Wanaolia
msibani hulizwa na mengi siyo kifo tu
l Njiani, wengine hucheka,
wanapokaribia msiba, wanalia kwa sauti
l Wengine
hulia huku wakishangilia kupata madaraka,
l
Wenye
uchungu zaidi, ni wanaolia sana, au wasiolia?
Na Mwandishi Wetu
KILIO cha machozi na sauti kubwa katika
msiba, kwa baadhi ya makabila huchukuliwa kama kipimo cha upendo wa mtu kwa
marehemu, ingawa wengine hucheka wakiwa njiani hadi wanapokaribia nyumba ya
msiba na kuanza kulia kwa sauti.
Ni dhahiri
kuwa msiba unapotokea, huwa kuna makundi tofauti miongoni mwa waombolezaji
wakiwamo wenye huzuni ya kweli na wanaotimiza wajibu
wa kuhuzunika na hata kulia ili wasionekane kuwa tofauti na wengine.
Wapo
wanaofurahia moyoni ili ama washike madaraka, au kurithi nafasi ya marehemu,
wapo wanaoshukuru Mungu kwani kwa kipindi cha maombolezo watautumia msiba huo
kupunguza makali yao ya maisha, wapo wanaotumia nafasi ya kifo au maafa kupora
mali za marehemu katika janga na kutaka kujitajirisha, na pia wapo wanaolia kwa
maana halisi ya kulia kwa kuondokewa na wapendwa wao.
Ingawa mara
nyingine mtu anaweza kulia kwa furaha, bado kuhuzunika
kwa wafiwa mara nyingi huhusisha kulia ingawa sio sharti wala kipimo muhimu cha
huzuni.
Katika jamii
nyingi, kulia huchukuliwa
“Unaweza
kukuta watu wakiwa wanaelekea msibani, huko njiani kote wakiwa wanazungumza na kucheka kwa furaha, lakini wanapofika karibu na nyumba
yenye msiba, huanza kupiga kelele za vilio
Ni dhahiri
kuwa msiba wa mtu unaemjua unahuzunisha uwe unamhusu
ndugu, mpenzi, jamaa au jirani, ukweli unabaki palepale kuwa msiba
unahuzunisha.
Ukweli huu
unabainisha kuwa, sio kweli kwamba wote wanaolia
Wataalamu wa masuala ya kisaikolojia wanasema kuwa, watu wenye huzuni
na mshituko mkubwa, mara nyingi huwa hawana uwezo wa kulia.
Wanasema, mtu
anayeweza kulia
Sababu za
wanasaikolojia hao ni kuwa,
mtu mwenye majonzi makubwa hususan yatokanayo na kufiwa, huwa
haamini hayo yaliyotokea na kwa kutoamini hivyo, huwa vigumu kulia.
Kwa kawaida, watu hawa huwa
wanaanza kulia baada ya mazishi kwani ndipo sasa huamini yaliyotokea na wakati mwingine, hata baada ya siku kadhaa kutokana na
matokeo halisi ya kifo hicho.
Hii ni pamoja na namna wafiwa wakiwamo watoto, ndugu na mjane
wanavyoishi katika majonzi na maisha
Hii haina
maana kuwa wanaolia baada ya mazishi ndio pekee wenye uchungu na majonzi au pengine kuliko wote wanaolia
Jambo la
msingi hapa ni kuonesha tofauti na ndio maana wakati
mwingine mtu anaweza kuwa na furaha hadi akalia na mwingine akawa na huzuni
kiasi cha kumfanya acheke.
Wanasaikolojia
wamebainisha kuwa kuna kulia zaidi ya namna moja.
Miongoni mwa
aina hizo, ni ile ya kulia kutokana na uchungu wa kweli, ipo aina nyingine
ambayo huibuka kama mazoea na nyingine ni ile ya kulia kwa kuambukizwa kutokana
na vilio na kauli za waliaji wengine na pia, athari zinazotokana na kifo hicho
katika maisha.
