Ahadi
ya Brigedia Kirigiti isiwe 'danganya toto'
TUNAZIPONGEZA juhudi kubwa zinazofanywa na Jeshi la
Kujenga Taifa (JKT) za kuhakikisha amani iliyopo nchini inadumu.
Hivi
leo katika Ulimwengu uliojaa vita, bado Tanzania inaonekana ni miongoni mwa
nchi chache zenye upendo, amani na umoja.
Kazi
hii siyo ya mchezo, ni ngumu inayohitaji moyo wa pekee na bila kuwa na jeshi
imara, bila shaka hata
Pamoja
na pongezi hizo, Jeshi hilo sasa linaonekana kuingiliwa na mdudu mbaya na hatua
za haraka zisipochukuliwa, sifa zote hizo zitatoweka.
Tunasema
hivyo kwani baadhi ya wanajeshi wa Jeshi
la Kujenga Taifa, kwa bahati mbaya sasa wamekuwa wakitumia jina la Jeshi
lao kuwanyanyasa wananchi na jamii kwa jumla.
Tukio
la hivi karibuni lililotokea jijini Dar es Salaam, ambapo wanajeshi wa JKT wapatao 12 walilizingira eneo la
Kariakoo na kuanza kuwashambulia Askari wa Jiji kwa madai kuwa askari hao wa
Jiji walikuwa wamevaa sare zinazofanana na zao, ni la kushangaza.
Katika
purukushani hizo, Wanajeshi hao mbali na
kuwachalaza bakora Askari wa Jiji, pia walimvua nguo mmoja wa askari wa Jiji na
kumuacha na nguo yake ya ndani.
Swali
tunalojiuliza ni kwamba, hivi kweli uongozi wa JKT ulishindwa nini kufanya
mazungumzo na uongozi wa Jiji na kufikia muafaka juu ya sare ipi itumike baina
ya pande zote mbili, badala ya askari hao kufanya mashambulizi ya aibu kiasi kile?
Wanajeshi
hao walifahamu fika kuwa wanachokifanya ni kinyume cha sheria za nchi na ndiyo
sababu waliamua kuharibu kamera ya mpiga picha wa kujitegemea ambaye alikuwa
akifuatilia tukio
Bila
shaka waliona picha hizo zikionekana kwenye vyombo vya habari, jamii itajenga
hisia mbaya dhidi ya JKT.
Kibaya
zaidi wafanyabiashara wa eneo hilo la Kariakoo baada ya kushuhudia askari
anavuliwa nguo, ilibidi waingilie kati. Wakachukua madaraka na sheria mikononi
na kuungana na askari wa Jiji kuwashambulia wanajeshi hao.
Sisi
tunasema, tabia hii iliyoanzishwa na askari hao wa JKT, ni hatari na iliyo na harufu ya damu.
Ikumbukwe
pia kuwa, askari wa Jiji ndio wanaohusika na suala zima la kuhakikisha Jiji la
Dar es Salaam linakuwa safi ikiwa ni pamoja na kuhahikisha kuwa wafanyabiashara
hao wanafanya shughuli zao katika maeneo waliyotengewa kufanyia biashara zao.
Kufuatia
kitendo cha wafanyabiashara hao kuungana
na askari katika kupambana na wanajeshi, upo uwezekano mkubwa wa shughuli za
kusimamia zoezi la usafi kukwama kwani tayari askari wa Jiji na
wafanyabiashara wameisha jenga ‘undugu’
hasa ikizingatiwa kuwa akufaaye kwa
dhiki, ndiye nduguyo.
Kuna
usemi kwamba "Usipo ziba
Pamoja
na kauli nzuri iliyotolewa na Msemaji wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Brigedia Jenerali
Philimon Kirigiti kwa vyombo vya habari kuwa Wizara yake itawashughulia
wahusika kwa kulizalilisha Jeshi la Kujenga Taifa, ni matumaini yetu kwamba
kauli hiyo haitakuwa ‘danganya toto’.
