Ushauri huo
ulitolewa na mwakilishi wa
“Hali ya
kutovumiliana kidini inayoibuka kichinichini inapinga haki ya dini kueleza
mambo yake waziwazi juu ya masuala ya aina za tabia ambazo zinapimwa kwa kufuata kanuni za maadili na misingi ya dini,” alisema.
“Wakati hali
nzuri ya dola kutokuwa na dini rasmi inabidi
iheshimiwe, wajibu wa waamini katika maisha ya umma unapaswa kutambuliwa,”
alisema Tomasi.
“Hili
linahusiana na haja ya kuwepo vyama vingi vya siasa na
kuchangia kujenga demokrasi halisi, miongoni mwa mambo mengine. Dini haiwezi
kusukumizwa katika pembe ya maisha binafsi na kwa njia
hii kuhatarisha hali yake kijamii na huduma yake ya wahitaji bila ubaguzi,” alisema mwakilishi
huyo wa
Askofu Mkuu
Tomasi alirejea Tangazo la Haki za Binadamu namna linavyoeleza na kukuza uhuru
wa dini, ambapo alinukuu ibara ya 18 ambayo inasema: “Kila mtu anayo haki ya
kuwa na uhuru wa mawazo, dhamiri na dini; haki hii inahusisha uhuru wa kubadili
dini au imani, na uhuru aidha wa mtu akiwa peke yake au katika jamii pamoja na
watu wengine na katika maisha ya umma au ya binafsi, kuonesha dini au imani
yake kwa kufundisha, kuishi, kuabudu na kuikiri.”
Aliongeza kusema kuwa “kwa bahati mbaya uhuru wa dini
unaendelea kukiukwa katika sehemu mbalimbali. Siku hizi kuna hali nyingine ya makundi yasiyo ya dola
ambayo hujichukulia hatua za kudhalilisha waamini wa
dini za wachache, ambayo mara nyingi huwa hayachukuliwi hatua.”
“Sehemu za ibada pamoja na makaburi yanachomwa au kuharibiwa na kubomolewa; waamini wanatishiwa, kushambuliwa na hata kuuawa, na viongozi wao wanafanywa kuwa malengo maalumu ya vitendo vyao,” alisema na kuongeza “Uwezo wa mtu kuchagua dini yake, ikiwemo haki ya kuibadili unakumbana na vikwazo vikubwa katika baadhi ya mazingira ya kijamii, ukikaji wa moja kwa moja wa uhuru wa dhamiri.” Alisema
Papa
apendekeza Pasaka ya pamoja kwa Wakristo wote
BABA Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili kwa mara nyingine
amependekeza Wakristo wa Magharibi na Mashariki kuadhimisha Pasaka kwa siku moja kila mwaka.
Papa
alichukua fursa hiyo kutokana na “kugongana kwa
bahati” mwaka huu kwamba, Pasaka iliadhimishwa siku moja kufuatana na kalenda
za Ki-Gregorian (Magharibi) na Ki-Julian (Mashariki). Kiongozi huyo alirudia
tena pendekezo
Baada
ya kutoa baraka zake
“Ninaomba
kwa Bwana Mfufuka kwamba, sisi sote tuliobatizwa muda
mfupi ujao tutaweza kuadhimisha sikukuu hii ya msingi katika imani yetu siku
moja kila mwaka,” alisema.
Pasaka ambayo ni
sikukuu muhimu
Kwa
sababu ya makosa yaliyokuwa katika kalenda ya Julian (iliyoanzishwa na Julius Caesar katika mwaka 46 KK), Baba Mtakatifu Gregori
wa 13 (1582 BK) aliifanyia marekebisho kwa kuzingatia vigezo vipya vya kuhesabu
siku ya Pasaka. Hata hivyo, Makanisa ya Mashariki hayakuafiki
kufuata mabadiliko haya.
Faharasa
(appendix) ya “Sacrosanctum Concilium,” katika katiba ya dogma juu ya liturujia
takatifu, Kanisa Katoliki lilieleza nia yake ya kufikia makubaliano na makanisa ambayo yalijitenga na Roma kuhusiana na tarehe
ya Pasaka.
Wakati
huohuo, Katika Misa ya Mkesha, Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa
Pili alitoa Sakramenti ya Ubatizo kwa wakatekumeni saba (7) katika Kanisa Kuu
la Mt. Petro
Wakatekumeni waliobatizwa walitoka nchi za
Wairaq
Watakiwa Kuishi kwa Amani
ASKOFU Mkuu wa
Kanisa Katoliki madhebebu ya Syrian amesema kwamba Wairaq wa dini zote wanaweza
kuishi pamoja kwa amani licha ya nchi
Askofu mkuu huyo wa
“Tunawaomba Wakristo wote kuwaombea watu wa
“Wakati wote Wakristo wa
Wakati wa Pasaka Askofu Mkuu Mattoka
yeye binafsi alijihusisha katika kukusanya misaada ya kutuma kwa watu wa
Falluja mahali ambapo kulikuwa na mapigano makali. Askofu huyo aliongea na Fides kabla ya kwenda kutembelea familia za watoto
waliokuwa wanajiandaa kupokea Komunyo Takatifu.
“Ninakaribia kwenda kwenye mkutano nje pamoja na watoto wa
“Leo (Aprili 16), watoto wa
madhehebu mbalimbali ya Kikatoliki
katika
Aliongeza kusema kuwa, katika wakati huu wa
muhimu katika sakramenti ya Ekaristi Bwana na Mkombozi wetu Yesu Kristo anakuja
kwa hawa watoto wadogo ambao ni matarajio ya hali ya baadae ya nchi ya
Ukweli kwamba kuishi pamoja kwa watu wa imani na dini mbalimbali kunawezekana nchini