Watu hawa
wenye uchungu mkubwa sana huwa na ugumu katika kulia hasa baada ya msiba,
lakini kulia kwa watu hawa siyo kule kulia kwa kelele na vurugu, bali wao hulia
kwa ishara na hata kukosa nguvu ya kutoa sauti na kelele nyingi zenye shutuma
na maelezo mengi kumhusu marehemu na nafasi anayoiacha.
Waliaji wa namna hii ni wale wanaoguswa kwa namna ya pekee na kwa
undani zaidi kwani hata
Wakati
mwingine baadhi
“Kuna wale
watu ambao hulia kwenye msiba kwa sababu ya mazoea,
yaani wameshajizoesha kwamba wakisikia mtu fulani wanayemfahamu kafa ni lazima
walie bila kujali ukaribu wao au kujali
Wanawake, ni wanachama wakubwa wa kundi hili.
Kuna watu
ambao huwa inaelezwa kwamba wana machozi ya karibu, miongoni mwao ni hawa ambao
wasikiapo fulani
wanayemfahamu amekufa, na hasa wanapokwenda kwenye misiba
Inawezekana
hawakuwa karibu
Kuna watu ambao hulia kwa kulizwa. Watu hawa wanapokwenda misibani huwa wanachotwa
kirahisi na haraka na kauli za waombolezaji na hasa
zile za wale wanaolia huku wakitoa kauli kali na zenye kusikitisha kuhusu
marehemu au kifo.
Kuna watu
ambao wanapolia hutaja kila kitu alichokuwa akikitoa marehemu; au kukifanya na hata namna alivyosema dakika chache kabla hajafa au
mengine ya aina hiyo. Waliaji hao tunaweza kuwaita “wenye hisia kali”
Kwa kusikia
kauli za aina hiyo, baadhi ya watu huwa wanajibainisha au kujiweka karibu
Mara nyingi
anaweza hata asionwe na watu alionao karibu.
Aina nyingine
ni ile inayohusisha kulia kwa nguvu
Hapa waliaji
huwa wanalia bila kujali mazingira na bila kujali
muda.
Imebainika
kwamba wengi wa waliaji hawa huwa ni wale ambao
wanajua wazi kwamba kifo cha mhusika kimewaacha pabaya kimaisha.
Unaweza
kukuta marehemu ndiye aliyekuwa akiwapa kila kitu katika maisha
Wengi kati ya
watu hawa ni ndugu, wazazi, watoto, waume au wake wa
marehemu.
Hata
ukisikiliza kauli zao katika kulia kuna wakati hutaja hofu ya kuishi peke
Miongoni mwa
hawa waliaji kuna wale ambao kifo cha mhusika kina maana wao kupoteza kitu fulani (
Kuna wakati
inawezekana marehemu alikuwa ndiye anayetatua migogoro mingi na
mikubwa ya kifamilia na hivyo, kufa kwake huchukuliwa
Siyo kwamba
watu wanaolia
Kwa sehemu
kubwa wana uchungu wa kumpoteza mhusika
pengine wana
uchungu zaidi, lakini ukweli ni kwamba wanazingatia zaidi
watakavyokabili ugumu wa maisha.
Ukiangalia
kwa makini utaona kwamba wengi kati ya wale wanaolia
kwenye misiba, hulilia nafsi zao zaidi kuliko kumlilia marehemu.
Hata hivyo,
ukweli unabaki palepale kwamba kulia
Kulia
Dini
zetu kuu zinafahamu
Ni kumdhihaki
kwa sababu kifo au uhai ni maamuzi yake na hivyo, kulia ni sawa na
kumwambia kwamba amekosea.
Inabidi jamii
ikubali kwamba hakuna anayeweza kuishi milele isipokuwa Mungu ambaye alikuwapo
tangu milele, yupo hadi sasa na bado atakuwapo katika
milele yote.
Lazima watu
waone umuhimu wa kuishi maisha ambayo kifo
kinapotokea, iwe ni miili tu iliyokufa lakini, imani, mawazo na busara za
marehemu ziwe bado hai.
