UJUMBE WA BABA MTAKATIFU YOHANE PAULO II KWA AJILI YA KUADHIMISHA SIKU YA AMANI DUNIANI JANUARI 1, 2004

 

MSISHINDWE NA UOVU  BALI MUUSHINDE UOVU KWA WEMA

1.         MWANZONI mwa Mwaka Mpya, kwa mara nyingine tena nawahutubia viongozi wa mataifa na watu wote waume kwa wake wenye mapenzi mema, ambao wanatambua haja ya kujenga amani duniani. Kwa ajili ya Siku ya Amani Duniani ya mwaka huu 2005 nimechagua maneno ya Mtakatifu Paulo kwa Waroma: “Msishindwe na uovu, bali muushinde uovu kwa wema” (12:21). Kamwe uovu haushindwi kwa uovu; mara njia ya namna hiyo inapofuatwa, badala ya kuushinda uovu, mtu atajikuta badala yake anashindwa na uovu.

Mtume mkuu anafichua ukweli wa msingi: amani ni matokeo ya mapambano ya muda mrefu na magumu ambayo ushindi unapatikana tu pale uovu unaposhindwa kwa wema. Iwapo tutashangaa matukio ya vurugu na migogoro katika sehemu mbalimbali za ulimwengu, na matukio yasiyosemeka ya mateso na ukosefu wa haki ambayo yamesababishwa na migogoro hiyo, chaguo pekee la kweli na lenye kujenga ni, kama Mtakatifu Paulo anavyopendekeza, kukimbia kile kilicho kiovu na kushikilia kwa nguvu kile kilicho chema (rej. Rom 12:9).

Amani ni wema ambao unapaswa kukuzwa kwa wema: ni wema kwa watu binafsi, familia, kwa mataifa na kwa watu wote; hata hivyo ni ule unaohitaji kutunzwa na kuendelezwa kwa maamuzi na matendo yanayosukumwa na wema. Tunaweza kushukuru kwa ajili ya ukweli wa msemo mwingine wa Mtakatifu Paulo: “Msilipe uovu na uovu kwa mtu yeyote” (Rom 12:17). Njia moja ya kutoka kwenye mduara wa maovu wa kulipa uovu kwa uovu ni kukubali maneno ya Mtume: “Msishindwe na uovu, bali muushinde uovu kwa wema” (Rom 12:21).

 

Uovu, wema na upendo

 

2.     Kutoka mwanzoni, binadamu wamejua hatari za uovu na wamepambana kujua mizizi yake na kueleza sababu zake. Uovu sio baadhi ya nguvu zisizo za kirafiki na zilizopangiliwa zinazotenda kazi ulimwenguni. Ni matokeo ya uhuru wa binadamu. Uhuru, ambao unatofautisha wanadamu na kila kiumbe kingine duniani, uko daima katika moyo wa mchezo wa uovu. Uovu daima una jina na sura: jina na sura za wale wale wanaume na wanawake ambao kwa uhuru kabisa uuchagua. Maandiko Matakatifu yanafundisha kwamba katika mapambazuko ya historia Adamu na Eva waliasi dhidi ya Mungu, na Abeli aliauawa na Kaini, kaka yake (rejea Mwa 3-4). Haya yalikuwa machaguo mabaya mawili ya mwanzo, ambayo yalifuatiwa na mengine mengi katika karne zilizofuatia. Kila moja la haya machaguo yana kipimo cha ndani cha kimaadili, kikihusisha wajibu maalumu wa watu binafsi na uhusiano mhimu wa kila mtu na Mungu, na watu wengine na uumbaji wote.

Katika hatua ya kina kabisa, uovu ni kukataa matakwa ya upendo.1 Kwa upande mwingine, wema wa kimaadili, unazaliwa na upendo, hujionesha wenyewe kama upendo na unaelekezwa kwenye upendo. Haya yote hasa yako wazi kwa Wakristo, ambao wanajua kwamba uanachama wao katika Mwili-fumbo mmoja wa Kristo yanawaweka katika uhusiano maalumu sio tu na Bwana bali pia na kaka na dada zao. Mantiki ya ndani ya upendo wa Kikristo, ambayo katika Injili ni chanzo hai cha wema wa kimaadili, inaongoza hata kwa upendo wa maadui wa mtu: “Iwapo adui yako ana njaa, mlishe; iwapo ana njaa, mpe kitu cha kunywa” (Rom 12: 20).

