Ugonjwa wa sare wazua manung'uniko
Simba
Na Lilian Timbuka
KLABU
ya Soka ya Simba ya jijini Dar es Salaam, imegubikwa na jinamizi nene baada ya
matumaini ya kutetea Ubingwa wa Tanzaania Bara kuwa finyu kutokana na mwenendo
mbovu wa timu hiyo uliotawaliwa na sare mfululizo.
Wanachama
wa klabu hiyo wameulalamikia uongozi kwa kushindwa kubuni mikakati madhubuti ya
ushindi ili kulibakisha tena taji
Wakizungumza
na Gazeti la KIONGOZI jijini Dar es Salaam, juma lililopita, wanachama hao
ambao hawakutaka majina yao yatajwe gazetini, walisema kwa pamoja kuwa “ugonjwa
wa sare” uliotawala Simba katika mechi mfululizo umesababishwa na
uzembe wa viongozi ambao wanajisahau na kutokuwa makini kutafuta mbinu mpya za
ushindi tofauti na mwaka jana.
Ugonjwa
wa sare umeikumba Simba katika Ligi ya VODACOM, Hatua ya Nane Bora inayoendelea
nchini.
Walisema
kitendo cha uongozi kushindwa kudhibiti nidhamu ya wachezaji, pia kimeonesha
udhaifu katika uongozi na kimechangia kuporomoka kwa kiwango cha uchezaji na
kuifanya timu ijikongoje kwa mfululizo wa sare.
“Tunajua
kwamba Ligi ni ngumu, uongozi nao
umejisahau mno; umeshindwa kubuni mikakati ya ushindi na kudhibiti nidhamu,”
alisema mmoja wa wanachama hao.
Akaongeza,
“Wachezaji wetu sasa hawachezi
Walisema
kushuka kwa viwango vya wachezaji, pia kumechangiwa na wachezaji kuendekeza
starehe na kushindwa kuthamini nidhamu ya mazoezi.
Walisema
hawana tatizo na Kocha wa Timu hiyo, James Siang’a kwani amejitahidi kurudisha
hadhi ya Klabu ya Simba na hivyo, hawana budi kumshukuru.
“Wa kulaumiwa hapa ni viongozi wenyewe
wanaoyafahamu fika mazingira ya
Nahodha
wa Timu hiyo ya “Wekundu wa Msimbazi,” Selemani Matola, alijibu madongo hayo
akisema alikiri kuwapo kwa tabia ya kuendekeza starehe miongoni mwa wachezaji
hali inayowafanya baadhi wajisahau katika mazoezi.
Hata
hivyo, alisema hiyo si sababu kubwa ya wao kutofanya vizuri katika Ligi hiyo.
Alisema
Ligi ya mwaka huu, ni ngumu mno kwa kuwa timu nyingi za mikoani zikuja juu
kiushindani.
"Tunachotakiwa
ni kubuni mbinu mpya za ushindi badala ya kukaa na kuanza kutupiana lawama
kwani hazitasaidia kuleta maendeleo ya timu," alisema.
Aidha,
aliwaomba wanachama wa Klabu ya Simba kuwa na subira na wakati mwingine,
wajaribu kukubali matokeo badala ya kuona kwamba timu
Aliongeza
kuwa, hata timu zingine ambazo zinazopambana na Simba, pia zinahitaji ushindi
na sio kufungwa
Hadi
juma lililopita, Timu hiyo ya Msimbazi ilikuwa ikishikaa nafasi ya nne katika
msimamo wa ligi kwa kuwa na pointi 15. Ilicheza mechi 10, ikashinda mechi 3 na
kutoka sare katika mechi 6. Ilikuwa imefungwa katika mechi moja.
Hata
hivyo Jumatano iliyopita katika pambano baina ya Simba na 82 Rangers
ya Shinyanga lililofanyika katika Uwanja wa Taifa.jijini
Watani
wa Jadi wa Timu hiyo, Yanga ya
Hata
hivyo, ili Wekundu hao wa Msimbazi waendelee kutetea ubingwa wao, itabidi
washinde mechi zote zilizosalia na
Endapo timu za Mtibwa na Yanga
zitapoteza michezo
Ubungo
Shooting yaifanyia
'roho mbaya' Sanaa Sports
Na Msafiri Mdami, DSJ
TIMU ya Soka ya Ubungo Shooting Stars imeifanyia roho mbaya klabu
ya soka ya Sanaa Sport zote za Dar es Salaam, kwa kuifunga mabao 3-0,
katika mchezo wa kirafiki uliofanyika wiki iliyopita katika Uwanja wa UFI,
Bao la kwanza la Ubungo Shooting Stars lilipatikana kunako dakika ya 10 baada ya
mchezaji Ally Issa kuwalamba chenga mabeki wawili wa Sanaa Sports
na kisha kuachia mkwaju mkali uliotinga kimiani.