Huo ni wakati
ambapo wazazi, ndugu na marafiki, hawana budi kuwasaidia wanaowategemea
ili wajitegemee na kuepuka kuendelea kuwa wategemezi.
Hata kwa ndugu ambao kwa kiasi kikubwa wanamtegemea mtu fulani
dawa ni kuwafanya wajitegemee na siyo kuona ufahari kwa kuwa tegemezi.
Lakini, kubwa
zaidi ni kwamba kulia kwa sababu fulani amekufa na
sasa maisha yetu yatakuwa magumu ni udhaifu mbaya
Kulia kwa namna hii kunaonesha ni kwa kiasi gani hatujiamini na ni
kiasi gani tunadhani utu na ukamilifu wetu uko mikononi mwa watu wengine.
Tunapolia kwa sababu fulani amekufa na sasa maisha yatatuwia magumu,
tunadhihirisha kwamba hatuko kamili na tunahitaji kujitazama upya.
(JITAMBUE Mei 23-29, 2001).
‘Mnaokosea makusudi kutegemea msamaha,
mnajidanganya’
Na Damasus Mtalaze,
MUNGU hatoi msamaha kwa makosa yanayotendwa kwa makusudi na watu eti ili baadaye
waungame; Amesema Paroko wa Parokia ya Kibakwe, Jimbo Katoliki la
Akihubiri parokiani
kwake hivi karibuni, Paroko huyo, Padre Faustin Mwenda, alisema baadhi ya watu hufanya makosa kwa makusudi
huku wakitegemea kupata msamaha baada ya kuomba radhi na kuungama hali
aliyosema, ni kinyume na mapenzi ya Mungu.
“Wengine wanatenda
makosa kwa makusudi eti kwa kuwa Injili inawalinda,
hao wanajidanganya kwa sababu Mungu husamehe makosa yanayotokana na kushindwa
kuyakwepa au yanayofanywa bila mtu mwenyewe kujua kuwa anafanya kosa; sio
kufanya mambo makusudi ukitarajia kusamehewa,” alisema Padre Mwenda.
Akaongeza, “Siku zote; mtu asiuangalie wema wa Mungu kwa kuuchezea maana ukicheza na huruma ya Mungu,
ujue unacheza na ghadhabu yake.”
Akitoa mfano, Padre Mwenda, alisema kuwa
hukumu dhidi ya Adamu na Hawa, inatokana na kosa
lililowaponza la kudharau na kukosa kuitii Amri ya Mungu na hivyo, wakala tunda
walilokatazwa wakitegemea kuwa watasamehewa kwa kuwa tangu awali walikuwa
wakitii maagizo ya Mungu isipokuwa
“Ukiamua kutii, ni vema utii
kabisa maana Mungu hutoa adhabu palepale unapoanza kutenda kosa,” alionya.
Alisisitiza kuwa, sio vema kwa mtu yeyote kutatiza maisha ya mwingine kwa kutomsamehe anapokukosea hali wewe mwenyewe ukimkosea mtu, unahitaji kusamehewa.
Wanasayansi wakiri sala zinatibu kuliko
dawa
l Profesa asema imani katika
Mungu ina manufaa
l ‘Hatutaki kuuza dini kwa jina la sayansi’
Na Joseph Sabinus
MANENO “Imani katika matendo,” sasa yameleta maana
mpya kwa jamii duniani kote hasa baada ya wanasayansi kuthibitisha kuwa imani
katika Mungu, ni dawa yenye nguvu dhidi ya magonjwa.
Katika makala ya “Imani Ni Dawa Yenye Nguvu”, iliyoandikwa na
Phyllis McIntosh na kuchapishwa katika kitabu cha “Than Diabetes,” kundi la
wanawake lilikuwa likikutana kwa wiki mjini humo ili kufanya mazoezi ya kiroho na kimwili sambamba na dawa
zilizoambatana na baraka za asubuhi za Wayahudi.