 

“Muundo” wa sheria ya maadili ya mahali pote

 

 3. Tukiangalia hali ya sasa ya ulimwengu, hatuwezi kusaidia isipokuwa kugundua msambao mbaya wa mambo kadhaa ya kijamii na kisiasa yanayodhihirisha kuwepo kwa uovu: kuanzia ugomvi hadi vurugu za kijamii na vita, kutoka ukosefu wa haki hadi vitendo vya vurugu na mauaji. Kuongoza njia kati ya madai yanayokwaruzana ya wema na uovu, familia ya kibinadamu inahitaji utunzaji na heshima ambayo usimamizi wa pamoja wa tunu za maadili uliotolewa na Mungu mwenyewe. Kwa sababu hii, Mtakatifu Paulo anawahamasisha ambao wamedhamiria kuushinda uovu kwa wema kuwa watu wa haki na kujihusisha katika kukuza ukarimu na amani (rej. Rom 12:17-21).

Miaka kumi iliyopita, katika kuhutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa juu ya haja ya dhamira ya pamoja kwa ajili ya huduma ya amani, niligusia “muundo” wa sheria maadili ya kila mahali,2 ambao juu ya huo Kanisa hutoa mwito katika matangazo yake kadhaa kwenye eneo hili. Kwa kuvuvia tunu na kanuni za pamoja, sheria hii huunganisha watu, licha ya tamaduni zao tofauti, na yenyewe haibadiliki: “inahimili ndani ya mjongeo wa mawazo na mila na husaidia maendeleo yake … Hata wakati inapokataliwa katika kanuni zake hasa, haiwezi kuharibiwa au kuondolewa kutoka kwenye moyo wa mtu. Daima huibuka tena katika maisha ya watu binafsi na jamii”.3

 4.    Muundo huu wa pamoja wa sheria ya maadili daima huhitaji dhamira na wajibu mkubwa katika kuhakikisha kwamba uhai wa watu bifasi na ya mataifa unaheshimiwa na kuendelezwa. Katika mtazamo huu, maovu yenye asili ya kijamii na kisiasa ambayo huiathiri dunia, hasa wale watu wanaochokozwa na milipuko ya vurugu, inalaaniwa kwa nguvu. Mara moja ninalifikiria bara pendwa la Afrika, mahali ambapo migogoro ambayo tayari imegharimu mamilioni ya wahanga na bado inaendelea. Au hali ya hatari ya Palestina, Nchi ya Yesu, mahali ambapo msingi wa maelewano ya pamoja, yaliyoraruliwa na mgogoro ambao kila siku unalishwa na vitendo vya vurugu na kisasi, haiwezi tena kurekebishwa katika haki na ukweli. Na vipi kuhusiana na matukio ya kutisha ya vurugu za kigaidi, ambazo zinaonekana kuwa nguvu inayousukuma ulimwengu wote kuelekea hali ya baadae ya hofu na mateso? Mwisho ni kwa vipi hatuwezi kufikiria kwa masikitiko makubwa kuhusu hali inayojiri nchini Iraq, ambayo ambayo imesababisha hali mbaya za ukosefu wa uhakika na usalama kwa wote?

Ili kupata wema wa amani ni lazima kuwepo kukiri kwa wazi na kwa kutambua kwamba matumizi ya nguvu ni uovu usiokubalika na kwa hayatatui matatizo. “Matumizi ya nguvu ni uongo, kwa vile unakwenda kinyume na ukweli wa imani yetu, ukweli wa ubinadamu. Matumizi ya nguvu yanaharibu kile yanadai kukitetea: heshima, uhai, uhuru wa binadamu”.4 Kinachotakiwa ni juhudi kubwa za kulea dhamiri na kuelimisha kizazi cha vijana kuhusu wema kwa kushikilia kwamba ubinadamu mzima na wa kidugu ambao Kanisa linautangaza na kuuendelea. Huu ni msingi kwa ajili ya utaratibu wa kijamii, kiuchumi na kisiasa unaoheshimu thamani, uhuru na haki za msingi za kila mtu binafsi.