Dakika saba tangu kuanza kwa kipindi cha pili, mchezaji huyo machachali,
aliiongezea timu yake bao la pili baada ya kuvunja mtego wa kuotea na hivyo,
kufunga bao kwa urahisi.
Bao la tatu liliwekwa kimiani na mshambuliaji Hassan Mpemba katika
dakika ya 70, baada ya kutokea piga nikupige katika lango la Sanaa Sports na
hatimaye Mpemba kufumua shuti lililojaa wavuni.
Hata hivyo, Sanaa iliongeza ushambuliaji katika kipindi cha mchezo japo
haikuambulia bao na hivyo, Ubungo Shooting kuondoka uwanjani kifua mbele kwa
kufunga bao 3-0.
Wakati huo huo: Uongozi wa Nyagatwa Inn, iliyopo
njia panda ya Uwanja wa Ndege,
Mlezi wa Klabu hiyo hiyo, Bibi. Grace Chacha, alisema wameamua kuanzisha
mchezo huo ili kuuinua na kuutangza kwani hadi sasa bado haujapata washiriki
wengi.
Hivi sasa klabu hiyo ikiongozwa na Kapteni wake, Aldoph, inajindaa kwa
ziara ya mechi za kirafiki wilayani Kibaha mkoani Pwani.
Hadi sasa imekwisha
cheza mechi tatu za kirafiki na kushinda katika michezo yote.
Waamuzi wa Tanzania si
'mabomu'- FRAT
l Yahoji:Mbona kuna wenye beji za FIFA?
l Wataka makocha waandae timu ipasavyo;
waache lawama
Na Lilian Timbuka
CHAMA cha Waamuzi wa Soka nchini
(FRAT), kimepinga vikali kauli iliyotolewa hivi karibuni na Kocha wa Timu ya
Simba, James Siang’a kuwa waamuzi wa hapa nchini hawana uwezo wa kuchezesha
mchezo huo.
Akizungumza na KIONGOZI jijini
Dar es Salaam, Katibu Mkuu Msaidizi wa FRAT, Lishie Liunda, alisema Tanzania
ina waamuzi waliobobea katika kuchezesha kabumbu na kwamba, baadhi yao wapo
wenye beji za Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA).
“Sikubaliani na kauli ya
Siang’a kwani hapa
Aliyataja majina ya waamuzi
ambao wana beji za FIFA kuwa ni pamoja na Omar Abdulkadir, Emmanuel Chaula,
Pascal Chiganga, Victor Mwandika na Fredeick Tibaijuka.
Waamuzi wengine ni David
Nyandwi, Charles Mchau, Soud Abdi pamoja na yeye mwenyewe Liunda.
Alisema imekuwa ni tabia ya
baadhi ya Watanzania hususan makocha wa timu, kuwalaumu waamuzi pindi timu zao
zinapofungwa na kuwasifia pale wanapofunga.
Akitoa mfano wa kauli ya
Kocha wa Yanga, Jack Chamangwana, Linda alisema kuwa, Chamangwana aliwahi
kutamka kuwa waamuzi wa Tanzania hawafai kuchezesha mechi kubwa, bali wanafaa
kuchezesha Ligi Daraja la Pili, lakini timu hiyo ilipopambana na Tukuyu Stars
na kushinda kwa mabao mengi, aligeuka na kuanza kumsifia mwamuzi wa pambano
hilo bila kukumbuka kuwa awali alisema kuwa hafai.
“Unajua timu zetu za Tanzania
huwa daima zinapenda ushindi tu na pindi timu ikifungwa, basi lawama zote huwa
zinakuja kwa waamuzi wa mchezo huo siku zote,” alisema Liunda.
Alisema kinachotakiwa ni
makocha kuziandaa vema timu zao badala ya kujenga dhana potofu ya kuwalalamika
waamuzi wa michezo yao ili kuficha udhaifu wa makocha hao.
Hivi karibuni, Kocha Siang’a
alitoa kauli kuwa waamuzi wa Tanzanaia hawana uwezo wa kuchezesha mashindano
mbalimbali yakiwemo ya Ligi Kuu, hivyo akapendekeza waletwe waamuzi kutoka nje
ya nchi.