Kijue Kilimo cha Kujinusuru
Maingilio:
Katika toleo lililopita tuliona kuwa kilimo cha kujinusuru ni rahisi kukimudu
kinakubalika katika jamii ni rahisi kutekeleza na kueneza kwa sababu jirani
anaweza kuona afanyalo mwenzake. Sasa endelea.
Njia za kudhibiti mmomonyoko wa udongo
Udongo wa juu wa ardhi wa kawaida huondolewa na maji
au upepo kwa ajili ya mmomonyoko wa ardhi ya juu ambayo ina rutuba nyingi ya
kuifanya mimea iweze kustawi vizuri na hatimaye kutoa mavuno mengi na bora.
Tunajua kuwa udongo ulio chini ya tabaka la juu hauna rutuba ya kutosha ya
kuwezesha mazao kustawi vizuri. Kutoweka kwa udongo wa juu toka shambani au
bustani kwa njia ya mmomonyoko ni hasara kubwa
Njia
za kuhifadhi ardhi zinaweza kutumiwa kwa kutegemea hali ya hewa, mazingira ya
eneo
Ziko
njia kuu mbili za kuhifadhi ardhi. Njia za asili au za kienyeji na njia ya
kisasa ambazo zimefanyiwa utafiti yakinifu na wataalamu.
Njia za asili
Huko Mbinga wenyeji wake walilazimika kubuni kilimo
cha ‘ngoro’ au ‘Ingoro’. Sehemu kubwa na wilaya hiyo ina miteremko mikali.
Wataalamu wakongwe
Ngoro hulimwa kwa kuchimba vishimo katika miteremko na
kupanda mazao
Nyasi zilizofunikwa hugeuka kuwa mboji na polepole
udongo wenye rutuba huongezeka. Maji ya mvua
yakisimama katika vishimo hivyo vidogo vidogo na hivi kulinda
unyenyekevu wa ardhi na kukinga mmomonyoko wa ardhi.
Tunaelezwa
pia kuwa wahehe na Wabena ambao waliishi huko Iringa walisifika
Mtindo
huu wa ulimaji ni wa matuta ambao
hutunza maji na unyevunyevu. Zaidi ya hayo huzuia mmomonyoko wa udongo.
Itaendelea
Chozi
la Matumaini kwa Watoto walioathirika kwa UKIMWI (2)
Na Pd. Richard Mjigwa
Sehemu hii ya awamu ya kwanza ya mradi wa Kijiji cha
Matumaini, kunatarajiwa kujengwa Maabara ya kisasa kwa ajili ya uchunguzi wa
Ugonjwa wa UKIMWI na maendeleo yake.
Ama kwa hakika kituo hiki
kitasaidia kutoa habari katika mapambano dhidi ya janga la UKIMWI kwenye mikoa
iliyoko Kanda ya Kati.
Kijiji hiki cha Matumaini
kitakuwa pia na kituo cha watoto wadogo pamoja na shule ya msingi itakayokuwa
inawahudumia hata watoto majirani, ili kuweza kutoa matumaini zaidi katika tunu
ya maisha. Kijiji hiki kinapokea watoto yatima na wale walioathirika kwa Virusi
vya UKIMWI kutoka mikoa ya
Ujenzi wa Kijiji hiki cha
Matumaini ni ishara wazi ya jinsi ambavyo Mwenyezi Mungu anavyoweza kubadili
miradi ya kibinadamu, ili kukidhi mipango ya Mungu katika maisha ya mwanadamu.
Hiki ni kijiji ambacho imani na sala vinakumbatiana. Huu ni mwelekeo chanya wa
kupambana na janga la ugonjwa wa UKIMWI, kwa kuchochea matumaini kwa siku za
usoni.
