WAWATA
wakabidhiwa kulea Utoto Mtakatifu wa Yesu
l Mkurugenzi asema kazi ya watoto huzaa matunda mengi, wanaweza kuwafundisha hata maaskofu
Na Neema Massawe, DSJ
WAKATI
Wanawake Wakatoliki Tanzania (WAWATA) wamekabidhiwa jukumu la kulilea Shirika
la Kimisionari la Utoto Mtakatifu wa Yesu nchini, Shirika
Mkurugenzi wa Shirika hilo
katika Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Padre Timothy Maganga Nyasulu,
aliyasema hayo Jumamosi iliyopita katika mkutano wa walezi mbalimbali,
waliokutana katika Ukumbi wa Mikutano wa Parokia ya Mtakatifu Yosefu jijini Dar
es Salaam,ili kujadili maandalizi ya Sikukuu ya Watoto Mashahidi
inayoadhimishwa Desemba 28 kila mwaka.
Katika
Mkutano huo ambao pia ulijadili juu ya siku maalumu ya watoto kufanya matendo
ya huruma jimboni humo Desemba 26, Padre Timoth alisema kuwa, wazazi na jamii
kwa jumla, hawana budi kuwafundisha watoto kuishi kwa upendo na kusaidiana huku
wazazi nao wakionesha mifano bora na hai.
“Tuwe
wakweli na tusimamie ukweli siku zote…mtoto akioneshwa mtu kwa lugha ya chuki,
atakuwa na chuki hiyo naye atafundisha wengine… Mara nyingi tumeona na
kuthibitisha kuwa watoto wanaweza kuwafundisha hata Maaskofu wakaelewa vitu
vingi…” alisema.
Akaongeza,
“Kazi ya watoto haipotei; inazaa matunda na kazi ya watoto, ina thamani kubwa
si mbele ya watu tu, bali hata mbele ya Mungu.”
Mintarafu
siku hiyo, Padre Timothy alishauri parokia zote kufanya mipango maalumu ili
watoto ambao hawatapata nafasi ya kufanya matendo hayo ya huruma katika vituo
maalumu, waandaliwe utaratibu ili watoe huduma zao kwa watu wenye matatizo
katika maeneo wanayoishi watoto hao.
“
…Tuwe makini ili watoto wasijenge utamaduni wa kudhani kuwa matendo ya huruma
ni kwa hospitali, magereza na katika vituo maalumu pekee. Wanaokosa nafasi
wafanyiwe utaratibu wa kuwatembelea wenye matatizo waliopo katika maeneo
Alisisitiza
watoto wenye ulemavu washirikishwe katika mambo mbalimbali ya kijamii. “Watoto
ni rahisi kujikubali hali zao na wenzao kuwakubali,” alisema.
Katika
siku ya matendo ya huruma, watoto hao huwatembelea watoto wanaolelewa katika
vituo mbalimbali wakiwamo yatima, wagonjwa, na pia watu mbalimbali wenye shida
huku wakiwapa misaada waliyonayo kusali, pamoja na kuzungumza nao.
Katika Mkutano huo ambao uliwashirikisha wawakilishi wa WAWATA toka maparokiani, masista na wadau wengine, Bw. Majani, alisema kuwa, katika tamasha la Utoto Mtakatifu wa Yesu lililoadhimishwa hivi karibuni katika Parokia ya Tabata, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Mashirika ya Kimisionari nchini (PMS), Padre Liberatus Mwenda, alitangaza rasmi kuwa WAWATA ndio Walezi rasmi wa Shirika la Kimisionari la Utoto Mtakatifu wa Yesu nchini.
Msiende Kanisani kuonesha mavazi,
nendeni kusali - Mch. Moravian
Na Brown
Sunza
KIONGOZI mmoja wa Kanisa la Moravian Tanzania (KMT),
ameiaumu tabia ya baadhi ya waamini wa madhehebu mbalimbali kwenda kanisani kwa
nia ya kuonesha mavazi badala kupeleka maombi
Kiongozi
huyo wa Usharika wa Magomeni katika
Wilaya ya Mashariki, Jimbo la Kusini, Mchungaji Arimanura Masongera,
alisema wakati akizungumza na KIONGOZI
jijini Dar es Salaam, kuwa wapo baadhi ya waamini wenye tabia mbaya ya
kwenda kanisani ili kuwatia vishawishini waamini wengine wenye nia
ya kumwomba Mungu.
