CHAYODE ilivyo jidhatiti kuelimisha umma
kuhusu umiliki ardhi
MIONGONI
mwa mambo yanayoonekana kuwa sugu katika jamii, ni suala la kugombea ardhi.
Suala hili hutokea ama baina ya nchi na nchi, kabila na kabila, wakulima na
wafugaji, na hata kati ya ndugu na ndugu. Katika Makala haya Lilian Timbuka anaeleza zaidi.
HIVI sasa Mahakama
mbalimbali nchini zimejaza kesi zinazohusiana na masuala ya migogoro ya ardhi.
Mara nyingi kesi hizi zimekuwa baina ya wanafamilia au wana ukoo walioshindwa
kupata muafaka wao wenyewe kuhusu eneo wanalokuwa wamedhulumiana au
wameingiliana.
Kwa
upande wa wafugaji huhitaji eneo kwa ajili ya malisho ya mifugo wao, wakati
wakulima huhitaji eneo
Hali
hii ikichochewa na mabadiliko ya hali ya hewa, ndiyo kichocheo hasa cha mgogoro
wa ardhi baina ya wakulima na wafugaji.
Tukigeukia
upande wa mgogoro wa ardhi baina ya nchi na nchi, hii huja baada ya nchi moja
kutaka kukalia na hata kuvuka mipaka ya nchi iliyopo na kuingilia eneo la nchi
jirani
Madhara
ya mgogoro huu baina ya nchi na nchi
kugombea mipaka, ni makubwa kwa jamii.
Licha
ya kuleta mtafaruku mkubwa miongoni mwa jamii, lakini pia migogoro
Migogoro
ya ardhi ni suala linalokithiri miongoni mwa wakulima na wafugaji na mfano bora
ni wafugaji wa jamii za Kimasai.
Mingine,
ni migogoro inayohusisha koo na koo
Migogoro
baina ya pande hizi imekuwa mikubwa kiasi cha
kusababisha mauaji ya watuwengi.
Mikoa iliyoathirika kwa kiasi kikubwa na
migogoro ya namna hii ambayo husababisha hata mauaji na wakimbizi wa ndani ya
nchi, ni pamoja na Arusha, Morogoro na Mara.
Ugomvi
baina ya Walenchoka na Wanchari mkoani Mara ulisababisha vifo na majereha kwa
watu wengi. Hili ni jambo lilo bayana kwa Watanzania.
Miongoni
mwa matukio ya kugombania ardhi ni lile
lililotokea mkoani Manyara katika wilaya ya Babati (enzi hizo Mkoa wa
Arusha), wakati mkoani Mara makabila ya Walyanchori na Walyanchoka waliuana
kutokana na kugombea ardhi ambapo ilisababisha zaidi ya vifo vya watu wapatao
35 na watu wengine zaidi ya 80 kupigwa mapanga na kuachiwa majeraha ambayo
yamepelekea kuwa na vilema vya maisha na huko
Morogoro katika Wilaya ya Kilosa
Matukio
kama hayo yalitokea baina ya wakulima na wafugaji yalisababisha madhara makubwa
kwani kijiji kilichokuwa kikaliwa na wakulima zaidi ya 1’500, kiliteketezwa kwa
moto.
Mapigano
hayo hayakuisha kwa kijiji kuchomwa moto pekee, bali ilifikia wakati wakulima
na wafugaji hao wakaanza kuuana kwa kutumia silaha
Hata
hivyo, ilidaiwa kuwa takribani 45 walikuwa wameuawa. Japo watu wengine ambao
idadi
Hivi
sasa kuna fukuto lingine la mgogoro wa ardhi linalofukuta katika Kijiji cha
Kibwaya kilichopo katika Wilaya ya Morogoro Vijijini.
Familia
zipatazo 171 zimedaiwa kutakiwa kuhama katika kijiji hicho kutokana na kile
kinachodaiwa kuwa kijiji kimeuzwa kwa raia mmoja mwenye asili ya Kiasia.
Ardhi hiyo inayogombewa na wakazi hao ina
ukubwa wa ekari zipatazo zaidi ya 1,000 ambazo wao wanazitumia kwa ajili ya
kilimo na ufugaji.
Tatizo
kubwa linakuja kuonekana kuwa ni wananchi walio wengi kutofahamu sheria za umilikaji
ardhi japokuwa wapo wataalamu wa suala
Kutokana
na matatizo kuongezeka kila wakati, hivi sasa vikundi na mashirika mbalimbali
vimejitokeza kuelimisha umma kuhusu sheria za umilikaji wa ardhi hasa katika
mikoa ambayo tatizo
Miongoni
mwa vikundi hivyo ni Shirika la
Maendeleo kwa Vijana na Watoto
(CHAYODE), ambalo limeanza kutoa elimu ya haki ya umilikaji wa ardhi
katika wilaya mbalimbali za Mkoa wa Morogoro.
Mkurugenzi
wa CHAYODE, Ramadhani Omari Timu, anasema wakati shirika
“Shirika
letu lililenga kushughulikia haki na maendeleo ya mtoto na kuwasaidia vijana
katika shughuli zao halali ili kwajiletee maendeleo,” alisema.
Akaongeza
kuwa, lengo lingine lilikuwa kuwaunganisha na kujenga ushirikiano miongoni mwa
watoto na vijana wa
Anasema
shirika
“Tumekuwa
na shughuli nyingi ambazo tunazifanya kama vile kuandaa na kuendesha mafunzo
kwa vijana juu ya shughuli wazifanyazo ili kuboresha na kuimarisha ujuzi wao na
pia, tunafanya utafiti wa masuala ya kielimu, kiutamaduni, kiuchumi na kijamii
unaoweza kuwasaidia watoto na vijana kuboresha maisha yao.”
Alisema
katika kutimiza malengo yake, Shirika
“Tumeona
kuwa mtoto akikua anahitaji kumiliki ardhi, na pia hata vijana wanaohitimu
masomo ya msingi au sekondari vijijini huhitaji kutumia ardhi katika shughuli
za maendeleo,”anasema.
Anasema
tatizo kubwa kwa makundi hayo lilikuwa katika suala la kujua sheria ya kumiliki ardhi kwani wengi
wamezoea kuwa alipokuwa analima baba yake, naye atalima hapo, yaani anarithi
ardhi sasa inapotokea uvamizi matokeo yake huwa ni mapigano yanayoonekana siku
hizi.
Aliongeza
kuwa, kutokana na hali hiyo, watu wanaotetea haki za watoto na vijana wameona
umuhimu wa kutoa elimu ya haki ya msingi ya kumiliki ardhi kwa wananchi na
wameanzia na Mkoa wa Morogoro.