Haya ni mapambano mazito yanayoyajumuisha
makundi mbali mbali katika jamii, ili kupambana kufa na kupona dhidi ya gonjwa
la UKIMWI, kwa upande wa Serikali na dini mbali mbali. Watoto ni tumaini la
mwendeleo wa Kanisa na taifa kwa ujumla. "Huu kwa hakika ni utajiri wa
jamii yoyote ile". Haya ni maneno mazito yaliyotolewa na Mhashamu Askofu Mkuu
Luigi Pezzuto, Balozi wa Vatican nchini Tanzania, wakati wa mahubiri yake. "Upendeleo
kwa watoto katika historia ya maisha ya Kanisa si jambo geni sana, kwani tayari
kuna mtu aliyetangulia kuonesha njia na huyo si mwingine bali ni Yesu Kristu
mwenyewe", alisema Askofu mkuu Pezzuto.
Awamu
ya pili ya Kijiji cha Matumaini ni kuhakikisha kwamba mpango huu unawanufaisha
watoto yatima walioathirika na UKIMWI wapatao mia nne, lakini ambao bado wanayo
nafasi ya kuishi pamoja na ndugu na jamaa katika mazingira ya mkoa wa Dodoma. Watoto
hao watahudumiwa huko huko wanakoishi kwa kupatiwa ushauri nasaha, elimu pamoja
na huduma ya matibabu.
Kwa
vile hakuna mtoto aliyejichagulia kubaki yatima, basi Kijiji cha Matumaini
kitatoa pia msaada wa kiuchumi katika kuboresha matumaini ya maisha ya watoto
hao.
Watoto
hao pia watapata nafasi ya kutumia huduma mbali mbali zinazotolewa na Kijiji
cha Matumaini kama zilivyobainishwa katika awamu ya kwanza.
Akitoa
shukrani zake za dhati kwa Shirika la Masista Waabuduo Damu Azizi ya Yesu, Mkuu
wa mkoa wa Dodoma Bw. Isidori Shirima, aliwashukuru Masista hao kwa jitihada
zote walizofanya hadi kufikia hapo na kwamba, Serikali itaendelea kushrikiana
na Kanisa katika kumhudimia mwanadamu.
Ufunguzi
wa Kijiji cha Matumaini lilikuwa ni tukio la aina yake katika kuleta matumaini
mapya kwa wale walioathirika na gonjwa la UKIMWI. Tabasamu lililosindikizwa na
mafuriko ya machozi lilionekana miongoni mwa wageni waalikwa, hasa pale watoto
hao walioathirika na UKIMWI walipokuwa wanacheza na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bw. Isidori
Shirima kana kwamba ni watoto wa familia yake. Busu la upendo lilipotolewa kwa
watoto watatu wanaofungua Kijiji hiki cha Matumaini na Mhashamu Askofu mkuu
Luigi Pezzuto na Mkuu wa Mkoa Bw. Isidori Shirima liliwaacha wengi wakiogelea
katika dimbwi la machozi ya matumaini.
Awamu
ya tatu ya Kijiji cha Matumaini ni utoaji wa Ushauri nasaa kwa wanawake
wajawazito ili kuchunguza maambukizo ya Virusi vya UKIMWI kabla ya kujifungua,
ili waweze kusaidiwa kujifungua salama na hivyo kupunguza uwezekano wa
maambukizo kwa watoto ambao hawajazaliwa.
Wanawake wajawazito wapatao ishirini na tano wataweza kuhudumiwa kwa mara
moja katika Kijiji cha Matumaini juma moja kabla ya kijifungua na juma moja
baada ya kijifungua, ili waweze kupewa mbinu mbadala katika kuwatunza watoto
wao bila kuwanyonyesha maziwa ikiwa kama wameathirika na Virusi vya UKIMWI.
Ujenzi
wa Kijiji cha Matumaini ulianza mwezi Juni mwaka jana. Hadi sasa zaidi ya dolla
za Kimarekani zipatazo laki sita zimekwisha tumika katika shughuli za ujenzi. Baadhi
ya nyumba zimekamilika na tayari zimeanza kutumika, bado ujenzi uko mbioni
kukamilisha majengo yaliyobaki.
Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa pili amekuwa ni kati ya
wafadhili wakuu wa Kijiji hiki cha Matumaini. Yeye amechangia ujenzi wa nyumba
moja ambayo tayari imeanza kutumika. Wafadhili wengine ni Kikundi cha
"AMICI delle Mission" kutoka Bagnolo Mella nchini Italia pamoja na
wafadhili wengine wa ndani na nje ya nchi ambao wanapenda chozi la matumaini
libaki katika sakafu ya mioyo yao. Watoto Hassani na Amani ndiyo sehemu kubwa
ya ufanisi katika Kijiji hiki cha Matumaini.
Ni matumaini ya
Masista Waabuduo Damu Azizi kwamba, watawapatia watoto hao matibabu, matunzo na
zaidi ya hayo pendo la kifamilia katika kipindi hiki wanaposafiri pamoja kwenye
hii hija ya matumaini.
sababu zinazo changia kushamiri kwa uchumba sugu (2)
Na Mwandishi
Wetu
Sababu ya Tatu :
Ukosefu wa kipato.Siku hizi kuna ukosefu
mkubwa wa fedha na ajira hasa miongoni mwa vijana. Hali hii inachangia
sana ‘uhalalishaji’ wa uchumba sugu eti
kwa vile uchumba sugu unapunguza gharama za mahari na harusi.
Rejea bei
ya ‘Mbuzi ya sale’ – kati ya
Wachaga
Bei ya
Ngo’mbe 40 wa mahari kati ya Wasukuma.
a) Je huu
ni ukweli ?
Huu si ukweli hata kidogo. Kwa nini ?
baadaye gharama huwa kubwa zaidi.
Gharama za
talaka, ‘utengano, uchangudoa, uchunaji mabuzi. Mayatima wa UKIMWI, watoto wa
mitaani ni kubwa kuliko zile za awali !!!.
b) Vile vile, kimaadili kama bado mmoja anayo
dhamiri safi, hai na sahihi atapaswa kulipiwa uvunjaji timamu na wa makusudi wa
sheria za Mungu na Kanuni za Kanisa.
c) Kiuchumi,
usuria na mtengano na hata talaka
utapswa kulipiwa zaidi – hata mara nne zaidi kama Zakayo alivyofanya :
Soma Luka 19 :9
d) Makabila
mengi yamepunguza sana kima cha mahari.
Sababu ya Nne :
Leo hii vijana wengi wanaoishi maisha ya
uchumba sugu wanadai ‘kila mmoja anafanya hivyo’
a) Je huu
ni ukweli ?
Hapana, si
kila mtu au kijana hapa Tanzania anaishi maisha ya uchumba sugu. Mara kwa mara
hasa kutokana na saikolojia ya vionjo vyao, vijana wengi katika urika wanaweza
‘wakaipenda’ na ‘kuushabikia’ mtindo huo wa maisha ya uchumba sugu.
b) Je si
kweli kuwa Kristo amesema bayana kuwa mlango au njia ya kwenda mbinguni ni
nyembamba ?
c) Je hatuoni umuhimu wa sheria, kanuni na miongozo
katika maisha na Kanisa hasa katika kutuongoza tupende na kutenda tu yale yaliyo mema ?
d) Fundisho kutoka katika
kielelezo cha kiafya.
Hebu tujaribu kufikiri kuwa kipo kijiji kimoja mahali fulani hapa
Hayupo. Hivyo basi, sisi kama Wakristo tunaona
faida za kuishi maisha ya Sakramenti ya ndoa, basi tufanye hivyo hata kama
inaonekana kuwa siku hizi ni wachache wanaochagua kilicho chema.
Sababu ya tano
Vijana
wengi wanaamini kuwa maisha ya uchumba sugu ndiyo njia pekee ya kumpata mwenzi
wa ‘kufaa’ kwa wakati uliopo.
Moja ya njia nzuri za kupima uwezekano wa kuishi
pamoja kama mume na mke ni kuangalia jinsi wanavyoweza kustahimili matatizo
dhidi yao.
Mara nyingi wasichana wanafikiri kuwa mapenzi
kabla ya ndoa ndio ‘mbinu’ au ‘njia’ muhimu ya kumpa mwenzi. Mwishoni wasichana
wengi hupata mimba na kuachika.
