Twiga Stars yalilia mechi za kirafiki
Na Anthony Ngonyani
TIMU
ya Soka ya Taifa ya Wanawake nchini
(Twiga Stars) imekitaka Chama cha Soka nchini (FAT), kuiandalia timu michezo mbalimbali ya kirafiki ili iitumie
Akizungumza na KIONGOZI hivi
karibuni mshambuliaji hatari wa timu hiyo, Ester Chabruma maarufu kwa jina la Lunyamila,
alisema michezo ya kirafiki itawawezesha kufanya vizuri zaidi kwani itaiongezea
ujuzi Twiga Stars.
Alisema timu ya Taifa ya
“Hata kama inatisha sisi tuna
uwezo mkubwa kuifunga timu hiyo, kinachotakiwa ni kufanyiwa maandalizi
bora,”alisema.
Hata hivyo mchezaji huyo aliipongeza FAT kwa kuiweka mapema kambini timu hiyo.
Prisons yaitaka FAT kuwa makini na
ratiba
Na Anthony Ngonyani.
TIMU ya soka ya Prisons
imekilalamikia Chama cha Soka Tanzania (FAT), kuhusu kushindwa kupanga ratiba
nzuri ya mzunguko wa awamu ya pili ya Ligi Kuu Hatua ya Nane Bora.
Malalamiko hayo yametolewa hivi karibuni na Meneja wa timu
hiyo Bw. Hassani Mlilo wakati alipokuwa akizungumza na Gazeti hili jijini
Dar-es-Salaam juu ya mashindano hayo.
Alisema ratiba hiyo inaibana
Alisema timu ya Prisons
italazimika kusafiri kila itakapocheza mchezo mmoja wa ligi hiyo ambayo ilianza
kutimua vumbi wiki iliyopita.
Aliongeza kuwa, kutokana
na safari hizo zitakazomalizika pindi ligi hiyo itakapo malizika mapema mwezi
ujao wachezaji wake watachoka na kushindwa kutafakari makosa yaliyojitokeza
wakati timu hiyo ilipokuwa imeshuka dimbani na kukosa muda mazoezi.
Mlilo aliongeza kusema
kuwa kutokana na mpango huo mbaya wa ratiba, kuna hatari kwa timu yake
kutofanya vizuri hasa ikizingatiwa
kuwa inao wachezaji wengi ambao ni
majeruhi.
Alisema kuwa hakuna
sababnu nyingine ambayo itakayopelekea timu hiyo kufanya vibaya zaidi ya hiyo,
hivyo wanakitaka FAT kufanya wawezalo
ili kubadili ratiba.
Akasisitiza kuwa kufanya
hivyo, kutaiokoa timu hiyo ambayo sasa iko katika wakati mgumu wa katika
kufanya vizuri Ligi Kuu ya VodaCom.
Prisons ni moja kati ya
timu ambazo ni tishio ambayo imeweka rekodi kwa kutoa dozi kwa timu kubwa
ambazo ni Simba na Timu ya Yanga zote za jijini Dar es Salaam.
Imefanikiwa kujiweka
katika nafasi nzuri ya kuweza kuingia Tabora na kuweza kushiriki Kombe la
Muungano.
Tunajisikia vibaya timu za Taifa zinapofungwa-Wizara
l Yaionya Twiga Stars isifuate mwenendo wa
Taifa Stars
Na Lilian Timbuka
SERIKALI
imesema kuwa inajisikia vibaya pindi timu zilizofikia ngazi ya Taifa katika
michezo mbalimbali, zinapofungwa na nchi nyingine.
Kauli hiyo ilitolewa na Naibu
Waziri Wizara ya Kazi na Maendeleo ya Vijana na Michezo, Mudhihir Mudhihir
wakati alipotembelea kambi ya timu ya mpira wa miguu ya
Wanawake ya Twiga Stars iliyoweka kambi katika hosteli za Jeshi
la Wokovu Jijini Dar es Salaam.
“Tunajisikia vibaya
“Timu hii imeweza kufanya vizuri licha ya
kukumbana na mazingira magumu katika kambi pindi ilipopambana na timu ya
Hata hivyo, Naibu Waziri aliwaasa akinadada
hao wa Twiga Star kuwa na moyo wa ustahimilivu na kujituma wawapo kwenye
mashindano makubwa
Mudhihir aliwaomba Watanzania ambao wana
mapenzi na timu zao za Taifa kuichangia timu hiyo ambayo tayari imekwishafunguliwa
Akaunti na Baraza la Michezo la Taifa (BMT), na akasema tayari kwenye akaunti
hiyo kuna kiasi cha sh.500,000 kwa ajili ya timu hiyo.