Anasema
Shirika
“Tumeendesha
mafunzo ya haki ya ardhi kwa viongozi wa vikundi mbalimbali vya sanaa ili
wakayatumie katika vikundi vyao, kuwaelimisha wananchi wa maeneo
Alisema
wanatumia zaidi sanaa katika shughuli zao kutokana na ukweli kwamba hiyo ni
njia rahisi ya kufikisha ujumbe kwa wanajamii.
Timu
alisema mafunzo hayo ya haki ya ardhi yalifanyika katika Tarafa ya Mang’ula
katika Wilaya ya Kilombelo ambapo mara baada ya mafunzo hayo, wananchi walipata
nafasi ya kuona michezo ya kuigiza inayoonesha migogoro ya ardhi na wao
waliweza kutoa maoni
Mafunzo hayo yalilenga hasa katika utamaduni na sanaa, sanaa
kwa maendeleo, uongozi wa vikundi vya sanaa, wanawake na maendeleo ya vijana na
wanawake, sheria ya ardhi namba 4 na 5 ya mwaka 1999.
Na Mwandishi Wetu
Inatoka Toleo Lililopita
Umaskini wa kupindukia unachochea ukiukaji wa haki za binadamu
ulimwenguni. Katika kwenda sambamba na kanuni ya uziada, maskini ni lazima
wasikilizwe juu ya masuala mbalimbali na wawe ni kiini cha mipango mahali
walipo, kitaifa na kimataifa kwa ajili ya maendeleo endelevu. Watu wanaoishi
katika umaskini lazima wachukuliwe
Moja ya vitu muhimu kwa uwepo wa mwanadamu ni maji. Leo idadi kubwa ya
watu wanakabiliwa na upungufu mkubwa wa maji na ukosefu wa huduma za usafi.
Wajibu wa msingi wa kuweka usawa na matumizi endelevu, utunzaji na usimamizi wa
rasilimali za maji uko mikononi mwa serikali.
Katika mapambano ili kuondoa umaskini, maji hutimiza dhima muhimu si tu
kuhusiana na afya lakini pia
Kipaumbele kikubwa kingine katika maendeleo endelevu ni maendeleo
vijijini. Maeneo ya vijijini yanabeba zaidi ya nusu ya idadi ya watu wote
ulimwenguni na watu maskini wanaoishi katika maeneo haya mara nyingi hukosa
huduma za msingi za jamii.
Kuendelea kukua kwa miji siku hizi mara kadhaa kumekuwa ni sababu kwa
watu wanaoishi vijijini kusahauliwa. Lakini kwa hakika ni kiwango kikubwa cha
umaskini katika maeneo ya vijijini kilichochangia kiasi kikubwa kwa watu kuhama
kutoka vijijini kwenda mijini.
Tukichunguza
Utawala unaweza kuitwa mzuri iwapo matarajio ya binadamu
yanashughulikiwa kuelekea kwenye ushiriki wenye ubunifu katika serikali na
katika jamii. Katika mazingira ya jumuiya ya kimataifa, utawala bora huhitaji
kwamba mataifa yote yakiwemo masikini na madogo
Itaendelea toleo lijalo
Lijue Shirika
la Kipapa la Misioni (PMS)
l Ni muunganiko wa mashirika manne
MARA nyingi watu mbalimbali wakiwemo waamini wa Kanisa
Katoliki na wale wenye mapenzi mema, wamekuwa wakisikia ama kusoma kwenye
vyombo mbalimbali vya habari juu ya Shirika la Kipapa la Misioni (PMS). Ili
ufahamu kwa undaji juu ya Shirika hili,ungana na Leocardia Moswery,SAUT,
katika makala yake.
KATIKA kuhamasisha
na kuelimisha waamini duniani kote ili washiriki kazi na shughuli za Misioni
kwa sala, sadaka na michango ya mali na fedha, Uongozi wa Kanisa Katoliki
Duniani ulianzisha Shirika la Kipapa la Misionn (PMS).
Shirika hili linaloongozwa na Baba Mtakatifu na Maaskofu,
lina jumuisha matawi manne ambayo lengo
lake ni kuhamasisha kila Mkristo kutambua kuwa ni mmisionari, mhubiri wa Habari Njema kwa
wengine kwa kadiri ya nguvu na uwezo wake, kwa kadiri ya wito na vipaji vyake.
Mashirika hayo ni pamoja na Shirika la Uenezaji Injili (Propagation
of Faith), Shirika la Kimisionari la Utoto wa Yesu (Missionary Childhood),
Shirika la Mtakatifu Petro Mtume (St. Peter the Apostle) na
Shirika la Umoja wa Wamisionari (Missionary Union).
Shirika la
Uenezaji Injili (Propagation of Faith)
Shirika
hili lilianzishwa na msichana mmoja, Maria Paulina Jaricot.
Tangu utoto wake,Maria ambaye alizaliwa Julai 22 ,1799
katika sehemu ya Lyons, Ufaransa,
alipata mafunzo ya imani katika shule za Kanisa Katoliki.
Kabla ya kuanza kupata mafunzo hayo ya imani,Maria baada ya kumaliza shule akiwa na umri wa
miaka 14 alianza maisha ya anasa, ya kujipamba kwa mavazi kulingana na mitindo ya wakati ule.
Alikuwa na kipindi kifupi cha uchumba, baadaye alipatwa
na ugonjwa na katika mahangaiko yake hayo, mama yake akafa mnamo mwaka 1816.
Tangu wakati huo Maria
aliamua kutoa maisha yake kwa Mungu akaamua kufunga nadhiri ya usafi wa
moyo, na akanza kuvaa mavazi kama ya wafanyakazi maskini.
Pia, aliamua kwenda kufanya kazi hospitalini ili
kuwasaidia na kuuguza wagonjwa maskini waliokuwa hawajiwezi kabisa.
Kwa kuitikia mwito
wa kaka yake aitwaye Phileas, aliyekuwa Mmisionari kuhusu mahitaji na matatizo ya Wamisionari, Maria
alikusanya wasichana wafanyakazi wa viwanda vya mji wa Lyons katika jumuiya ya sala, wakajitolea kwa hali
na mali kutegemeza misioni.
Paulina alitambua wazo hilo na ghafla mwaka 1819, alipata
wazo na mwanga wa kuunda vikundi vya watu kumi, ambao watakuwa 100 na baadaye
1000 na kila kikundi na kiongozi wake.
Kila mwanachama atakuwa na wajibu wa kusali kila siku na
kutoa mchango wa kila juma kwa misioni.
Shirika la Paris la Wamisioni lilipokea wazo la Paulina
na yeye alipatwa na matatizo na upinzani mwingi na akaamua kujitenga na hata
shirika lilipoanzaishwa rasmi Mei 3, 1822, jina lake halikutajwa.
Paulina hakukata tamaa alianzisha vikundi vya sala na vya
kitume ambavyo ni pamoja na LORETO (Shirika la Watawa kwa Misioni),
Maisha ya Rozari kwa kuombea Misioni, na hata Maktaba kwa Walei ili wafahamu
habari za Kanisa na za Misioni.