 

Wema wa amani na mafao ya pamoja

 

 5.        Kuendeleza amani kwa kuushinda uovu kwa wema unahitaji tafakari makini juu ya mafao ya pamoja5 na juu ya maana yake ya kijamii na kisiasa. Pale mafao ya pamoja yanapoendelezwa katika kila ngazi, amani inakuzwa. Je mtu binafsi anaweza kupata utimilifu kamili bila kutimiza asili yake ya kijamii, yaani kuwepo kwake “pamoja na” na “kwa ajili ya” wengine? Kwa karibu mafao ya pamoja yanamhusu yeye. Kwa karibu yanahusu kila kila maelezo ya asili yake ya kijamii: familia, mikoa (kanda), madola, jumuia ya watu na mataifa. Kila mtu, kwa namna fulani, anaitwa kufanya kazi kwa ajili ya mafao ya pamoja, kuendelea kutazama nje kwa ajili ya mambo mema ya watu wengine kana kwamba yangekuwa yake mwenyewe. Wajibu huu kwa namna ya pekee ni wa viongozi wa kisiasa katika kila ngazi, kwa kuwa wanaitwa kutengeneza ule muhtasari wa masharti ya kijamii ambayo yanaruhusu na kukuza katika watu maendeleo mazima ya nafsi zao.6

Kwa hiyo mafao ya pamoja yanahitaji heshima na maendeleo mazima ya mtu na haki zake za msingi pamona na heshima na uendelezaji wa haki za mataifa katika kila mahali. Kwa maana hii, Mtaguso wa Pili wa Vatican ulisema “kuendelea kwa hali ya kutegemeana kwa karibu ambayo polepole inajumuisha ulimwengu mzima kunasababisha kuongezeka mafao ya pamoja ya kila mahali… na hii inahusisha haki na wajibu pamoja na heshima kwa jamii yote ya binadamu. Kila kundi la kijamii ni lazima lazingatie mahitaji na jitihada halali za makundi mengine na mafao ya pamoja ya familia nzima ya binadamu”.7 Wema wa binadamu kwa jumla, ikijumuisha vizazi vijavyo, unatoa mwito kwa ajili ya ushirikiano wa kweli wa kimataifa, ambao kila nchi ni lazima itoa mchango kwa ajili yake.8

Baadhi ya mitazamo-punguzi ya binadamu inajaribu kuonesha mafao ya pamoja kama hali ya mafanikio ya kijamii na kiuchumi ikiwa inakosa lengo madhubuti, na hivyo kuyaondolea maana yake ya kina kabisa. Hata hivyo bado mafao ya pamoja yana kipengele madhubuti, kwa kuwa Mungu ni mwisho kamili wa viumbe wake wote.9 Wakristo wanajua kwamba Yesu ameangaza nuru kamili juu ya namna mafao ya kweli ya pamoja kwa ajili ya binadamu yanavyopaswa kufikiwa. Historia inasafiri kumwelekea Kristo na katika yeye inapata kilele: kwa sababu ya Kristo, kwa njia ya Kristo na kwa ajili ya Kristo, kila ukweli wa kibinadamu unaweza kuelekezwa kwenye ukamilifu kamili katika Mungu.

 

 Wema wa amani na matumizi ya mema ya dunia

 

 6.        Kwa kuwa wema wa amani umeunganika maendeleo ya watu wote kwa karibu, matakwa ya kimaadili kwa ajili ya matumizi ya mema ya nchi ni lazima daima yazingatiwe. Mtaguso wa Pili wa Vatican kwa usahihi kabisa ulikumbuka kwamba “Mungu alikusudia ulimwengu na vyote vilivyomo ndani yake kwa ajili ya matumizi ya kila mmoja na watu wote; ili mambo mema ya uumbaji vipatikane kwa wote kwa usawa, kwa haki kama mwongozo na upendo katika uwepo.”10

Kama mwanafamilia ya binadamu, kila mtu anakuwa raia wa dunia, kama ilivyokuwa kwa wajibu na haki mfuatano, kwa kuwa binadamu wote wanaunganishwa na mwanzo mmoja na mwisho mmoja ulio kamili. Kwa kule kuchukuliwa mimba tu, mtoto ana haki na kustahili matunzo na uangalifu; na mtu fulani ana haki ya kutoa vitu hivi. Kulaani ubaguzi, ulinzi wa watoto, utoaji wa misaada kwa watu waliokimbia makazi yao na wakimbizi, na uhamasihaji wa mshikamano wa kimaifa kwa ajili ya wahitaji wote ni kitu kingine zaidi ya matumizi kamili ya kanuni za uraia wa dunia.