“Baadhi
hawana lengo la kusali ila wanafika kanisani ili kutimiza wajibu na baadhi
Aliwataka
waamini wenye tabia hiyo watambue kuwa kanisani ni mahali patakatifu ambapo kila mtu anaruhusiwa
kuingia na kusali kadiri ya imani yake,
lakini si mahali pa kuoneshana uwezo wa mtu kiuchumi.
Aidha,
Mchungaji Alimanura alisema kuwa, kukithiri kwa
ubinafsi miongoni mwa jamii, uumedumaza maendeleo.
Alisema
baadhi ya watu wana uchoyo wa kushiriki katika
shughuli za kuleta maendeleo ama
kimawazo, au kivitendo.
Alisema,
kuwa si sahihi jamii kusingizia uduni na ugumu wa maisha kuwa ndiyo chanzo cha
kudidimiza maendeleo.
“Ubinafsi hauna
tajiri , msomi , wala masikini ni
kitu kilichopo ndani ya moyo
wa mtu” alisema .
Aliwataka
waamini kushirikiana pindi linapotokea jambo la kuweza kuleta maendeleo katika
mazingira wanayoishi.
Mchungaji huyo alisema katika jitihada za kuleta maendeleo ya kweli,kuna haja kwa serikali kurejesha Mashirika ya Umma vijijini. Sambamba na hayo amewataka watu wenye mawazo binafsi wayatoe katika barua za wasomaji hususani kwa magazeti yote yenye utaratibu wa kutoa nafasi hizo ili kubaini matatizo yanayoikabili jamii kwa wakati unaofaa na kupelekwa mahali panapohusika ili kupewa ufumbuzi wa haraka kabla ya madhara kutokea.
Chuo Kikuu kuchangia Milioni 20/- kuzuia mmomonyoko
Na Dalphina Rubyema
UONGOZI
wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ,umesema kuwa uko tayari kuchangia kiasi cha sh.milioni 20 kwaajili ya kuzuia
mmomonyoko wa undongo unaoendelea katika bonde la Chuo hicho.
Kauli
hiyo ilitolewa hivi karibuni na Afisa
Mkuu wa Utawala chuoni hapo, Profesa John Mshana wakati akijibu risala kutoka
kwa Mwenyekiti wa Utunzaji Mazingira,
Bw.Emmanuel Mbasha, aliyoitoa wakati wa sherehe za upandaji miti chuoni hapo.
Katika
risala yake hiyo,Bw.Mbasha alieleza kuwa zaidi ya sh.milioni 20 zinahitajika
kwa ajili ya kununulia vifaa mbalimbali ili kuweza kujaza katika bonde
Akijibu
risala hiyo,Profesa Mshana ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo za
upandaji miti,alisema ofisi yake itasaidia kutatua tatizo
“Ofisi
ya chuo iko tayari kutoa msaada,mnachotakiwa
kufanya ni kuorodhesha idadi ya vitu vinavyohitajika nasi tutawataarifu
nini tutachangia”alisema Profesa Mshana.
Awali
katika risala yake,Mwenyekiti huyo wa Utunzaji wa Mazingira,alisema kuwa mbali
na mvua, pia bonde hilo linazidi kuchimbika kutokana na baadhi ya watu
kuendelea kuchimba mchanga kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa
nyumba.
Hata
hivyo Bw.Mbasha alisema kuwa wananchi
wanaozunguka eneo
Kanisa Katoliki jimboni Moshi lazindua maandalizi ya Jubilei ya Dhahabu
Na Mwandishi Wetu
KANISA Katoliki
jimboni Moshi,limezindua rasmi maandalizi ya Jubilei ya Dhababu ya Jimbo.
Uzinduzi huo
ulienda sambamba na adhimisho la Misa Takatifu iliyoongozwa na Askofu wa Jimbo
hilo,Mhashamu Amedeus Msarikie, ambaye katika mahubiri aliyoyatoa kwa .mamia ya
waamini waliohudhuria Misa hiyo
iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Kristu Mfalme, aliwataka waamini kufanya
maandalizi kabambe ya kusali kwa nia dhabiti wakati wa maandalizi,maadhimisho ya baadaye.
Aliwaalika kufanya toba ya kweli ili kuitikia mwaliko
wa Bwana wetu Yesu Kristu. wa kuwa wakamilifu
Wakati wa maandalizi ya maadhimisho hayo,waamini
watapata nafasi ya kumwenzi Mama Bikira
Maria kwa Ibada mbalimbali.
Vile vile sanamu ya Bikira Maria Mhujaji
Siku hiyo ya uzinduzi wa Jubilei,Mhashamu Msarikie
alibariki sanamu tatu kwa ajili ya Vikariati zote tatu zilizomo jimboni humo.