Vile vile, alinzisha hata
benki kwa ajili ya wafanyakazi wa Lyons. Lakini juhudi zake hazikuleta
mafanikio kwa vile benki ilifilisika na
Paulina alipoteza mali zake zote, akawa maskini na 1862 akiwa na umri (63)
alikufa.
Zipo hatua za kumtaja Mtakatifu kwani hatua ya kumtaja
‘Mwenyeheri’ imekamilika.
Shirika la Kimisionari la Utoto wa
Yesu (Missionary Childhood)
Shirika hili ambalo lengo lake kuu ni kufundisha watoto
imani, kulinda na kutetea haki za watoto na kutoa misaada kwa watoto
wanaoteseka, lilianzishwa Mei 9, 1843 na Askofu Charles de Forbin Janson,
ambaye alipata elimu safi ya Kanisa
Katoliki.
Baada
ya kumaliza masomo yake, Charles ambaye alizaliwa Novemba 3, 1785, nchini Ufaransa katika
familia tajiri, alipewa kazi na Serikali ya Ufaransa kujifunza kuwa Balozi
katika nchi yake.
Macho
yake yaliona mateso ya Kanisa la Ufaransa ambapo makanisa pamoja na nyumba za Watawa
ziligeuzwa kuwa mapokeo ya kale na watoto wengi walikuwa hawajui tena imani ya dini
Baada
ya kuona hivyo, alimua kuwa Padre na kumtaka dereva wake ampeleke katika
Seminari ya Mtakatifu Sulpice kitu ambacho
kiliwashangaza watu wote.
Wakati
huo alikuwa na umri wa miaka 23.
Wakati
akiwa Seminari, Charles alipenda kujifunza habari za misioni na akaanza
kuwafikiria mamilioni ya watoto duniani ambao
hawakuwa na mtu wa kuwafundisha habari za Mungu.
Akiwa
na umri wa miaka 38, Charles aliteuliwa kuwa Askofu wa Jimbo la
Askofu
Charles alitoka
Mwaka
1839, wimbi la watu wenye kuwachukia maklero likavamia nchini kote Ufaransa.
Askofu
Charles akafukuzwa kutoka jimboni kwake na kukimbilia mafichoni. Akiwa
mafichoni aliweza kutembelea eneo la Amerika na
Aliporundi
Ufaransa, Askofu Charles, alifanikiwa kukutana na Paulina Maria Jaricot Mwanzilishi wa Shirika la Uenezaji Injili
Duniani.
Kukutana
kwake na Paulina, kulimfanya Askofu Charles aone umuhimu wa kuhamasisha watoto
wa Urafansa ili wasaidie kazi za Misioni kwa sala zao na kwa michango
Askofu
Charles alitambua kuwa, hayupo tena mwenyewe katika kufikisha Injili kwa
watoto, bali yupo pamoja na jeshi kubwa la watoto wamisionari.
Shirika
hili la Kimisionari la Utoto wa Yesu linafanya kazi zake duniani kote kupitia
kwa Maaskofu, mapadre, watawa, wamisionari wakiwasaidia watoto wanao
teseka, maskini, wasio na makazi, wagonjwa, waliotupwa ili
watoto wote wajisikie wanapendwa na Mungu.
Shirika la Mtakatifu Petro Mtume (St.
Peter the Apoltle) Hili ni Shirika linalojishughulisha na elimu ya
waseminaristi, manovisi, mapadre na watawa ambalo mara nyingi huboresha elimu
na malezi
Mwanzilishi
wa Shirika hili ni binti mmoja wa Kifaransa, Jean Bigard aliyezaliwa Desemba 2,
1859.
Akiwa
na umri wa miaka 19, alimua kuacha anasa za kidunia na ubatili wake na kujitoa
kikamilifu kwa kazi ya Mungu. Jean na
Mama yake Stephanie walianza kuchangia mfuko wa kuwasaidia mapadre wazalendo wa
nchi za misioni kwa ajili ya masomo na mahitaji
Waliomba
misaada kutoka nyumba hadi nyumba, wakaomba na sala zao wakaandika maandishi
kuelezea uhitaji mkubwa wa seminari katika nchi
Pia,
Jean alitoa urithi wake kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa jipya Ujapani lililopewa
jina la Mtakatifu Fransis Xavieri.
Ijapokuwa
kazi ya Jean ilithaminiwa na Maaskofu wa nchi za Misioni, Maaskofu wa nchi ya
Ufaransa hawakupenda kusaidia.
Ni
baada ya miaka mingi ya mapambano, ndipo Maaskofu wa Ufaransa walipokea Shirika
lake la Mtakatifu Petro Mtume (mwaka
1886).
Mpaka
mwaka 1903 alipofariki mama yake Jeann Mama Stephinie Bigard, tayari walikuwa
wamekusanya kiasi kikubwa cha fedha kwa kuwaelimisha mapadre wa misioni.
Baada
ya kifo cha Stephinie, Jean alishindwa kuendeleza shirika na akaamua
kulikabidhi kwa wamisionari Wafransiskani.
Baada
ya hapo, Jeann alijiunga na nyumba ya watawa.
Shirika la Umoja wa Wamisionari (Missionary
Shirika hili
ambalo kibali chake kilitolewa na Baba Mtakatifu Benedikti wa 15, lina
malengo ya kuwaunganisha mapadre, watawa na walei katika kusali pamoja na ndugu
na dada zao wenye kufanya kazi za misioni.
Pia,
shirika hili ni moyo wa mashirika mengine kwa vile linachochea roho ya
umisionari na kutoa elimu ya misioni kwa mapadre, watawa, waseminaristi,
manovisi na walei ambao wanahusika katika kuhamasisha na kupandikiza roho ya
umisionari katika Taifa la Mungu.
UCHAMBUZI WA KITABU
Tamthilia na Ulimwengu Ulivyo Sasa (2)
Kitabu: MORANI.
Mwandishi: Emmanuel Mbogo.
Mhakiki:
Projest
M. Christopher
Inatoka Toleo lililopita
Nungu
na Mlemeta ambao tayari tumekwisha elezwa kuwa ni kupe na mkia wa ng’ombe na
kazi ya kupe ni kunyonya kile asichopanda ili mradi yeye ashibishe tumbo lake.
Watu hawa wanawapa watu wakati na hali ngumu.
Pesa ndogo wanayoipata haifai kitu kwani bidhaa
zote ni bei mbaya. Huu wala sio utani
hata kidogo, uhalisi upo katika jamii zetu na ndio maana Mwandishi suala hili
likamshughulisha ipasavyo. Tumeshuhudia
Serikali ina nia njema, lakini ifikirie ni
mamilioni mangapi yatakayotolewa kugharamia vyombo hivyo huku wakulima wakilia
na bei ndogo ya kahawa kwa shilingi 40/- kwa kilo na wakati uti wa mgongo wa
taifa ni kilimo.
