjwa katika hospitali yake, Dk. Patel alisema
uamuzi wa kuongeza gharama za matibabu katika hospitali hiyo ya serikali,
haukuwa wa busara kwa kuwa hakujali kipato cha mtu wa kawaida.
“Yeyote aliyeshinikiza uamuzi huo (mabadiliko
hayo) hakuwa na takwimu ya umaskini wa wananchi.
Hakuna Mtanzania mwenye kipato cha kawaida anayeweza kutumia shilingi 10,000 kwa matibabu ya siku moja,” alisema.
Mmoja wa
maafisa wa Utawala wa Hospitali ya Regent ambaye hakutaka kutajwa jina
Aliishauri serikali kutumia kodi
inayokusanywa toka vyanzo mbalimbali vya mapato, kugharamia matibabu ya
wananchi wake badala ya kuwaachia gharama hiyo ambayo kwa
hali yoyote ile hawawezi kuimudu.
“Huwezi kuongeza
gharama za matibabu kabla ya kuongeza kipato cha mtu. Wagonjwa wengi
wameanza kukimbilia hospitali za watu binafsi kuogopa gharama za Muhimbili,”
alisema,
Akaongeza kuwa, katika hospitali
yake na zile anazozifahamu, kumekuwa na wagonjwa wengi
zaidi ikilinganishwa na siku za nyuma na utafiti walioufanya, umeonesha kuwa ni
kutokana na ongezeko la gharama za matibabu katika Hospitali ya Muhimbili.
Hivi karibuni katika uamuzi
uliolalamikiwa mno na Watanzania, Uongozi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili,
uliongeza gharama za matibabu kutoka shilingi 500/= hadi 10,000/= kwa ugonjwa
wa kawaida na shilingi 50,000/= kwa upasuaji mdogo.