Sanamu hizo zilikabidhiwa rasmi kwa Mapadre wa
Vikariati hizo ambazo ni Rombo,Vunjo na
Hai.
Kipindi hicho cha
Maandalizi ya Jubilei kimeanza tangu Agosti 18 mwaka huu na kilele chake ni
Machi 23 mwaka kesho.
Katibu wa Miradi
Moravian ahofia UKIMWI kuacha makanisa matupu
l Mch. Asema wanawake wakitaka,
utakwisha
Na Mwandishi Wetu
KATIBU wa Miradi
na Uwakili, wa Kanisa la Moravian Tanzania (KMT), Wilaya ya Mashariki, Jimbo la
Kusini, Bw. Yonah Sonelo, amesema hali inazidi kutisha kwani waamini na
viongozi mbalimbali wa kiroho wanakufa kwa UKIMWI na hivyo, makanisa yamo
hatarini kubaki matupu.
Bw. Sonelo alikuwa akizungumza katika ibada
iliyofanyika Jumapili iliyopita katika Kanisa la KMT, Usharika wa Keko,
Wilayani kwake, ikiwa ni sehemu ya ziara yake katika sharika za Wilaya hiyo.
Alisema kwa kuwa awali baadhi ya watu walifikiri UKIMWI
ni utani na hivyo kutozingatia tahadhari, vifo na madhara ya UKIMWI
yanayoonekana sasa duniani hayana budi kuwafanya watu wamgeukie Mungu na hivyo,
kufuata njia sahihi za kuepukana nao.
“Inatia uchungu, watu wanazidi kwisha na haya makanisa
yetu tunayojenga tusiposhituka sasa na kumgeukia Mungu, tutakwisha wote na
yatabaki makanisa matupu,” alisema.
Naye Mchungaji wa Ushirika huo, Salatieli
Mwakamyanda, alisema wanawake wanayo
nafasi kubwa kuamua
“…Ninaamini kabisa
Ugonjwa wa UKIMWI ambao unazidi kuangamiza mamilioni
ya watu, kwa kiasi kikubwa huenezwa kwa njia ya kuvunja Amri ya Mungu inayozuia
kuzini.
Aidha, Mchungaji Mwakamyanda, alihimiza kila mwanandoa
kuiheshimu ndoa yake na kuitii Amri ya Mungu ya kutokuzini huku, wasio na ndoa
wakibaki waaminifu bila kushiriki vitendo vya ndoa.
Alisema endapo jamii itaelewa usahihi huo, upo
uwezekano mkubwa wa kushinda vita hii.
Njia nyingine
zinazochangia kuenea kwa ugonjwa wa UKIMWI, ni kuchangia vyombo vya kutogea
visivyochemshwa sawasawa, kuongezwa damu isiyopimwa, na mawazo potofu ya
kuamini kondomu
WAWATA Moshi
waadhimisha miaka 30
Na Aneth Mwakatobe, SAUT, Moshi
WANAWAKE Wakatoliki Tanzania (WAWATA), Jimbo la Moshi,
wameadhimisha miaka 30 tangu Umoja huo uanzishwe hapa nchini sambamba na
uoneshaji wa kazi za mikono.
Maadhimisho
hayo, yalianzia ngazi ya vigango, parokia na hatimaye kilele chake kufanyika
ngazi ya Jimbo.
Maonesho
ya kazi za mikono za wana WAWATA, yalizinduliwa na Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa
wa Kilimanjaro, Bibi Betty Minde ambapo katika nasaha zake, aliwataka akinamama
hao watambue kuwa jukumu la malezi walilo nalo ni zito hasa siku hizi.
Aliwataka
wawe walezi bora na imara, waimarishe malezi adilifu, wawe tayari kukemea na
kupambana na maadili potofu na mabovu, umasikini na uchumi tegemezi na pia
kupambana na kuenea kwa UKIMWI.
“Mwanamke
ana nafasi muhimu
Maadhimisho
hayo yaliyo hudhuriwa na Parokia 31 kati ya 48 za Jimbo
Parokia za Kindi, Chekereni na Korongoni ndizo zilizoibuka washindi wa maonesho ya kazi za mikono za akina mama hao.
Bunini mikakati ya kupata pesa, msitegemee
misaada-Monsinyori Kangalawe
Na Leocardia Moswery,SAUT
WAAMINI
wa Kanisa Katoliki nchini wametakiwa kushirkiana katika kubuni mikakati ya
kupata kipato cha kuendesha Mashirika ya Kipapa badala ya kutegemea misaada
kutoka nje.