Kila siku wimbi la ujambazi linaongezeka hata
mpaka vyombo vya dola vimeshukiwa kufanya hujuma hizo, sababu kubwa ni utawala
usio mbadala: mazao hayana soko, ajira hamna, bidhaa bei ghali, kodi inadaiwa,
tumbo linadai unategemea mtu atafanya nini? Wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia
ya Kongo ni matajiri kwa
Rushwa:
Pamoja
na kufanya magendo kunyonya jasho la wenzao na kuhujumu uchumi, bado rushwa
imekithiri na kuonekana kuwa silaha ya wakubwa dhidi ya wanyonge. Mlemeta na
Yusufu wanapinga kuliweka jina la Nungu katika orodha ya wahujumu uchumi kwa
sababu wamepewa ruhusa
“Mlemeta kama wewe umenunuliwa sio mimi” (Uk.
13). Jaji anahukumu visivyo kwa
maana amepewa rushwa isingekuwa hivyo, basi Jaji yule angeweka wazi uovu wa
Nungu. Badala yake, kibao kinageukia makabwela kuwa ndio wahujumu.
Msanii anasema: “... Mhujumu uchumi mkubwa! Eti
kukutwa nyumbani kwake na tenga mbili za kisamvu na dawa tatu za kolgeti”
(Uk. 35).
Hii imetupa picha halisi kuwa ukandamizaji ni
nyenzo ya wakubwa kwa Makabwela. Hakimu hakuona walaolundika fedha ughaibuni,
wenye hoteli Marekani, wanaovusha karafuu, kahawa na tanzanite kwa magendo,
badala yake kaona wenye tenga mbili za kisamvu!
Hili ndilo tatizo linalozifanya nchi zetu
zishindwe kuendelea na kusababisha vita kwani
daima rushwa ni adui wa haki. Na haki isipokuwepo ndipo mtutu hushikwa
ili kuitafuta kwani haki haipatikani ila kwa ncha ya upanga.
Hapa
Usaliti:
Dhana
hii pia ni kikwazo cha maendeleo. Mlemeta na Yusufu walipewa kazi ya kuwa
Wanakamati, Kamati ya kubaini wahujumu uchumi, wanamsaliti Jalia na jamii kwa
jumla uliyowapa shughuli hii kwa kuwaamini.
Mlemeta anamtamkia waziwazi Dongo kuwa:
“Unaweza kumkamata Mzee, lakini mimi sikubaliani na wewe” (UK.12). Pia,
usaliti ni ule wa Nungu kwa Aisha. Nungu alistarehe na Aisha mpaka usiku wa
manane pale Night Club Bar huku akijua dhahiri kuwa ni mwanafunzi
na bado yu mikononi mwa wazazi.
Kukosa kwake siku nyingi shuleni kunamfanya
afukuzwe shuleni na pia nyumbani. Anapokuja nyumbani kwa Nungu na kumweleza
hayo, Nungu anasema: “Kakufukuzia kwangu ?… Mpumbavu mkubwa…!” (Uk. 26).
Sakata hili haliishii hapo, hatimaye
wanaachana: “Vipi mzungu wako? Alinishagaza na mie nikamshiti” (Uk.32). Chanzo
cha kufukuzwa kwa Aisha ni Nungunungu, lakini anakataa kupokea matokeo ya
starehe
“Indiketa” kwa wanafunzi na vigogo naziwasha!
Enyi wanafunzi nani kawafundisha tabia hii hamwoni kuwa mnawasaliti wazazi
wenu? Enyi vigogo, viongozi na wengine waacheni wanafunzi wasome ushawishi wenu
wa fedha, lifti na madoido mengine uwe kikomo.
Ukweli ni kwamba katika jamii yetu, usaliti upo
hasa kuanzia mtu na mtu mpaka mtu na kikundi cha watu. Viongozi waliopewa
dhamana na wananchi ya kuwakilisha mawazo na matatizo ya serikalini, Unashindwa
kuwa karibu na waliokutuma, shida zinazowakabili utazijua vipi?
Ujasiri:
Pamoja
na njaa, kiu na hali mbaya ya msituni, Mzee, Malongo na Mzee Mapoto wanaendelea
na safari
Jalia mwanamke wa pekee anayetisha asiyeogopa
kitisho chochote, anakabiliana na Yusufu na Nungu pale wanapoleta matata.
“...Jalia ananikata mtama mimi!” (
Hapa sio kweli kuwa uhalisia haupo, upo ila kwa
kiasi kidogo kwani katika jamii yetu ni
wanawake wachache wawezao kuwa
Kila kazi ya fasihi ina manufaa kwa jamii
ikitegemea jinsi msanii alivyoiweka wazi na kuwafunua macho hadhira juu ya lile
linalijiri katika jamii
Mtazamo wa
Kikatoliki kuhusu namba za Biblia(2)
Inatoka Toleo lililopita
Namba saba:
Kibiblia namba hii ina maana zifuatazo:
i.Utilimilifu au Ukamilifu
ii. Jumla ya 3 jumlisha 4
iii. Utimilifu unaoongoza mtiririko wa muda:
- Wiku moja ni siku saba
Wiki moja na siku saba; Mwaka wa Jubilei ni (7X7) +
1= 50.
Maana nyingine ni Mashemasi
saba walioteuliwa ili kugawa huduma (mahitaji) ya kila siku – (Matendo 6:5);
Mwinjili Mathayo anaipendelea sana namba saba katika Injili yake; Kitabu cha
Ufunuo wa Yohane kinaitaja na kuirudia sana namba hii saba.
Namba Nane (8): Kibiblia namba hii inadokeza mambo
kadhaa ikiwa ni pamoja na Uhai au maisha mapya:
Rejea wale watu wanane waliobakia na kukombolewa kwenye safina ya
Nuhu.
Pia, inadokeza Siku ya nane
baada ya mtoto kuzaliwa ni siku ya kutahiriwa- hivyo ni uhai mpya, maisha
mapya, mwanzo mpya na pia, Daudi alikuwa ni mtoto wa nane wa Yesse.
Namba Kumi (10): Kibiblia namba hii inadokeza
mintarafu Ujazo au utimilifu tele, ukamilifu rejea vidole vyote vya mikono
miwili ya mwanadamu; Amri Kumi za Mungu; Mababu wa Israeli kabla ya ile Gharika
Kuu pamoja na Pembe kumi za yule mnyama aliyeonekana na Dani.