Roberta Schweitzer, Mmoja wa
washiriki ambaye ni Muuguzi, alifurahishwa na utulivu uliokuwapo kutokana na
sala zilizokuwa zikiendelea.
Schweitzer ambae ni Profesa Msaidizi
katika Chuo Kikuu cha
Alisaidia pia kuandaa mpango maalumu wa
kuwafundisha watu kutumia matibabu ya kiroho kukabiliana na magonjwa.
Dhana kuwa mwili unaweza kuponywa kwa
imani ya kiroho, si kitu kigeni. Watu wamekuwa wakisikia mara nyingi kuwa
wagonjwa wanapona katika imani na maombi baada ya kuugua kwa muda mrefu au hata
kupona na
pengine, kuishi na maradhi kwa muda mrefu kuliko hata madaktari walivyofikiri
kuwa inawezekana.
Kwa sasa, jambo lililo jipya, ni kwamba imani ya kidini sasa
inakuwa chanzo na
msukumo wa sayansi duniani.
“…Hatuwezi kuthibitisha kisayansi kuwa Mungu anaponya, lakini
ninaamini kuwa tunaweza kuthibitisha kuwa imani katika Mungu ina manufaa
makubwa,” alisema Dk. Dale A. Matthews ambaye ni Profesa Mshiriki
katika Chuo Kikuu cha Tiba cha
“Mashaka yaliyopo ni madogo
Nguvu za ushahidi wa wanasayansi
zinasema kuwa zaidi ya tafiti 30 zimebaini kuwapo uhusinao wa kiroho (imani ya
kidini), na maisha marefu ya watu.
Katika utafiti uliofanywa kwa
Wacarifonia 5286, ilibainika kuwa Wanakanisa wana kiwango kidogo cha uwezekano
wa vifo kuliko wasio na dini, ukiachilia mbali vigezo vinavyotokana na tabia na
matatizo ya kuvuta sigara, unywaji pombe, vitambi na kutofanya kazi na mazoezi.
Pia, katika tafiti 8 juu ya kansa,
tafiti 7 zilibainisha kuwa, wanaojitoa na kujishirikisha kikamilifu katika
imani za kidini, wana dalili chache na wana matokeo bora ya kiafya kuliko
wasiojishirikisha na imani za kidini.
Tafiti nne pia kati ya tano zilifanywa juu ya mgandamizo wa
damu katika mwili wa binadamu, tafiti nne kati ya sita juu ya ugonjwa wa moyo
na tafiti nne kati ya tano juu ya afya kwa jumla, zikabainisha kuwa
wanaojihusisha na imani za kidini wanadalili chache au wana nafuu zaidi kuliko
wasiojihusisha kabisa na dini.
Utafiti mwingine ukabainisha kuwa, watu wenye imani kali za
kidini, hawana mwelekeo na wala hawavutiki katika
unywaji pombe, kujiua na hata kushiriki mambo mbalimbali ya uovu.
Uchunguzi mwingine wa kina umeonesha
kuwa muunganiko baina ya dini na afya, unavuka umri, jinsia, utamaduni na
mipaka ya kijiografia.
Uchunguzi huo unazihusisha pia, zaidi ya tafiti 200
zilizothibitisha kuwa imani ya kidini ni kigezo muhimu
katika kupambana na maradhi, alisema Jeffrey S. Levin, Profesa wa
Levin alibaini uhusiano baina ya afya njema na dini katika tafiti zilizowahusisha watoto na wazee
Waprotestanti wa
Mintarafu ni jinsi gani imani
inaonekana kuwa na nguvu za kinga kiasi hicho, wataalamu wanatoa majibu
mbalimbali.
“Tabia ya kujitoa katika imani za kidini, huwawezesha watu
kushughulikia vema magonjwa na hasara,” anasema Dk.