Watanzania
tumezoea kuambiwa na viongozi wetu kupitia vyombo vya habari kwamba watachukuwa
hatua kwa watu ama vikundi vinavyo kwenda kinyume na sheria za nchi, lakini
baada ya kutolewa tamko, hatua ama maendeleo ya adhabu hizo huwa hayatangazwi
tena.
Hii
ni sawa na watoto wanapo pigana na ikatokea mmoja akaenda kushtaki mwenzake kwa
mzazi ama mlezi wake, halafu eti katika kumridhisha mtoto aliyeshitaki, basi
mzazi huyo anamwambia mtoto mlalamikaji "Mwangu ndiyo kakupiga! Basi
nyamaza akija nitampiga".
Sasa, mtoto kwa kuridhisha na kauli hiyo, mtoto huyo
huondoka kwa furaha iliyojaa matumaini ya kutendewa haki.
Yetu
sisi siyo matumaini ya ahadi tupu, tunategemea Brigedia Generali Kirigiti
hapendi hao vijana wake wachache waharibu sifa nzuri ya JKT nzima.
Tafadhali, mapema, mapema, mchuzi huu
unywewe; kabla haujachacha.
Kwaheri Baba
Mwanyika, Karibu Baba Maluma
1. Mpendwa Baba Mwanyika, tamko ulilitoa,
Kustaafu kazini, umri umeshatimia,
Hata sisi tunaona, muda umeshawadia,
Kwaheri Baba Mwanyika, karibu Baba
Maluma.
2. Kustaafu sio tamati, bado tunakuhitaji,
Njombe tunakushukuru, kazi ulofanya
fiti,
Hatuna cha kukulipa, Mungu
atakubariki,
Kwaheri Baba Mwanyika, karibu Baba
Maluma.
3. Kazi
uliyoifanya, ilikuwa ni kabambe,
Neno
ulilihubiri, hapa Kanisani Njombe
Mkate
ulitulisha, na divai mu kikombe
Kwaheri Baba Mwanyika, karibu baba Maluma.
4. Mwanyika kafanya mengi, yasoweza
lesabika,
Kanisa kuliongoza, miongo mitatu
sasa,
Kanisa ulilijenga, tusipate taabika
Kwaheri baba Mwanyika, karibu baba
Maluma.
5. Ulienda kotekote hata kusikofikika,
Jimbo lote twakujua, kwa jina lako
Mwanyika,
Matembere wanakujua, Ikonda wewe
Mwanyika
Kwaheri baba Mwanyika, karibu baba
Maluma.
6. Milimani ulienda, mabondeni ukashuka,
Wa sunji na wa Mundindi, uwemba hadi
kisinga,
Kipengere Lugarawa, Igwachanya na Usuka,
Kwaheri baba Mwanyika, karibu baba
Maluma.
7. Mara ulipotangaza kustaafu hiyo kazi,
Mungu akatupa macho kwa wake watenda
kazi,
Akamuona Maluma, anafiti hiyo kazi
Kwaheri baba Mwanyika, karibu baba
Maluma.
8. Ndipo
kamtuma Papa, atangaze hadharani,
Naye hakulaza damu, akatoa redioni,
Jina tukalisikia twamshukuru Manani,
Karibu baba Maluma, kwaheri baba
Mwanyika
9. Atafuta
nyayo zako, sisi tunamuamini,
Elimu
anayotosha, tena yeye ni makini,
Mkufunzi
si mdogo wa pale seminarini,
Karibu baba
Maluma, kwaheri baba Mwanyika.
10. Papa ameona mbali, hata akamteua,
Hata mimi namjua ndo mana nakupa
shua,
Maluma anatufaa, shetani kumbutua,
Karibu baba Maluma, kwaheri baba
Mwanyika.
11. Maluma Karibu
Utufundishe kusali Mungu wetu
tumwombe,
Utufundishe ibada, sio kucheza
likembe
Karibu baba Maluma, kwa heri baba Mwanyika.
