Miujiza
Kisiwani
Na Peter Dominic
WANAKIJIJI wote walikuwa wamepatwa na mshangao mkubwa
baada ya watu kupotea katika mazingira
yasiyo eleweka.
Kila
mmoja alikuwa hajui chanzo cha kupotea kwa watu hao ambapo wapo wengine waliodhani kutoweka huko
kulitokana na nguvu za giza.
Ukweli
ni kwamba upotevu huo ulichangiwa na suala la njaa kali katika eneo hilo na
sehemu pekee ambayo ingekuwa kimbilio ni katika kisiwa cha Shoshwa.
Tangu
enzi za mababu,ilisadikika kisiwa
hiki kuwa kina vyakula vingi. Lakini
hajabu ni kwamba watu waliokwenda kisiwani humo,hawakurudi!
Wazee
vikongwe walikusanyika pamoja katika mkutano ulioitishwa na mtawala wao, Mfalme
Bwile Kitakwete, ambaye kwa upande mwingine alitawala kitabaka.
Mazungumzo
kati yao yaliendelea kutafuta muafaka wa suala lililokuwa likiwasumbua muda
mrefu. Agenda katika mkutano huo ilikuwa ni kwanini watu wote waliokwenda
katika kisiwa cha Shoshwa kilichokuwa Kasikazini mwa kijiji hicho
cha Mategula.
Waliojiita
waganga wa kienyeji na wapigaramli walizishika tunguli zao na kuanza kuagua
kinachowamaliza ndugu zao, kwa amri ya mfalme huyo yeyote ambaye angefanikiwa
kupata jibu la kitendawili katika kisiwa hicho, angepewa robo ya mali ya Mfalme
huyo.
Waganga
walizipiga tunguli zao usiku na mchana, watabiri walitoa maelezo yao lakini
hakuna aliyebahatika kutegua ama kufanikisha kwa namna yoyote siri iliyojificha
katika kijiji hicho.
Ilikuwa
ni jambo la kawaida ufikapo katika kijiji hicho kuambiwa kuwa waedao Shoshwa
hawarudi kamwe. Hivyo ilikuwa ni jambo la kawaida mtu kukutishia kuwa
atakupeleka katika kisiwa hicho endapo ungemfanyia jambo lolote lisilompedeza.
Mkutano
wa siku moja haukutosha kumaliza tatizo hilo, mara kwa mara ilifanyika mikutano
mikubwa ikiwemo ya hadhara na ile ya kawaida acha vile vikao vya kila familia
juu ya muujiza huo wa hatari.
Kadri
vikao vilivyozidi kushamiri ndivyo hali ilivyozidi kuwa mbaya katika himaya ya
Mfalme Kitakwete.
Siku
moja baada ya kumaliza mkutano, mtoto wa
kwanza wa Mfalme aitwaye Lwiza
aliyekuwa akitarajiwa kuwa mrithi wa kiti baba yake, hakuonekana katika nyumba yake ya msonge iliyokuwa
pembezoni mwa jumba la Mfalme Kitakwete.
Hofu
kubwa ilitanda, amri ilitolewa Ikulu ya
Mfalme huyo kuwa haiwezekani mwanae akauawa na wanakijiji wakakaa kimya,
aliamuru ipigwe ngoma watu wakusanyike
na waanze msako hadi mwanae apatikane, awe hai ama amekufa.
Msako
uliingia katika wiki ya nne lakini hakuna lolote la maana lilopatikana zaidi wa
kijana mmoja na mzee wa makamo kuraluliwa na mamba mara walipokuwa wakimtafuta
Lwiza kwenye Mto Ngono.
Vifo
havikuwakumba hao peke yao,pia wanaukoo wengine wa Mfalme wapatao watatu nao
walipoteza maisha katika msako huo wa mtoto wa Mfalme.
Baada
ya kuona watu wanazidi kuuwawa bila mafanikio ya Lwiza kupatikana,msako
ulisitishwa, na amri ilitolewa kwamba
mtu wa aina yoyote asithubutu kwa namna yoyote kutumia maji ya kisiwa
hicho wala kujishughulisha na uvuvi kwa
namna yoyote ile.
Tangu
hapo samaki walikuwa hadimu, watu waliishia kuvua samaki wa mito.
Hata
hivyo ilikuwa ni marufuku kuingia katika
nyumba ya Mfalme.
Watu
wengi walimlalamikia Mfalme wao wakidai
kwamba huenda kuna mambo hakuyatimiza ndiyo maana wamekumbwa na mabalaa hayo.
Hakukuwa
na amani tena kwa Mfalme, maelfu ya watu walikuwa wamepoteza maisha yao.
Wengi walipotea katika kipindi cha njaa
kali iliyoikumba himaya ya Mfalme.