Harold G. Koeng, Mkurugenzi wa Kituo cha Mafunzo ya Dini, kiroho na kifya
katika Chuo Kikuu cha
Kusali huleta mabadiliko mengi ya manufaa
katika mwili. Dk. Harvard Benson wa
Kusali rozari kwa mfano, kunahusisha
hatua
Benson anazidi kusema kuwa, wanaochagua imani za kidini huwa
katika nafasi kubwa ya kufaidi
Katika utafiti mwingine kuthibitisha nguvu za sala kuwa bora
katika uponyaji, Dk. Biyrd aliwagawa wagonjwa wa moyo
393 wa Hospitali ya San Fransisco General Hospital Medical Center, katika
makundi mawili.
Kundi la kwanza, lilifanyiwa maombi na
Watafiti Wakristo nchini kote, lakini kundi lingine halikufanyiwa maombi na
sala hizo. Hata hivyo, wagonjwa hawakujua kuwa walikuwa
katika kundi lipi katika ya hayo.
Kundi lililoombewa, lilibainika kuwa na matatizo kidogo zaidi
ya magonjwa
Madaktari nao ni waamini wazuri sasa.
Dk. Dossey, hatimaye alishawishika juu
ya nguvu za sala na akaanza kuwaombea
wagonjwa wake kwa sala zake binafsi.
Hata hivyo, yeye na wenzake, hatimaye
wakaitahadharisha jamii katika eneo hilo kwa kusema, “Hatutaki kuuza dini kwa
jina la sayansi,” alisema na kuongeza kuwa, Watu wanahitaji kufanya uchaguzi
wao wenyewe.”
Mpaka sasa, vituo vya afya kwa kutambua
umuhimu wa sala na maombezi, vimeanza kuwa makini na uhusiano ulipo baina ya
afya na imani.
Mikutano juu ya roho na afya imekuwa
ikidhaminiwa na Harvard Medical School, pamoja na Mayo
Clinic.
Karibu nusu ya Shule za Kitabibu za U.S, sasa zinatoa kozi
juu ya mada ya uhusiano baina ya afya na imani.
Katika utafiti wa madaktari 296, katika mkutano wa American
Academy of Family Physicians, asilimia 99 walisema wanaamini kabisa kuwa imani
za kidini zinachangia kwa kiasi kikubwa katika uponyaji.
Walipoulizwa juu ya uzoefu wao binafsi, asilimia 63 ya
madaktari hao, walisema Mungu aliwasaidia kuboresha hali zao za kitabibu.
Kwa uwazi kabisa, hata wagonjwa wao wanakubali kuwa SALA
NI KIFAA CHENYE NGUVU KATIKA UPONYAJI.
“Karibu asilimia 80 ya Waamerika, wanaamini kuwa imani za kiroho(sala), zinaweza kuwasaidia watu kupona kutokana na
magonjwa au maumivu waliyonayo na zaidi ya asilimia 60 wanafikiri kuwa, ni vema
madaktari wangefanya mpango wa kuzungumza na wagonjwa wao juu ya imani za
kidini na hata kusali pamoja na wagonjwa wanaotaka. (Polls
by Time? CNN and
Hata hivyo, unachotakiwa kufanya, unapougua na unahitaji imani yako ya kidini ikusaidie na kuwa sehemu
ya uponyaji na kigezo cha afya yako; ni kusema wazi mbele ya Mungu wako na
kuufungua moyo huku ukimkaribisha Yesu afanye kazi ndani yako.
Hapa haimaanishi kwamba umtegemee Daktari akuombee au asali
pamoja na wewe tu, ingawa ni muhimu kumtegemea
akusikilize mahitaji yako, apange utaratibu wa kutembelewa na padre mlezi wa
hospitali au, aruhusu muda wa sala kabla ya kuingizwa katika chumba cha
upasuaji.
Basi ni wakati
sasa kila jambo linalofikiriwa, linalofanyika, lifanyike kwa kuzingatia mapenzi
ya Mungu na imani thabiti.