 7.    Wema wa amani unapaswa kuonekana leo kama unahusiana kwa karibu na mambo mema ambayo ni mapya yanayotokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia. Haya pia, katika matumizi ya kanuni ya hatima kuu ya mema ya dunia, inahitajika kuwekwa katika huduma ya mahitaji ya msingi ya binadamu. Juhudi zifaazo katika ngazi ya kimataifa zinaweza kutoa utekelezaji kamili wa kivitendo kwa kanuni za hatima kuu ya mema kwa kutoa uhakikisho kwa wote – watu binafsi na mataifa – masharti ya msingi kwa ajili kushirikishana katika maendeleo. Hii inawezekana pale vizuizi na ukiritimba vinavyoweka watu pembezoni vinapoondolewa.11

Amani kama wema itahakikishwa vizuri zaidi iwapo jumuia ya kimataifa itachukua wajibu mkubwa kwa ajili ya mambo ambayo kwa pamoja yanaitwa mema ya umma. Haya ni mema ambayo raia wote wanafaidika nayo moja kwa moja, bila kuyachagua au kuyachangia kwa namna yoyote. Kwa mfano, suala la namna hiyo katika ngazi ya taifa, ikiwa na mema kama mfumo wa mahakama, mfumo wa ulinzi na mtandao wa barabara na reli. Katika ulimwengu wetu suala la utandawazi alioongezeka lina maana kwamba mema ya umma zaidi na zaidi yanachukua tabia ya ulimwengu mzima, na matokeo yake maslahi ya pamoja yanaongezeka siku kwa siku. Tunahitaji kufikiria vita dhidi ya umaskini, ukuzaji wa amani na usalama, kushughulikia mabadiliko ya hali ya hewa na udhibiti wa magonjwa. Jumuia ya kimataifa inatakiwa kuitikia maslahi haya kwa mtandao mpana mwafaka wa mahakama wenye lengo la kusimamia matumizi ya mema ya umma na kumotishwa na kanuni kuu za haki na mshikamano.

 8.    Kanuni ya hatima kuu ya wema inaweza pia kufanya makabala fanisi zaidi uwezekane ili kukabiliana na changamoto ya umaskini, hasa pale tunapofikiria umaskini mkubwa sana ambamo mamilioni ya watu bado yanaishi. Mwanzoni mwa milenia mpya, jumuia ya kimataifa iliweka kipaumbele cha kupunguza umaskini kwa nusu mpaka kufikia mwaka 2015. Kanisa linaunga mkono na kutia moyo dhamira hii na kuwaalika wote wanaomwamini Kristo kuonesha, upendo mpendelevu kwa maskini12, kwa vitendo na katika kila sekta.

Janga la umaskini linabakia kuunganika kwa karibu na suala la deni la kigeni kwa nchi maskini. Licha ya maendeleo muhimu katika eneo hili, tatizo bado halijatatuliwa vya kutosha. Miaka kumi na mitano iliyopita nilitoa wito kwa umma kutazama suala la deni hilo la nchi maskini kwamba “linahusiana kwa karibu na mfululizo wa matatizo mengine kama vile uwekezaji wa kigeni, utendaji kazi mzuri wa asasi kubwa za kimataifa, bei ya mali ghafi na mengine.”13 Hatua za hivi karibuni kutaka deni lipunguzwe, zikiwa zimejikita kwenye mahitaji ya maskini, kwa hakika zimeboresha ukuaji wa uchumi. Hata hivyo, kwa sababu ya mambo kadhaa kiwango hiki cha ukuaji wa uchumi bado hakitoshi, hasa kuhusiana na malengo ya milenia kwa ajili ya maendeleo. Nchi maskini bado zimebaki zikiwa zimenasa katika mduara wa uovu: kipato kidogo na ukuaji hafifu wa uchumi unazuia uwekaji akiba, na hivyo uwekezaji hafifu na matumizi yasiyotosha ya akiba hayasaidii ukuaji wa uchumi.