Yote haya huwaletea majuto makubwa maishani!.
Sababu ya sita:
Siku hizi vijana wengi wanadai kuwa maisha yao ya uchumba sugu hayamwumizi
mtu yeyote!
Je huu ni ukweli?
Si ukweli hata kidogo. Ni jambo lililo dhahiri
na wazi kabisa kuwa maisha ya uchumba sugu husababisha makovu mengi ya
kisaikolojia kwa familia nzima. Utafiti unaonesha kuwa wazazi wengi wa pande
zote huumia na kusononeka sana mara wanaposikia kuwa watoto wao wanaishi maisha
ya uchumba sugu.
Aidha, wengi wao hunyimwa kupokea Ekaristi
Takatifu kutokana na uamuzi wa maisha ya uchumba sugu wa watoto wao. Wazazi hao
hujuta na kukumbuka jitihada za malezi kwa watoto wao hasa walipokuwa wadogo.
Sababu ya Saba
Leo hii wanasema kuwa Kanisa sehemu nyingi
linaonekana kuwa ‘kimya’ kuhusu uchumba sugu.
Je
huu ni ukweli ?
Kimsingi
Kanisa haliko kimya. Linakemea sana hali hiyo hata hivyo, Yuda Iskariote
alimsaliti Kristo. Je hali hii ilihalalisha usaliti huo ?
Mtakatifu Paulo naye aliwaasa na kuwagombeza wale
wakristo wa Kanisa la Pergamo kutokana na tabia
yao ya uasherati (Ufunuo
2 :15).
Tabia ya uasherati inakemewa aghalabu mara 14
katika kitabu cha Ufunuo peke yake.
Rejea Ufunuo 2 :15, 20-23 ;
21 :8 ; 22 :15). Mtakatifu Paulo anatukumbusha kuwa Wayahudi 23,000 waliangamizwa kutokana
na uasherati (Rejea 1Kor 10 :8) Rej pia 1Kor 6 :9-10).
Ama kweli mapadre, wachungaji na walezi
wanaowajibu mkubwa na wa pekee kabisa wa kukemea maisha ya uasherati na uchumba sugu.
Sababu ya nane :
Wapo baadhi ya vijana wanaohalalisha uchumba
sugu kwa kile wanachodai kuwa haiwezekani kubadilika tena.
Je huu ni mwono
sahihi ?
Hapana, Mtakatifu Augustine wa Hippo alifaulu
kubadilika na kufikia hatua ya juu ya utakatifu mwishoni mwa maisha yake.
Basi vijana tuelewe kuwa kamwe
hujachelewa kuachana na upotovu, nenda
ukaungame na kufanya toba
Daima huruma ya Mungu ipo kwa wale wanaomkimbilia
na kufanya uongofu wa kweli. Tuzingatie ukweli
huu hasa katika mwaka huu wa
toba.
SATF
ilivyo jizatiti kuwasaidia watoto yatima
WATOTO yatima wanahitaji msaada kama walivyokuwa wakipata
kutoka kwa wazazi wao. Katika makala haya ya Mwandishi Joseph Kiboga anaeleza jinsi shirika liitwalo Social
Action Trust Fund (SATF), linavyobeba jukumu hilo nchini.
MTOTO
mwenye wazazi huridhika na maisha, hujiona yuko huru kwa sababu hupata mahitaji
ya msingi kama vile elimu, chakula na malazi kulingana na uwezo wa wazazi wake.
Lakini mtoto huyo huyo hukata tamaa, hujiona mpweke na mwenye kila aina ya
shida anapopoteza wazazi hao.
Mahitaji ya mtoto, awe na wazazi au asiwe nao
hayabadiliki, yanabaki ni vile vile kwani bado atahitaji kula, kujisitiri na
kupata elimu ya kumwezesha kupambana na maisha.