Wanaopokea Kipaimara wasibweteke na mafuta Matakatifu- Pengo
Na Elizabeth Stephen
ASKOFU
Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama
Polycarp Kardinali Pengo, amesema wanaopokea Sakramenti katika Kanisa ikiwamo
ya Kipaimara, wasiridhike kwa kupakwa mafuta matakatifu, bali waongeze
bidii katika kuihubiri Injili kwa watu.
Kardinali
Pengo aliyasema hayo katika Ibada ya Sakramenti ya Kipaimara iliyofanyika,
Jumamosi iliyopita katika kanisa la Parokia ya Makuburi, jimboni humo.
Katika Ibada hiyo, Kardinali
Pengo alitoa Sakramenti ya Kipaimara kwa vijana 346.
Kati
Aliwataka vijana waliopokea
Sakramenti hiyo kuiga mfano wa Mtume Mathayo kwa
kutenda mambo yanayompendeza Mungu na hivyo, kuepuka uovu wote.
“Mtume Mathayo aliacha kazi ya
kutoza ushuru na kumfuata Yesu, hivyo nasi tunaopata
Kipaimara tuimarike kiimani na tubaki na wito uleule aliotuelekeza Mtume
Mathayo… Bwana Yesu anatuita kwa njia ya kutupaka
mafuta,” alisema Kardinali.
Akaongeza, “Sakramenti hiyo
iwe chimbuko la pekee kwa kila mmoja wetu kutembea
pamoja na Kristo".
Wakati huo huo:
Akisoma risala kwa niaba ya Parokia hiyo, Mwenyekiti Msaidizi wa Halmashauri ya
Walei, Parokia ya Makuburi Ndugu. Lyimo alimpongeza Kardinali Pengo kwa
kuteuliwa hivi karibuni na Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili kuwa Mjumbe
katika Idara ya Mafundisho ya Imani.
Aidha,
walimshukuru Askofu kwa kuwaletea mapadre wenye imani
na misimamo iliyonyooka ambayo imefanya Parokia ya Makuburi kuimarika kiimani
na kimaadili.
Parokia ya
Njombe yaongezwa wachungaji
Na Frt. Carlo Mwalongo, Njombe
PAROKIA
ya Njombe Mjini katika Jimbo Katoliki la Njombe, imeongezewa mapadre wawili ili kukidhi mahitaji ya kichungaji katika vigango vyake, imefahamika.
Mwenyekiti
wa Halmashauri Walei, Jimbo la Njombe, alisema kwa
niaba ya Paroko wa Parokia ya Njombe, Padre Erasmo Lugome, kuwa ingawa Parokia
hiyo ina vigango 31 vinavyoweza kuunda parokia tatu, bado imekuwa ikihudumiwa
na mapadre wawili.
Aliyasema hayo hivi karibuni wakati akizungumza katika
Ibada ya Jumapili, katika Kanisa la Mtakatifu Yosefu, Njombe Mjini.
Alisema, “Ongezeko la mapadre hao litaleta mafanikio
zaidi kiroho na kimwili.”
Aliongeza
kuwa, ni wajibu kwa waamini wa Parokia hiyo kuwapokea
vema na kuwapa ushirikiano mapadre hao wageni, ili watimize vema majukumu
waliyotumwa na Mungu ili wayafanye katika Parokia hiyo.
“Inatupasa
kuwaheshimu, kuwasikiliza na kuwatii kwa sababu kazi
wanayoifanya wamekabidhiwa na Mungu,” alisema.
Akiwakaribisha
mapadre hao, Zenobius Mtewele na Edmund Kayombo, Paroko wa Parokia hiyo, Padre
Lugome, alisema mapadre hao wajisikie vema kuanza kuhudumia waamini wa eneo
hilo na kwamba, kwa namna anavyowafahamu waamini hao, anaamini kuwa mapadre hao
watapata ushirikiano unaotakiwa.