Namba Kumi
na Mbili (12): Kibiblia namba hii ni muhimu
Inadokeza pia kuwa,
Yerusalemu Mpya imejengwa katika misingi kumi na miwili na ina milango kumi na
miwili; Nyota kumi na mbili katika kile kilemba cha mwanamke, katika Kitabu cha
Ufunuo. Rejea Ufunuio
Namba Arobaini (40): Kibiblia namba hii ina maana
muhimu
Waisraeli waliihusisha na
kukadiria miaka 40
Pia, Nuhu alikaa katika
safina kwa siku 40; Namba hii 40 inahusishwa na kipindi cha taabu, dhiki,
majonzi, kasheshe, adhabu, simanzi, misiba, toba, mateso, shida na toba kwa
Waisraeli: Mfano, Gharika Kuu ilidumu kwa siku 40; Waisraeli walikaa na
kutangatanga jangwani kwa miaka 40; Musa alikaa mlimani Sinai kwa siku 40;
Eliya alitumia siku 40 kufikia Mlima Sinai na Watu wa Ninawi walipewa siku 40
watubu.
Mfano mwingine ni ule wa Yesu
kukaa jangwani kwa siku 40 akifunga na kusali; na Kristo Mfufuka alikaa kwa
siku 40 kabla ya kupaa mbinguni. Hivyo, zipo siku 40 kati ya Pasaka na Kupaa.
Namba Hamsini (50): Kibiblia hii ni namba
inayoelezea: Furaha: Siku 50 baada ya kuvuna mashambani ni kipindi cha
furaha, shangwe na nderemo.
Shukrani: Mwaka wa
50 yaani (7x7)+1 ni mwaka wa kutoa shukrani kwa Mungu.
Pentekoste- Siku 50
baada ya ufufuko wa Bwana Wetu Yesu Kristo- Mavuno ya Ukristo.
Namba sabini (70): Kibiblia namba hii
inadokeza:-
Utimilifu,
ujazo- usiopimika wala kufahamika na akili ya mtu wa kawaida (10x7)
kadiri ya Wayahudi.
Ukamilifu: Waana wa
Israeli wanawakilishwa mbele ya Mungu na Wazee 70. Pia, Kadiri ya Biblia, dunia
ilikuwa na watu 70 wengi ajabu- kadiri ya utambuzi wa kiwango cha hesabu za
Kiyahudi.
Pia, Wana wa Yakobo (Israeli)
walioingia Misri walikuwa 70; Miaka 70 inachukuliwa na Mwandishi wa Zaburi kama
muda tosha na mrefu wa binadamu kuishi hapa duniani na Yesu anawataka wafuasi
wake wasamehe 7x70 yaani bila mwisho bila kikomo:
Wazazi kulea leo,ni kulelewa kesho
l Watoto
wasipozingatiwa, hatma ya
l
Askofu Mkuu:
Kuvunjika kwa ndoa na Umasikini, ni chanzo cha tatizo
Na John
Pinini, Tabora
“Hatupendi na tunaona uchungu sana kuwaona watoto hao wazuri wakiendelea
kusumbuka mitaani kwa kuishi maisha ya hatari katika mabehewa ya treni,
vibaraza vya maduka na sehemu zingine ambazo zinahatarisha maisha yao,
tunasikia uchungu kwa kuishi maisha hayo ndiyo sababu Shirika letu limeanzisha
kutuo hiki ili wapate msaada wa malezi,” anasema Mkurugenzi wa Kituo
cha St. Fransis de Sale (S.F.S.)
Children’s Home.
Anaongeza, “Tunawakuta wakiwa katika hali mbaya wengine
wakiwa nusu uchi, wanaombaomba na kuokota chakula katika mapipa ya takataka,
miili
S.F.S. Children’s Home ni Kituo cha kulelea watoto wa mitaani kilichopo
katika Kata ya Ipuli mjini Tabora. Kituo hiki kimefungua ukurasa mpya wa maisha
ya watoto hao baada ya kuzinduliwa rasmi na hivyo, kuwawezesha kuwa na uhakika
wa kupata huduma muhimu
Kituo hicho kilichoanzishwa kwa madhumuni ya
kuwasaidia watoto wasio na makazi maalumu mjini Tabora, kilizinduliwa rasmi mwezi Agosti mwaka huu na
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Bw. Abbas Kandoro.
Kimekuwa mfano kwa jamii hususan mji huo katika suala
ziama la kuwapenda na kuwathamini watoto wa mitaani.
Kituo hiki kimeanzishwa na Wamisionari wa Shirika la
Mtakatifu Francis wa
Lengo la Kituo
hicho ni kuwasaidia watoto wa mitaani
ili waishi kwa furaha
Alisema watoto hao pia wanahitaji malezi bora bila
ubaguzi ili waandaliwe kuwa raia wema wa baadaye watakaolitumikia vema Kanisa
na Taifa. “Hivyo, kuna haja ya kuwasaidia ili wakue na kuvitumia vipaji
walivyopewa na Mungu,” alisema.
Kuendelea kuwaacha watoto hao bila kuwasaidia ni
kuandaa tabaka la vijana watakao kuwa chanzo cha vitendo viovu
Anasema kwa sasa kituo hicho kina watoto 48 kati
Kituo kinawapa huduma hizo muhimu kwa kuamini kuwa,
watoto wakisaidiwa wataonesha na hata kuviendeleza vipaji vyao mbalimbali
vitakavyo lililetea faida Taifa, ameongeza.
Padre Kurian, Mkurugenzi wa Kituo hicho anasema kuwa,
katika kuwaandalia mazingira bora ya kielimu, kituo hicho kinatoa mafunzo ya
kusoma na kuandika kwa watoto ambao hawajui kusoma kabla ya kuwapeleka katika
shule mbalimbali za msingi.
Aidha, ameongeza kuwa kituo hicho kina mpango wa
kuwaendeleza zaidi kielimu watoto hao kwa kuwapeleka katika vyuo vya ufundi
stadi na hata kwa wale watakaobahatika kuendelea na masomo ya elimu ya juu.
Akizungumzia huduma ya afya, Mkurugenzi huyo ambaye
pia ni Padre wa Shirika la Mtakatifu Francis wa
Anasema kwa
kuwapa huduma bila ubaguzi na kwa kuzingatia upendo, wamekuwa wakipata
taarifa zaidi za watoto wanaohitaji kusaidiwa na kuwafikia.
“Idadi ya watoto hao katika mji wa Tabora imekuwa
kubwa na inayoongezeka kwa kasi kutokana na kukosekana kwa ushirikiano wa
malezi katika jamii au familia zao…Hii ndiyo inawafanya watoto watoroke
nyumbani kwao”.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kuhusu tatizo la
watoto wa mitaani katika mji wa Tabora, baadhi ya wakazi wa mji huo wamesema
kuwa umaskini, ulevi wa kupindukia, uzazi usio wa mpango na UKIMWI ni kati ya
sababu zinazochangia kuongezeka kwa watoto wa mitaani.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Bw. Abbas Kandoro, anasema
umaskini umechangia kwa kiasi kikubwa kuwepo kwa watoto wa mitaani katika mji
huo na nchini kote kwa jumla.