Kutokana na mahitaji hayo, ndio maana wengi
waliopoteza wazazi wao, huondoka nyumbani kwao kwenda mitaani kutafuta misaada
mbalimbali itakayowawezesha kukidhi mahitaji yao. Hilo ni tatizo kubwa la
kijamii katika nchi masikini kama Tanzania.
Kutokana na tatizo hilo kuongezeka siku hadi siku,
mashirika kadhaa yasiyokuwa ya kiserikali, yameanza kujitolea kusaidia watoto
wa namna hiyo katika harakati zake za kuondokana na tatizo hilo.
Moja ya mashirika hayo ni lile liitwalo 'Social Action Trust Fund'
(SATF), ambalo limetumia mamilioni ya pesa kuhakikisha watoto hao wanapata
elimu.
Mkurugenzi wa shirika hilo, Bw. Valentin Rweyemamu, anasema tatizo la
watoto yatima ni kubwa licha ya jitihada zinazofanywa na shirika lake.
Anakiri kuwa shirika lake kusaidia
idadi ndogo ya watoto ikilinganishwa na wale wanaohitaji msaada.
Bw.Rweyemamu anasema idadi ya
watoto yatima nchini haipungui milioni moja, hivyo kufanya msaada unaotolewa na
SATF kutokidhi mahitaji halisi.
Kwa kutumia msaada kutoka shirika
la Misaada la Serikali ya Marekani
(USAID), limewezesha watoto yatima kupata misaada mbalimbali ikiwa ni pamoja na
kupatiwa elimu.
Anasema tangu SATF ianze kuwasaidia yatima, watoto wameweza kusoma bila
matatizo japo hawana wazazi.
Kuanzia Aprili mwaka 1998 shirika
lilipoanzishwa, Bw. Rweyemamu anasema bodi ya wadhamini iliidhinisha sh. milioni 600 ili zitumike
kuwasaidia watoto yatima.
Mwaka juzi anasema shirika
liliwezesha watoto yatima 10,621 kupata
elimu katika shule mbalimbali katika mikoa 12 Tanzania Bara.
Idadi hiyo ni sawa na ongezeko la asilimia 263, ikilinganishwa na watoto
3,717, waliosaidiwa mwaka 1999.
Mikoa iliyonufaika ni Pwani, Dar
es Salaam, Iringa, Kagera, Kilimanjaro, Lindi, Mbeya na Morogoro. Mingine ni
Mwanza, Ruvuma, Tabora na Tanga.
Mwaka jana Bw. Rweyemamu anasema
shirika lilitenga milioni.300 kuwahudumia watoto hao wakiwemo wa shule za
sekondari ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 50 tofauti na mwaka juzi ambapo
sh. milioni 200 zilitumika.
Msaada wa mwaka jana ulisaidia
mikoa 14, mikoa miwili ikiwa ni mipya kuingizwa kwenye mpango huo, mikoa
hiyo ni Kigoma na Mtwara.
Akieleza sababu ya ongezeko hilo, Bw. Rweyemamu anasema limechangiwa na ongezeko la msaada
wa pesa kutoka sh. milioni 100, mwaka
1999 hadi kufikia sh. milioni 200 Mwaka juzi.
Sababu nyingine anasema ni kule kuweka viwango vya matumizi kwa kila
mtoto, ambavyo mashirika yasiyo ya kiserikali (NGO’s) ambazo wanashirikiana
nazo zilipashwa kuzingatia.
Anasema viwango hivyo viliwekwa baada ya kubaini kuwa NGOs, nyingine
zilisaidia idadi ndogo ya watoto mwaka 1999, na kujikuta zikitumia pesa nyingi kwa kila mtoto.
Ili kuhakikisha pesa zinawafikia walengwa,Bw. Rweyemamu anasema mashirika yanayohusika yanatakiwa kupeleka
picha za watoto wanaosaidiwa, majina yao, shule wanazosoma, sahihi za wakuu wa
shule na wahusika wengine.
“Misaada yetu inasaidia watoto wetu kupata elimu, tunawalipia karo,
vitabu, sare za shule, usafiri na gharama nyingine,” anasema, Bw.Rweyemamu.