Katika
ibada hiyo, Padre Mtewele alisema, “Bahati mbaya Wakristo hawapewi nafasi ya
kuchagua mapadre wa kuwahudumia, nasi mapadre hatupewi
nafasi ya kuchagua parokia za kwenda kuhudumia, hivyo tunaomba mtupokee kwa
sababu sisi
Naye
Padre Kayombo, alisema, “Kazi tuliyopewa ni ya Mungu
siyo yetu, hivyo tunaomba tushirikiane ili tuifanikishe.”
Padre Mtewele kutoka Parokia ya Matola alipata Daraja
la Upadre Juni 10, 2001 katika Parokia ya Njombe Mjini. Kisha alikuwa Msaidizi wa
Paroko wa Madunda na sasa ni Mlezi wa Vijana, parokiani hapo.
Naye
Padre Kayombo alipata Daraja la Upadre Juni 27, 2002 katika Parokia ya Mlangali
pamoja na Padre Dietram Mwinuka. Sasa ni Msaidizi wa
Paroko katika Parokia
ya Njombe Mjini.
Mapadre
wengine waliopata Upadre mwaka huu jimboni humo ni
Padre Bosco Mwenda wa Parokia ya Njombe Mjini, Padre Bononius Mkonga na Padre
Laurent Mwalongo wa Parokia ya Lugenge walipata Upadre Juni 30, 2002 katika
Kanisa la Njombe Mjini.
‘UKIMWI ajali kazini! Hujui usemalo'- Askofu
Ngalalekumtwa
Na Getrude Madembwe, Iringa
“ETI mtu anafahamu kabisa UKIMWI ni
ugonjwa hatari, lakini hajali na badala yake, anasema ni ajali kazini! Ajali gani hiyo wakati unajitakia mwenyewe!”
Hayo
yalisemwa na Askofu wa Jimbo Katoliki la Iringa,
Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa, wakati akitoa salamu kwa waamini wa Parokia
ya Kihesa jimboni humo hivi karibuni.
Alisema
kauli na tafsiri potofu za watu wenye uelewa finyu
kuwa UKIMWI ni ajali kazini, ni hatari na zinazopaswa kupuuzwa na kila mwenye
akili timamu.
Alisema
UKIMWI si tatizo bali matokeo ya wanadamu kumkaidi
Mwenyezi Mungu kwa kushiriki vitendo vinavyopingana na Amri za Mungu ikiwamo
inayozuia kuzini.
“Watu
wanakwenda kinyume na maagizo ya Mwenyezi Mungu,
wanavunja miiko na ndio hao wanaowafanya hata wengine wafikirie njia haramu za
kupambana na UKIMWI,” alisema.
Mhashamu
Ngalalekumtwa alitoa mfano wa mti unaoanza kukauka,
ambapo huanza kwa kudondosha majani na kisha, usipochunguzwa mapema, huanguka
wenyewe.
“Inabidi
mtu achunguze ni kwanini majani hayo yanadondoka
badala ya kusubiri hadi mti huo uanguke ndipo aanze kutafuta chanzo,” alisema.
Aliendelea kusema kuwa, watu wengine hufanya
makosa kwa kutafuta njia za mkato za kupambana na
tatizo la UKIMWI, badala ya kutafuta kiini ambacho ni zinaa hivyo kuachana nayo
na kuishi kimaadili.
Aidha,
Mhashamu Ngalalekumtwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa
Liturujia katika Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), alisema viongozi
wa dini wakiwemo Maaskofu hawatachoka kuwahimiza waamini juu ya kuacha zinaa
“Ole wao wale watakao hamasisha matumizi ya
kutumia zana mbalimbali kuzuia UKIMWI zaidi ya kumrudia Mungu, maana wanapinda
ukweli juu ya jambo
Wakati huo huo:
Mhashamu Ngalalekumtwa amewataka vijana kutoyumbishwa na
mambo ya dunia bali waishi katika njia ya kweli ya Bwana Yesu Kristo kama
Maandiko Matakatifu yanavyosema.
“Msifuatishe
namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia
zenu mpate kujua hakika ya mapenzi ya Mungu (Warumi 12:2).