 9.    Kama Papa Paulo wa Sita alivyosema na kama mimi mwenyewe nilivyosisitiza tena, njia pekee za kuwezesha Mataifa kushughulikia tatizo kubwa la umaskini ni kuyapa rasilimali muhimu kwa njia ya misaada ya kigeni ya kifedha – ya umma na binafsi – iliyotolewa chini ya masharti mazuri, ndani ya wigo wa uhusiano wa biashara ya kimataifa unaosimamiwa kwa haki.14 Kinachotakiwa kwa haraka ni uhamasishaji wa kimaadili na kiuchumi, ambao unaheshimu makubaliano ambayo tayari yamefanyika kwa ajili ya kuzisaidia nchi maskini, na wakati huohuo uko tayari kupitia upya makubaliano hayo ambayo yameonekana kuwa mzigo kwa baadhi ya nchi. Kwa maana hiyo, msukumo mpya unapaswa kutolewa kwa Msaada wa Umma kwa ajli ya Maendeleo, aina mpya za kutoa fedha kwa ajili ya maendeleo zinapaswa kuchunguzwa, bila kujali ugumu wowote wa kazi hiyo.15 Baadhi ya serikali tayari zinatazama kwa uangalifu mbinu za matumaini kwa ajili ya kufanikisha suala hili; juhudi hizi muhimu zinapaswa kuchukuliwa katika roho ya ushirikishanaji wa kweli, kwa kuheshimu kanuni ya ukamilishanaji. Usimamizi wa rasilimali za fedha unaolenga maendeleo ya nchi maskini unapaswa pia kuhusisha uangalifu makini, kwa upaned wa wote wafadhili na wapokeaji wa misaada, kwa hatua muhimu za kiutawala. Kanisa linatia moyo na kuchangia jitihada. Mtu anahitaji tu kutaja mchango muhimu uliotolewa na asasi nyingi za Kikatoliki zinazoshughulikia misaada na maendeleo.

 10.  Mwishoni mwa Jubilei Kuu ya mwaka 2000, katika Barua yangu ya Kitume Novo Millennio Ineunte, nilizungumzia juu ya haja ya haraka ya creativity katika upendo,16 ili kueneza Injili ya matumaini duniani. Haja hii inaonekana wazi pale tunapofikiria matatizo mengi magumu yaliyopo kwenye njia ya maendeleo barani Afrika: migogoro mingi ya silaha, majanga ya magonjwa yanayochochewa na umaskini wa kupindukia, udhaifu wa kisiasa unasababisha ukosefu mkubwa wa usalama. Hizi ni hali za kutisha ambazo zinatahitaji mwelekeo mpya kabisa kwa ajili ya Afrika: ipo haja ya kubuni aina mpya za mshikamano, katika kiwango cha upande mmoja na pande nyingi, kupitia kwa wajibu muhimu kwa upande wa wote, kwa imani kamili kwamba mafaniko ya watu wa Afrika ni sharti muhimu kwa ajili ya ufikiaji wa mafao ya watu wote kila mahali duniani.

Watu wengi wa Afrika wanakuwa wahusika wakuu wa mustakabali wao wenyewe na maendeleo yao ya kiutamaduni, kiraia, kijamii na kiuchumi! Ni maombi yangu kwamba Afrika itakoma kuwa mpokeaji tu wa misaada, na kuwa mpatanishi anayewajibika wa ushirikishanaji wa matumaini na wenye kuzaa matunda! Ufikiwaji wa lengo hili unadai utamaduni mpya wa kisiasa, hasa katika eneo la ushirikiano wa kimataifa. Kwa mara nyingine tena ningependa kutamka kwamba kushindwa kuheshimu ahadi zinazojirudia za Misaada wa Umma kwa ajili ya Maendeleo, swali ambalo bado halijatatuliwa la deni kubwa la kigeni la nchi za Afrika na kushindwa kuzifikiria nchi hizo kwa namna ya pekee mahusiano ya biashara ya kimataifa, kunawakilisha kizingiti kikubwa kwa amani ambacho kinhitaji kushughulikiwa na kutanzuliwa kwa haraka kabisa. Leo zaidi ya wakati wowote ule, sharti muhimu kwa ajili ya kuleta amani kwa ulimwengu kukiri hali ya kutegemeana kati ya nchi tajiri na maskini, kiasi kwamba “maendeleo ama yanakuwa ya kushirikishana kwa pamoja na kila sehemu ya ulimwengu au yanapitia mchakato wa kurudia nyuma kimaendeleo hata yale maeneo yenye maendeleo imara.”17

 Mtapakao wa uovu na matumaini ya Kikristo

 11.  Mkabala na hali nyingi za hatari zilizomo ulimwenguni, Wakristo wanakiri kwa tumaini nyenyekevu kwamba Mungu pekee anaweza kuwapa uwezo watu binafsi na mataifa kushinda uovu na kupata wema. Kwa kifo na ufufuko wake , Kristo ametukomboa na kutununua “kwa bei” (1 Kor 6:20; 7:23), na kuleta wokovu kwa ajili ya wote. Kwa msaada wake, kila mmoja anaweza kushinda uovu kwa wema.