Amesema hali hiyo ya umaskini imesababisha watoto
wengi kukimbia familia zao na kuingia mitaani kwa lengo la kupata unafuu wa
maisha.
“Iwapo familia zitafanikiwa kuupiga vita umaskini,
tatizo la watoto wa mitaani litapungua maana sasa watatulia katika familia zao
kwani wana uhakika wa kupata mahitaji muhimu,” alisema.
Naye Mkazi wa Kata ya Gongoni mjini humo, Bw. Alfred
Mallugu, anasema ulevi wa kupindukia na uzazi usio na mpango ni kati ya sababu ambazo zinachangia katika kuwepo kwa
watoto wa mitaani mjini Tabora.
Amesema tabia ya baadhi ya wazazi ya kubobea katika
ulevi na kusahau majukumu
Hata hivyo, Padre Kurian, anasema uzoefu umeonesha
kuwa, wengi wa watoto hao wanatoka katika mikoa ya jirani ya Kigoma, Shinyanga
na
Analitaja kundi lingine kuwa ni la watoto wanotoka
katika wilaya jirani na mji huo yaani Nzega, Urambo na Sikonge.
Anasema watoto hao hukimbilia katika mji huo ambao ni
makutano ya njia ya reli kutoka katika mikoa hiyo kwa lengo la kutafuta kazi
ndogondogo, na pindi wanapokosa kazi hizo, ndipo huanza kuzurura mitaani
kujitafutia riziki.
Aidha, amesema kuwa kituo hicho kitaendelea kuelekeza
nguvu zake katika kuwasaidia watoto hao ili kuisaidia Serikali katika kupambana
na tatizo la watoto wa mitaani.
“Serikali pekee haiwezi kumaliza tatizo
Anaongeza kuwa, endapo jamii nzima itaelewa umuhimu wa
kuwasaidia watoto wa mitaani, itakuwa rahisi kupunguza kasi ya ongezeko la
watoto hao nchini kwani wao wanawakuta katika mazingira magumu na ya
kusikitisha.
Naye Mbunge wa Viti Maalumu Vijana, Aziza Sleyum Ally,
anasema kuibuka kwa maambukizo na vifo vya watu kutokana na ugonjwa wa UKIMWI,
kumesababisha familia nyingi kukosa viongozi na hali hiyo kusababisha
wanafamilia kusambaratika.
“Hali ni mbaya zaidi kwa familia ambao zimeondokewa
wazazi wote wawili na kuacha watoto wadogo bila mtu wa kuwaongoza. Matokeo yake
watoto hao wanajiingiza katika biashara na hatima yake kuishia kuwa watoto wa
mitaani,”anasema.
Naye Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la
Tabora Mhashamu Mario Abdallah Mgulunde, anadokeza kuwa kuvunjika kwa maadili
na ndoa katika jamii ni moja ya sababu zinazosababisha kuwa na watoto wa
mitaani, ambao kutokana na kukosekana kwa malezi ya wazazi au walezi wao,
wanajikuta wakiishi katika maisha yasiyo na msaada na kukata shauri kuingia
mitaani.
Amesema udhaifu wa baadhi kushindwa kuishi maadili ya
dini au jamii, unawakosesha dira ya kuwaongoza katika maisha
Mmoja wa watoto wanaoishi katika kituo hicho, Toyi
Musa (5), anaamini kuwa kufiwa na wazazi kunachangia watoto kwenda kuishi
mitaani kutokana na kukosekana kwa malezi ya dhati kutoka kwa jamaa inayorithi
dhamana hiyo.
Mtoto huyo ambaye awali alikuwa akiishi na wazazi wake
katika kijiji cha Kazulamimba mkoani Kigoma, anasema kuwa
Mtoto huyo amesema kuwa walilazimika kuondoka kwao
baada ya kufiwa na wazazi wao na hivyo, kukosa mtu wa kuwatunza na kukimbilia
mjini Tabora kwa lengo la kutafuta kazi.
“Tulikuwa tunaishi na wazazi wetu, lakini baada ya wao
kufariki tulikosa mtu wa kututunza, tukaamua kupanda treni tukaja Tabora
kutafuta kazi tuliambiwa huku kuna kazi”, ndivyo anavyoelezea mtoto huyo.
Kila mmoja katika jamii kwa kutumia upendo wa kimungu
ulipo ndani yake, awasaidie watoto hawa ili wamjue Mungu na kuishi maisha mema
kiadilifu.
Mwisho ulitolewa mwito kwa jamii nzima kutoa
kipaumbele katika suala zima la malezi kwa watoto, hasa wale waliopoteza wazazi
wao; kwani wao wanahitaji kupewa matumaini na upendo zaidi.
ECAWIDNET: Mtandao unamkomboa mwanamke asinyanyaswe
VIKUNDI
mbalimbali duniani vikiwemo vya Kitaifa
na Kimataifa, vimepiga hatua katika suala zima la kumkomboa mwanamke. Moja ya
vikundi hivi ni Mtandao wa Maendeleo ya Akinamama chini ya Kanisa Katoliki
katika nchi za Afrika Mashariki na Kati (ECAWIDNET). Katika Makala haya, Mwandishi
Dalphina Rubyema anaeleza zaidi.
HIVI sasa mataifa mbalimbali duniani
yanaoonekana sasa kuithamini kazi kubwa inayofanywa na mwanamke tofauti na siku
za nyuma ambapo mwanamke alionekana hana manufaa yoyote mbele ya jamii mbali na
kuwa
Enzi hizo, mwanamke
alichukuliwa
Hata miongoni mwao, baadhi ya
wanawake hawakuwa na chaguo lolote katika kumpata mume, mbali na chaguzi na
maamuzi yaliyofanywa na wazazi wao.
Kazi za mwanamke hazikuishia hapo, bali pia
wanawake walitumika
Ni dhahiri kuwa licha ya kazi
kubwa waliyoifanya ikiwa ni pamoja na maandalizi ya mwanzo hadi mwisho ya
shamba, bado baada ya mavuno kuuzwa na pesa kupatikana, ni baba pekee aliyekuwa
ndiye maamuzi mkuu na wa mwisho juu ya matumizi ya pesa hiyo.
Wanawake hawakushirikishwa
kabisa katika masuala ya elimu na
Lakini, kadri siku zilivyozidi
kuendelea, ndivyo mashirika mbalimbali duniani yalivyoona umuhimu wa kumkomboa
mwanamke.
Katika kuhakikisha mwanamke
anapata elimu, Serikali ilianza kutoa nafasi za upendeleo katika shule na vyuo
mbalimbali vikiwemo vile vya Elimu ya Juu.