Kauli hiyo ilitolewa hivi
karibuni na Katibu Mtendaji wa Idara ya Liturujia katika Baraza la Maaskofu
Katoliki
Mosinyori Kangalawe alisema
vongozi wakishirkiana na walei katika kuweka mikakati ya kupata pesa,mashirika
hayo yataweza kujitegemea badala ya kuwa tegemezi kwa Mataifa mengine hususani
yale ya Magharibi.
Mbali na hayo,Monsinyori
Kangalawe aliwataka viongozi wa dini watambue kuwa wao ni chachu katika
kuhamasisha na kuendeleza uinjilishaji wa Neno la Mungu.
“Viongozi wajitambue kuwa wao wanapaswa kuwa mstari wa
mbele ili Uinjilishaji uweze kukomaa na
kuingia ndani kwa kila mtu, awe mtoto ama
mkubwa”alisema Monsinyori Kangalawe.
Naye Mkurugenzi wa Mashirika
ya Kipapa Taifa, Padre Liberatus Mwenda aliwaambia washiriki wa semina hiyo
kuwa waamini wengi wanaona ugumu wa kutoa michango kwa ajili ya ujenzi wa kitu
fulani kwa vile awali walizoeshwa na Wamisionari kufanyiwa kila kitu bure.
“Waamini wengi hawajui maana
ya ‘toa ndugu’ kuwa ina maana gani!
kitendo hiki kinawafanya
washindwe kuchangia kanisa kwa maendeleo zaidi”alisema.
Aliongeza “Wamisionari wa
zamani hawakuwashirikisha waamini wakati wa ujenzi wa makanisa, mahospitali,
shule pamoja na miradi ya maendeleo ya kanisa, kitu ambacho kiliwafanya
kubweteka zaidi na kushindwa kuelewa pesa ilikuwa ikitoka wapi”.
Nao washiriki wa semina hiyo ambao walitoka
katika Majimbo Katoliki ya Dar es
Salaam, Tanga, Morogoro, Mahenge na
BAADA YA KUMALIZA
MGOGORO WA MISHAHARA KATIKA KIWANDA CHA URAFIKI
Wayanyakazi
sasa wadai nyumba za kiwanda ni chafu
Na Anthony Ngonyani
BAADHI ya wafanyakazi
wa Kiwanda cha nguo cha Urafiki kilichopo jijini Dar es Salaam,wanaoishi
kwenye nyumba za Kiwanda hicho,wamedai kuwa nyumba hizo ni chafu.
Madai
hayo yamekuja siku chache baada ya kumalizika kwa mgogoro wa nyongeza ya mishahara baina ya wafanyakazi na uongozi wa
kiwanda hicho.
Wakizungumza
na KIONGOZI kwa nyakati tofauti,wafanyakazi hao walidai kuwa nyumba hizo ambazo
zimejengwa kwa mtindo wa ghorofa,ni chafu na hazijapigwa rangi muda mrefu sasa.
Wafanyakazi
hao ambao walizungumza kwa masharti ya majina yao kutoandikwa gazetini kwa
kuhofia kufukuzwa kazi,walidai kuwa tatizo hilo tayari limekwisha pelekwa kwa
uongozi wa kiwanda,lakini hakuna hatua iliyokwisha chukuliwa.
“Majengo
haya yalipakwa rangi kwenye miaka ya 80,hadi leo yamechakaa sana utadhani
wanakaa wanyama na si binadamu”alisema mmoja wa wafanyakazi hao.
Licha
ya uchafu,wafanyakazi hao walidai kuwa nyumba hizo pia zinakabiliwa na tatizo
la ukosefu wa taa hususani katika ngazi za kupandia , ambapo walidai
zilizokuwepo siku za nyuma, kwa sasa zimeharibika.
Walisema
hali hiyo ni hatari katika maisha yao kwani hulazimika kupanda juu kwa shida
wakati wa usiku.
Hivi
karibuni wafanyakazi wa kiwanda hicho waligoma kufanyakazi kwa muda wa siku
moja kwa kile walichodai kuwa wanafanyishwa kazi ngumu na kupewa mshahara
kidogo.
Hata
hivyo mgomo huo ulizimwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Luteni Yusuph Makamba
ambaye aliuita uongozi wa kiwanda hicho
ofisini kwake na kujadiliana na kufikia muafaka wa kuboresha mishahara ya
wafanyakazi hao.