Twiga Star inatarajia kupambana na timu ya
wanawake kutoka nchini Zimbabwe Septemba 21, mwaka huu mchezo utakaofanyika jijini
Endapo itafanikiwa kuitoa
Tarimba ailaumu FAT
Na Lilian Timbuka
Kufuatia
kipigo kikubwa kilichoipata timu ya Taifa ya
Akizungumza jijini
Alisema endapo FAT imeshindwa
kuongoza soka nchini ni vema iwaachie wadau wengine wenye uchungu na timu za
nchi hii, “Sijui ni kwanini wanang’ang’ania hii aibu ambayo timu yetu imekuwa
ikifedhehesha kila mwaka na kubakia kulalamikia waamuzi wa kila mchezo
wanaochezesha mechi za Stars,” alinung’unika Tarimba.
Alisema Stars iliyokwenda
Alihoji,
“Uliona wapi timu inayojiandaa na mashindano makubwa ikafanya mazoezi kwa mechi
za majaribio na timu za ligi ya soka ya Daraja la kwanza nchini kwake badala ya
kuitafutia timu mechi kubwa za kimataifa?”
Alisema
yeye binafsi hakuona sababu ya FAT kuivunja ile timu ya kwanza, “FAT
wangetafuta namna ya kukosoa makosa ambayo yalionyeshwa na timu ile, sasa
wamefanya nini wavunje basi na hii iliyofungwa mabao 4”, alisema Tarimba.
Hata
hivyo alisema kwa ushauri tu, anakishauri FAT kujaribu kuziandaa timu zake za
Taifa kwa kuzitafutia mechi za kirafiki za kimataifa na si
Timu ya Taifa ambayo inashiriki Mashindano ya Fainali za
Kombe la Mataifa ya Afrika, hivi karibuni ilipata kipigo cha kufedhehesha
kutoka kwa mwenyeji wao timu ya Taifa ya
Mtambo
wa Gongo aapa kuua mtu
Na Steven Charles
BINGWA wa ndondi
wa IBF, barani Afrika katika uzani wa Kati, Maneno Oswald (Mtambo wa Gongo),
amesema washabiki wa Bondia Francis Cheka, wajiandae kubeba maiti kwani
atamdunda vibaya katika pambano lao litakalofanyika Septemba 29, mwaka huu.
Bondia Maneno aliyezungumza na KIONGOZI katikati ya
juma jijini Dar es Salaam, atapanda ulingoni katika Ukumbi wa Friends Corner
uliopo Manzese, Dar es Salaam, Septemba 29, mwaka huu akijindaa kupambana na
Rashid Matumla.
Mwezi Julai, mwaka huu, Bondia Maneno alipambana na
Bondia Cheka, ambapo Maneno alitolewa katika raundi ya nane huko Morogoro.
Alisema, endapo Cheka atamdunda katika pambano hilo,
atajiuzuru mchezo huo kwa kuwa Bondia huyo sio saizi yake.
“…Ushindi wake siukubali kwa sababu halikuwa pambano…
yale yalikuwa mazoezi tu; lingekuwa pambano ningesaini mkataba kabla ya mwezi
na nikajua nachezea shilingi ngapi, lakini sikujua,” alisema Maneno.
Akaongeza, “Kama alinipiga kweli, tutaona sasa… najua
walimpa ushindi katika mazoezi hayo wanayoita mechi kwa sababu wanataka
kumnyanyua kupitia mazoezi hayo tuliyochezea kwenye mchanga.”
Akisisitiza azima yake ya kumdunda Cheka, Maneno
alisema, ”Washabiki watakaokuwapo uwanjani wajiandae kubeba maiti kurudisha
Morogoro. Hawezi kunipiga kwa sababu hana mkanda wowote. Hawezi kunipiga kwanza
yeye sio saizi yangu na mimi ninacheza naye kama mazoezi tu, ili kujiandaa
kucheza na Rashid. Huyo (Matumla) na akina Joseph Marwa na wengine kutoka nje
ya nchi, ndio saizi yangu”.
Mwaka juzi Bondia Rashid Matumla na Maneno Oswald,
walipambana katika Ukumbi wa PTA Dar es Salaam ambapo Matumla aliibuka mshindi
kwa KO katika raundi ya tisa.
Maneno Oswald anadai ana usonga wa kuthibitisha kuwa
yeye ni mbabe dhidi ya Matumla na kwamba, pambano baina yake na matumla
linalotarajiwa kufanyika hivi karibuni, ndilo litalithibitisha ubabe wake.