Serikali ya
Hadi sasa wanawake wanapewa
nafasi za uongozi na kuna wanawake wengi wenye nyadhifa mbalimbali za uongozi
ikiwa ni pamoja na uwaziri, ubunge wa kuchagulia na hata wapo wabunge wa viti
maalumu na viongozi katika nyanja mbalimbali.
Aidha, wanawake nao kwa upande
wao hawapo nyuma katika kutetea maslahi
Vikundi hivi vimeanzia ngazi
ya shina hadi ngazi ya kimataifa.
Moja ya vikundi vyenye hadhi
hii ya kimataifa ni Mtandano wa Maendeleo ya Akinamama katika Afrika Mashariki
na Kati (ECAWIDNET).
Mtandao huu ulioanzishwa mwaka
1993, unavijumuisha Vitengo vinavyohusika na masuala ya Maendeleo ya Akinamama
katika nchi za Umoja na Ushirikiano katika Mabaraza ya Maaskofu Katoliki katika
nchi za Mashariki mwa Afrika (AMECEA).
Madhumuni ya kuanzishwa kwa
Mtandao huu unaozihusisha nchi za
Waratibu wa Vitengo vya
Maendeleo ya Wanawake katika nchi husika, ni wahusika wakuu katika mpango huu.
Tangu mtandao huu uanzishwe
mambo mbalimbali yamekwisha fanyika. Miongoni mwa mambo hayo ni warsha za
mafunzo, wanachama wa mtandao huo kubadilisha vifaa vya kufundishia, kuweka
bayana mipango mbalimbali ya kuendeleza Mtandao pamoja na uandaaji wa vitabu
mbalimbali vilivyobeba ujumbe wa kumkomboa mwanamke.
Miongoni mwa vitabu hivyo,
ni Unyanyasaji Dhidi ya Wanawake
cha mwaka 1996 na kitabu cha Wanawake na Usawa cha mwaka 2001.
Mikakati ya Mtandao huo
Vile vile, Mtandao huo
unalenga kuhakikisha unalinda na kuendeleza haki za mwanamke pamoja na
kumkomboa mwanamke kiuchumi ambapo suala zima la uanzishaji wa vikundi vya
kuweka na kukopa, linahamasishwa.
Vile vile, ECAWIDNET inaweka
nguvu zaidi katika suala zima la kupinga unyanyasaji wa mwanamke likiwemo suala
la kutahiriwa na kurithiwa.
Katika kuhakisha Mtandao huu
unafanya kazi yake
Mwaka huu, mkutano huo
umefanyika Septemba Mosi hadi 14, nchini
Mratibu wa ECAWIDNET, Bibi
Oliva Kinabo, anasema pamoja na mambo mengine, mkutano huo ulilenga kuangalia
“Mafundisho ya Kanisa Katoliki kwa Jamii”.
Anasema katika mkutano huo
liliangaliwa suala zima la nafasi ya mwanamke katika mafundisho ya Kanisa kwa
jamii.
Anasema
Anasema pamoja na mambo
mengine, wajumbe wa mkutano huo pia walitembelea vikundi mbalimbali vya akina
mama nchini
Anavitaja vikundi vilivyotembelewa kuwa ni Mt.siliza
kilichopo kwenye Jimbo Katoliki la
Bibi Kinabo anasema kikundi
hiki ambacho kipo chini ya usimamizi wa Kanisa Katoliki Jimbo la
“Wanakikundi wanafundishwa
jinsi ya kuendesha miradi midogo midogo likiwemo suala la kazi za mikono,”
anasema Bibi Kinabo.
Aidha, washiriki hao
walitembelea kikundi cha MAU ambacho kinahusika na masuala ya uzazi wa mpango
kwa njia ya asili.
Anasema katika mkutano huo wa
siku 12, maamzi na mapendekezo ya washiriki yalikuwa ni kupinga kwa kauli moja
suala la kuendelea kuwanyanyasa wanawake na watoto likiwemo suala la
usafirishaji wa makundi haya kwa lengo la unyanyasaji.
“Unajua kuna baadhi ya watu
ambao wanatoa wanawake na watoto sehemu moja kwa ahadi za kuwapatia kazi
inayofaa, lakini wakisha wafikisha wanakotakiwa, hufanyishwa kazi zinazodhalilisha
utu wao,” alisema.
Vile vile washiriki hao
walitoka na msimamo kuwa, watu wa jinsia zote bila kujali rangi, wala umri wana haki sawa mbele ya macho ya Mungu, hivyo
katika kupambana na suala zima la UKIMWI kila mmoja anatakiwa awe na maamuzi
juu ya mwili wake.
Hata hivyo, Mratibu huyo wa
ECAWIDNET anasema kuwa baadhi ya nchi zilizopo kwenye Mtandao huo, hazishiriki
mikutano katika muda unaotakiwa kulingana na hali ya kisiasa katika nchi zao.
Mfano mzuri ni nchi ya
Vile vile anasema kuwa
miongoni mwa nchi wanachama wa mtandao huo, hazina uhusiano mzuri hali
inayofanya nchi hizo zisiwe wenyeji wa mkutano.
“Mfano
Mkutano huo uliofanyika nchini
Neokatukumenato si Dhehebu,
wala Ulokole ndani ya Ukatoliki
Historia
ya Kanisa imeingia sasa katika milenia ya tatu ambapo Kanisa limeendelea
kuwapo, kumshuhudia Kristu na kuwasaidia watu kukomaa katika ujuzi na imani kwa
Mungu.
Njia
mbalimbali zimejitokeza ndani ya Kanisa ili kulifanya Kanisa kuendelea kutimiza
azma yake ndani ya nyakati zinazobadilika, bila kubadilika kwa mafundisho ya
Kristu.Neokatukumenato ni moja ya njia hizo ambazo sasa Kanisa linazifanyia
uchunguzi ili kuuona mchango wake katika kuitamadunisha tunu hii ya Imani.
Katika makala hii Padre SIFFREDUS
RWECHUNGURA wa Parokia ya
Njia ya Neokatekumenato ni nini?
Tunaweza kuieleza Njia ya Neokatekumenato kwa njia mbili; kwanza
kutokana na neno lenyewe; pili kutokana na utume wake.
Neno Neokatekumenato linaonekana
'Neo' ni neno la kilatini maana yake ‘mpya’. Katekumenato
ni malezi au kipindi cha ukatekumeni. Mkatekumeni ni yule ambaye anaandaliwa kwa ajili ya ubatizo. Kwa hiyo
tunaweza kusema Neokatekumenato ni katekumenato mpya ; ikiwa na maana
kwamba siyo tu inajumuisha wale wanaojiandaa kubatizwa bali ni zaidi ya hao
kama tutakavyoona hapo mbele tutakapoelezea utume wake.