Alitoa
kauli hiyo hivi karibuni wakati akihubiri katika Ibada ya Misa Takatifu ya
Sakramenti ya Kipaimara kwa vijana 366,iliyofanyika
katika Parokia hiyo ya Kihesa.
“Mabango,
vipeperushi, video, filamu, internet Cafe na
mambo mengine
Katika tukio jingine: Kanisa Katoliki Jimbo la Iringa, limebuni
mbinu mpya za kuwaepusha wenye imani ndogo wasidanganywe na kukimbilia katika
madhehebu na dini nyingine.
Katika
maazimio ya Mkutano wa hivi karibuni wa Halmashauri ya Kichungaji jimboni humo, uliofanyika Tosamaganga, mbinu
hizo zimetajwa kuwa ni pamoja na kuwa na
ujuzi wa kutosha kuhusu misingi ya imani ya Kanisa Katoliki hasa nyaraka
zitolewazo na viongozi wa Kanisa.
Nyingine
ni kutowaacha wenye upweke katika matatizo na shida
mbalimbali za maisha
Mkutano
huo uliongozwa na Askofu wa Jimbo katoliki la Iringa,
Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa, pia uliazimia kutoa semina za kiroho mara kwa
mara kwa wanafamilia ya Mungu, zenye lengo la kuimarisha uhusiano na Kristo na
kuchochea upendo wa Kanisa Katoliki.
Maazimio hayo pia yamewasisitiza wazazi
na walezi wa familia, kuyapiga vita maandishi,filamu, video na mitandao yenye
kupotosha usafi wa moyo na kuimarisha uhimizaji wa yale yanayojenga akili na
roho.
Mchungaji
KKKT afananisha mwili, simu ya mkononi
Na Godwin Kaijage, DSJ
KIONGOZI
mmoja wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania
(KKKT), ameufananisha mwili wa binadamu na simu ya mkononi inayopokea kadi za
njia za simu ‘line’ toka makampuni mbalimbali.
Kwa mujibu wa Mkuu wa KKKT,
Jimbo la Ilala, Mchungaji Julius Mong’ola, Kiongozi huyo Mchungaji Daniel
Christopher wa Usharika wa Unga LTD, Arusha,
aliyasema hayo hivi karibuni wakati akizungumza usharikani Kipawa, Dar
es Salaam, alipotembelea Usharika huo pamoja na Kwaya ya Vijana toka Unga LTD
Arusha.
Mchungaji
Mong’ola alimnukuu Mchungaji Christopher toka Arusha akisema, “Unaweza kuingiza
kadi yoyote kwenye simu ya mkononi.
Ukiingiza kadi ya Mobitel, itakuonesha Mobitel, ukiingiza
kadi ya Vodacom, itaonesha Vodacom. Na maisha ya mtu ndivyo yalivyo,
ukiingiza kadi ya shetani utaonekana kuwa ni wa
shetani na ukiingiza kadi ya Yesu, utaonekana kuwa wewe ni wa Yesu.”
Alisema ni
vema binadamu wote wakaamua kwa moyo kuingiza kadi ya Yesu katika maisha
Katika mazungumzo hayo,
Mchungaji Mang’ola alisema, mtindo wa vikundi na asasi
za dini kutembeleana kwa lengo la kufanya kazi ya Mungu, hauna budi kuimarishwa
na wote wenye mapenzi mema katika Kristo ikiwa ni njia muhimu ya
kuimarishaUkristo duniani.
Kwa mujibu wa
Mchungaji Mang’ola, Mchungaji Christopher aliwasili na Kwaya ya Vijana jijini
Dar es Salaam, wakiwa na kanda tano huku Kwaya hiyo ikikusudia kurekodi kanda
ya sita iitwayo Maisha ya Kukaa Ndani ya Yesu.
Majina ya kanda zilizorekodiwa na tayari
zinauzwa ni Alaaniwe
Mtu Yule, Jamani Mnayo habari, Tukumbuke Siku Hizi za