Anasema kwa kuanzia SATF inatoa
misaada kwa watoto yatima wa shule za msingi ili watoto hao, walau waweze kujua
kusoma na kuandika.
Anasema wanafunzi walioanza nao shule za msingi kwa kuwagharamia, mwaka
huu, wameanza kuwapeleka sekondari.
“Baadhi ya watoto wetu tuliowasomesha wameweza kufaulu mitihani ya
darasa la saba,” anasema na kuongeza:
“Baadaye watakaoshinda vizuri kwenda Chuo Kikuu tutawasaidia kuwapeleka
huko”.
Kuhusu msaada unaotolewa katika mkoa wa Pwani, Bw.Rweyemamu anasema
shirika lake linashirikiana na Chama cha Afya ya Msingi kwa wanaoishi na Virusi
vya UKIMWI (SHDHEPHA) kuwahudumia watoto hao.
Anasema mwaka jana, SATF ilikabidhi kwa SHDHEPHA, sh. milioni 10, hivyo
kuweza kusomesha watoto 973.
Kwa mwaka huu, SATF imetoa sh.milioni 15, na kuwa msaada huo utaweza
kuwasaidia walengwa wengi zaidi.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Bw
Nicodemus Banduka anasema msaada unaotolewa na SATF katika mkoa huo umeweza
kuwasaidia watoto wengi walengwa.
Anasema kasi ya ugonjwa huo, ni kubwa hivyo kufanya idadi ya watoto
yatima kuongezeka mara kwa mara.
Bw. Banduka anasema 1998, mkoa huo ulikuwa na wagonjwa 420;
1999 waathirika 1056 na mwaka jana wagonjwa 5,405.
Hata hivyo anasema idadi hiyo inaweza kuwa mara tano kwani takwimu
zilizopo kwa sasa zinakanganya.
“Mkoa wetu unaweza kuwa wa tatu kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa,
ingawa takwimu za zamani zinasema mkoa ni wa sita kitaifa,” anasema,
Bw.Banduka.
Akieleza sababu ya kuongezeka kwa ugonjwa huo, Bw. Banduka anasema ni
barabara kuu ya kwenda mikoani na kuzidi kukua kwa mji wa bagamoyo.
Bw. Banduka anasema mwaka jana, watu 3248 walipimwa damu na 368 sawa na asilimia 11.4, walipatikana na virusi vya ugonjwa huo.
Ili kuhakikisha mkoa huo unapunguza kasi ya UKIMWI, anasema mkoa unaendesha kampeni ya uelimishaji
watu ili wabadili tabia.
Mbali na mkakati huo, anasema wameanzisha kitengo cha kupima watu
ugonjwa huo kwa siri, na majibu hayo yanakuwa siri ya daktari na mhusika.
Akieleza mbinu waliojiwekea kudhibiti maambukizo ya virusi kutoka kwa
mama mjamzito kweda kwa mtoto, Bw. Banduka alisema wanawake wote wajawazito
mkoani humo watakuwa wakipatiwa vidonge.
Anasema tayari mkoa
umekubaliana na shirika moja la Hispania
linalojulikana kama Doctors of the World litakalokuwa likitoa vidonge hivyo.
Ni wazi kuwa vidonge hivyo vitasaidia watoto wasipate maambukizo ya
virusi hivyo wakati wa kuzaliwa au kwa kunyonya maziwa ya mama zao.
Mwalimu wa
shule ya Twende Pamoja ya Kibaha, Bw. Julius Mbonea mbele ya Bw. Banduka na
Bw.Rweyemamu alisema kuwa mkoani
humo kuna watoto yatima waliokwisha anza kuonesha dalili za ugonjwa huo.
Mwalimu
huyo, anasema serikali iwatafutie dawa za kurefusha siku za kuishi ambayo
yametangazwa kuwa tayari yanauzwa nchini.
Mbali na kuwa na
dalili za ugonjwa huo, Bw. Mbonea anasema watoto wengi yatima hawana makazi na
kuiomba serikali kuwapatia makazi ya kuishi..