12. Wino umemalizika, kalamu naweka chini,
Nami sasa nakitoa, nenda zangu
kanisani,
Mhariri
nashukuru, kuniweka gazetini
Karibu baba Maluma, kwa heri baba Mwanyika
Na Sir, Ephraim J. Sanga (Baba Filo)
Silver Tailoring centre
NJOMBE
Maisha ya kiroho na Kondomu
haviendani
1. Tafuteni mtapata, ombeni mtapewa,
Popote mkiniita, kwangu
mtafunguliwa,
Njia mtakayopita,
2. Kuna
mambo mengi bora, hapa nchini duniani,
Na mengine yaso bora, naomba tuyaacheni,
Akili ni kitu bora, kuliko mali
jamani
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
3. Tusisome kwa papara, tena kwa
kurukaruka,
Tulia tafuta sara, Mungu peke
katanka,
Utii ni kitubora, kuliko mali
jamani.
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
4. Musa
toka mlimani, Alitufanyia kazi,
Na
kweli ndugu zanguni, ya nne twasoma wazi
Kwa
maisha ya mbinguni tuwaheshimu wazazi
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
5. Tuwaheshimu
wazazi kwa maisha ya mbinguni
Tukawatii
wazazi kwa dhati na kwa makini,
Wao
ni yetu mizizi kwa chakula cha mbinguni
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
6. Wametuzaa
wazazi, nakutupa tunzo bora,
Juu
chini ya wazazi, Twapata kipaimara,
Ni
kwa haki bila wizi, leo waumini bora,
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
7. Matunda
Mifano huweka wazi, Watoto
wafate
Katika kundi la mbuzi, mwanawe
awe kondoo
8. Mungu wetu tumwamini, Neno
Asema tumwabuduni, na chochote
hafanani
Asema usizini hata kama ni moyoni
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
9. Tungo
yangu akisoma, inamisha kichwa chini
Kwa busara na hekima, utafakari moyoni,
Kwa kutumia salama twampongeza
shetani
Kama kweli muumini leo kondom
zanini?
10. Tamaa tuziacheni, jamani tafadhalini,
Mndoa wako nyumbani, ni mzuri
kama nini
Ukiranda mitaani, utaingia
wimbini
Kama kweli muumini leo kondom
zanini?
11. Eti maparokiani tuzitangaze salama,
Hatuna haya usoni, kukaribisha
kiyama
Kwa dhati tukiamini kwa Yesu
yote salama
Kama kweli muumini leo kondom
zanini?
12. Wala sioni msala, kukuonyesha pengine,
Fungua chuo cha sala,
kurasa sabini na nane,
Pale
tumepewa sal, ni namba kumi na nane
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
13. Wapendwa ndugu zanguni, tuangalie nyakati
Uwapo
majaribuni, Mwombe Mungu uthabiti
Utamshinda
shetani, ukikemea kwa dhati
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
14. Hebu ndugu fikiria, Mchele umepembua,
Mawe yote umetoa, na chuya umeondoa,
Mwingine
anatokea, mchanga anamwagia
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
15. Watu
wote Tanzania, Janga hili twalijua,
Mikakati
twaandaa, kwa sala kuliondoa
Hatujalimalizia,
Kondomu zinaingia
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
16. Kwa
dhati mnatambua, kila mtu ana dini,
Kama
Mungu twamjua, kondom sisi zanini?
Naomba
kuwaambia, zisitawanywe nchini
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
17. Hebu
kwanza fikiria, uzinzi pia ni dhambi
Kondomu
wazitumia, umeisahau dhambi,
Eti
umepata njia yakukwepa hili wimbi
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
18. Ilitakiwa
kwa Mungu si baa, aweza kuliondoa,
Ndugu
yangu na jamaa, ujumbe wangu pokea,
Yeye
tukimlilia kweli atatusikia
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
19. Mvua
isipotua, Sala tunakimbilia,
Na
kweli hutusikia wanawe kutuokoa,
Jamani na hili baa hawezi
kutukataa,
Kama
kweli muumini leo kondom zanini?
20. Usiku
huu wa manane nimerishiwa mawazo,
Rudia
beti ya nane, tena kwa msisitizo
Hekaluni
tuonane, kuzianza sala hizo
Na Simon A. Nsekella,
C/O Ally Kissiwa,
S.L.P
IRINGA