Kwa upande mwingine tunaweza kuielezea njia ya
Neokatekumenato kufuatana na maneno ya Baba Mtakatifu Yohana Paulo wa pili
aliyoyasema katika waraka wake ‘Ogniqualvota’ wa Agosti 30, 1990 : ‘
Naitambua Njia ya Neokatekumenato kama utaratibu endelevu wa malezi ya
kikatoliki yaliyomuafaka kwa jamii yetu na kwa nyakati zetu’.
Kimsingi Njia ya Neokatekumenato nia yake au utume wake
ni kumsaidia Askofu wa Kanisa mahalia kama njia mojawapo ya utekelezaji kijimbo
wa kazi za uingizaji katika Ukristu na elimu endelevu katika imani kwa wahusika
kama wanavyoagizwa na Mababa wa Mtaguso wa pili wa Vatikano na Magisteria ya
Kanisa.
Kwa maana hiyo, Njia ya Neokatekumenato inaweza kuelezwa
kuwa ni makusanyiko wa shughuli zifuatazo :
- Neokatekumenato
au katekumenato baada ya ubatizo ;
- Elimu au
malezi endelevu katika imani
- Katekumenato
kwa wale ambao bado hawajabatizwa ;
Sasa tuangalie kiundani zaidi shughuli hizi za Njia ya
Neokatekumenato.
I. Neokatekumenato au katekumenato baada ya ubatizo
Walengwa
Kama nilivyosema awali, njia ya Neokatekumenato ni nyenzo iliyo chini ya
Askofu mahalia kuwasaidia waliobatizwa kuishi kwa ukamilifu ahadi zao za
ubatizo. Kwa maana hiyo wafuatao waweza kufaidika na chombo hiki:
- Waliolegea
katika imani;
- Ambao
hawakuinjilishwa au kupata katekesi vya kutosha
- Wanaotaka
kukua na kukomaa katika imani.
- Wanaotoka
katika madhehebu mengine ambayo hayako katika ushirika kamili na Kanisa Katoliki.
Hii
inawajumuisha hata mapadre na watawa ambao wanataka kuishi kwa ukamilifu ahadi
zao za ubatizo kwa njia ya Neokatekumenato. Katika kufanya hivyo huweza
vilevile kutoa huduma mbalimbali kwa wahusika kufuatana na wito au nafasi zao,
mfano kuongoza ibada mbalimbali n.k
Jumuiya za Neokatekumenato
Neokatekumenato huendeshwa
parokiani katika jumuiya ndogondogo zinazoitwa ‘jumuiya za Neokatekumenato’
chini ya uangalizi na malezi ya paroko wa parokia husika pamoja na wasaidizi
wake.
Utaratibu wa kujiunga na jumuiya za Neokatekumenato
Jumuiya za Neokatekumenato huanzishwa parokiani kwa mwaliko wa Paroko.
Makatekista ambao ni waamini ambao tayari wamo katika
jumuiya za Neokatekumenato huja kwenye parokia husika na kuwaalika waamini kuja
kusikiliza katekesi. Halafu kufanya ‘katekesi za mwanzo’ ambazo huendeshwa kwa
kipindi cha miezi miwili. Katika kipindi hiki cha miezi miwili katekesi hizi hufanyika mara mbili kwa juma kwa muda
wa saa moja kila mkutano. Kipindi hiki cha katekesi za mwanzo humalizika kwa
mkutano na kuishi pamoja wa siku tatu ambao hufanyika kwenye nyumba mbalimbali za mafungo. Katika mkutano huo
huzaliwa jumuiya ambayo huanza kutembea chini ya miguu au misingi mitatu ambayo
ni muhimu kwa maisha ya Kikristu kama walivyosisitiza Mababa wa Mtaguso wa pili
wa Vatikano: yaani Neno la Mungu, Liturujia (Ekaristi) na Jumuiya.
Neno la Mungu, Liturujia (Ekaristi na
Jumuiya)
Kwa kuadhimisha ibada ya Neno la Mungu mara moja kila
juma, ambamo wahusika hushiriki kikamilifu kwa kuandaa, halafu kutoa mwangwi-
yaani mang’amuzi baada ya kuoanisha Neno la Mungu na maisha halisi ya mhusika-
polepole wahusika hutambua hali ya mapungufu, hali ya dhambi, lakini vilevile
hugundua huruma na upendo wa Mungu alio nao kwa mdhambi. Kwa njia hiyo mhusika
huweza kuanza safari ya wongofu (toba) akisaidiwa na neema kutokana na
sakramenti za Kanisa hasa Sakramenti ya Upatanisho na Ekaristi. Polepole huanza
kuonja uhuru halisi (uhuru waw ana wa Mungu) na kuanza kugundua na kuishi ahadi
zake za ubatizo ambazo huwa dhahiri katika jumuiya na jamii kwa ujumla.
II. Elimu
au malezi endelevu katika imani
Kugundua na kuishi ahadi zako za ubatizo sio kazi ya siku
moja, ndio maana tunahitaji malezi endelevu katika imani. Malezi yanayotumiwa
na njia ya Neokatekumenato si mengine bali ni kuendelea kuazimisha Neno la
Mungu kila juma na kuadhimisha Ekaristi.
Ibada hizi hufanyika katika jumuiya ndogo ndogo za
Neokatekumanato ambamo mhusika akisaidiwa kwa Neno na Ekaristi, vile vile husaidiwa na wanajumuiya wenzake kwa kumuita
kwa wongofu hasa anapotambua kwamba anashindwa kwa namna moja au nyingine kuwapenda
wengine katika jumuiya.
Kwa njia hiyo wanajumuiya huwa kioo au nyenzo wao kwa wao
kujitambulisha hali zao za mapungufu na kwa njia hiyo kukimbilia msaada wa
neema ya Mungu kwa njia mbalimbali. Pole pole ishara za ‘umoja na upendo’
huanza kuwa dhahiri katika jumuiya, ishara ambazo kristu alisema zitawafanya watu watambue kuwa sisi ni wafuasi
wake na kwamba alitumwa na Mungu (Taz. Yoh. 13,34-35 na Yoh 17, 21-23).
III
Katekumenato kwa wale ambao hawajabatizwa
Njia ya Neokatekumenato vilevile ni chombo cha kumsaidia Askofu kwa
uingizaji katika ukristu kwa wasiobatizwa. Wahuska hushiriki katika ‘katekesi
za Mwanzo, na baadaye huendelea kushiriki Neno la Mungu katika jumuiya .
Wakatekumeni hutumia mafundisho kutoka mababa wa Kanisa, hati mbalimbali za
Mtaguso wa pili wa Vatikano na Magisteria, Katekisimu ya Kanisa Katoliki na
mafundisho kutoka waandishi wa masuala ya kiroho waliokubaliwa na Kanisa.
Huendelea na mafundisho hayo mpaka Kanisa linapowaona wako tayari kupokea
ubatizo.
Itaendelea toleo lijalo