Kwa msingi wa uhakika kwamba uovu hautashinda, Wakristo wanakuza matumaini yasiyoshindwa ambayo yanaendeleza jitihada zao za kukuza haki na amani. Licha ya dhambi za binafsi na za kijamii ambazo zinazosheneza shughuli zote za binadamu, matumaini daima hutoa msukumo mpya wa kushughulika haki na amani, pamoja na hali thabiti ya kujiamini katika uwezekano wa kujenga ulimwengu ulio bora.

Ingawa “fumbo la uchafu” (2 Thes 2:7) lipo na liko hai ulimwenguni, tunapaswa tusisahau kwamba binadamu waliokombolewa wanaweza kuupinga uovu. Kila mwamini, aliyeumbwa kwa sura ya Mungu na kukombolewa na Kristo, “ambaye kwa njia fulani amejiunganisha na kila mwanadamu,”18 anaweza kushiriki katika ushindi wa wema. Kazi ya “Roho wa Bwana anaijaza dunia” (rej. Hek 1:7). Wakristo, hasa waamini walei, “hawapaswi, baadae, kuficha matumaini yao katika kina cha mioyo yao, bali kuyaeleza kwa njia ya maisha yao ya kiraia katika uongofu na vita endelevu ‘dhidi ya wakuu giza hili katika ulimwengu, dhidi ya nguvu za uchafu wa kiroho’ (Efe 6:12).”19

 , 12.            Hakuna mwanamume au mwanamke mwenye mapenzi mema anayeweza kuachana na vita ili kuushinda uovu kwa wema. Vita hivi vinaweza kupiganwa ipasavyo kwa kutumia silaha mwafaka za upendo tu. Pale wema unapoushinda uovu, upendo unatamalaki, na hapo amani inatamalaki pia. Haya ndiyo mafundisho ya Injili, yaliyosisitizwa tena na Mtaguso wa Pili wa Vatican: “sheria ya msingi ya ukamilifu wa binadamu, na vivyo hivyo ya mabadiliko ya ulimwengu, ni amri mpya ya upendo.”20

Jambo kama hilo pia ni kweli katika mazingira ya kijamii na kisiasa. Kuhusiana na hili Papa Leo wa 13 aliandika kwamba wale wenye madaraka ya kutunza amani kwenye uhusiano kati ya mataifa wanapaswa kukuza ndani yao na kuwasha wengine kwa “upendo, mama na malkia wa fadhila zote.”21 Wakristo ni lazima wawe mashahidi waamini wa ukweli huu. Wanapaswa waoneshe kwa maisha yao kwamba upendo ni nguvu pekee inayoweza kuleta ukamilifu kwa watu na jamii mbalimbali, nguvu pekee ya kuongoza mwendo wa historia katika njia ya wema na amani.

Wakati wa mwaka huu uliotolewa kwa Ekaristi, ninaomba wana na mabinti wa Kanisa wapate katika sakramenti kuu ya upendo chemchemi ya umoja wote wa kiroho: umoja pamoja na Yesu Mkombozi na, katika yeye, pamoja na kila binadamu. Kwa kuzaliwa na kifo cha Kristo, ukweli unaokuwa halisi katika kila adhimisho la Ekaristi, tumeokolewa kutoka katika uovu na kuwezeshwa kutenda wema. Kwa njia ya maisha mapya ambayo Kristo ametupatia, tunaweza kutambuana kama kaka na dada, licha ya kila tofauti za lugha, utaifa na utamaduni. Katika neno, kwa kushirikishana katika mkate mmoja na kikombe kimoja, tunakuja kugundua kwamba sisi ni “familia ya Mungu” na kwamba kwa pamoja tunaweza kutoa mchango wetu fanisi wa kujenga ulimwengu wenye misingi ya tunu za haki, uhuru na amani.

 

Kutoka Vatican, 8 Desemba 2004.

 

Yoannes Paulus II