Wakatoliki
Palestina wahofu machafuko Arafat
aking'olewa
BAADHI
ya Wakristo wanahofu kuwa Waislamu wenye itikadi kali wanaweza kuchukua uongozi
iwapo Rais wa Wapalestina Yasser Arafat ataondolewa madarakani.
”Nina hofu kwamba Waislamu
wenye itikadi kali watachukua madaraka, kwa sababu hiyo ninataka Arafat abakie
kuwa Kiongozi wetu,” alisema mwanafunzi mmoja Mkatoliki wa Chuo Kikuu cha
Kikatoliki cha
Naye Kiongozi wa
wafanyabiashara ambaye pia ni Mkatoliki alisema kuwa Wakristo wengi katika eneo
Alisema kuwa wafuasi wa
Arafat hawana ushawishi mkubwa miongoni mwa Wapalestina kama Waislamu wenye
itikadi kali
”Arafat amekuwa sehemu ya
makundi ya watu wa kawaida, na Wakristo wanaogopa pale wanapoona makundi
makubwa ya Kiislamu,” alisema.
Katika Bethlehem, mahali
ambapo Wakristo japo ni wachache wana msingi mkubwa wa kiuchumi, na chama cha
Arafat cha Fatah kina ushawishi mkubwa.
Alisema katika maeneo
mengine
Majeshi ya
Katika uvamizi huo majeshi
ya
Hapo Septemba 24, wanajeshi
wa
Katika uvamizi huo watu
sita walikufa wakiwemo raia watatu wa Palestina na wanamgambo sita wa Hamas.
Naye Meya wa
"Palestina bila Arafat
haifikiriki,” alisema
Pia alielezea mashaka yake
juu ya hali ya sasa na kusema kwamba mambo yakiendelea hivi itakuwa vigumu
kufanya uchaguzi wa Palestina mwezi Januari
Hata hivyo, Bernard
Sabella, profesa wa elimu jamii katika Chuo Kikuu cha
"Arafat amekuwa mwema
hasa kwa uhusiano kati ya Waislamu na Wakristo, lakini nadhani pia kuwa kuna
busara ya kutosha katika viongozi wa Kipalestina wa kisiasa, kijamii na
kiuchumi katika jamii ya Palestina hata kati ya wale wenye msimamo mkali,”
alisema Sabella.
Alisema Wakristo wanapaswa
kuondokana na mawazo kwamba wao ni wachache na badala yake wajiingize katika
siasa za Palestina na katika ajenda ya kijamii. Alisema wakati kuna Wakristo ambao
tayari wamejihusisha katika mdahalo wa kisiasa kuna wengine wanajisikia
Katika Bethlehem hapo
Septemba 23, Chama cha Fatah cha Arafat na Chama cha Kiislamu cha Kitaifa
viliandaa maandamano ya pamoja mbele ya Kanisa la Nativity, huku wanafunzi wa
chuo kikuu wakiimba nyimbo za kumuunga mkono Arafat.
"Tupo hapa kuonyesha
uungaji wetu mkono kwa Arafat,” alisema Haneen Abu Sauda, 18,mwanafunzi wa
biashara katika Chuo Kikuu cha
"Yuko katika hali
ngumu sasa hivi na tunataka kumwonyesha kwamba tuko naye. Siwezi kufikiria
Palestina bila yeye. Sidhani kitakachotokea bila yeye. Sitaki kuona mauaji
mengi zaidi,”alisema dada huyo.
Rafiki yake, Tamara
Rishmawi, (18), wa Kanisa la Kiorthodoksi la Ugiriki ambaye pia ni mwanafunzi
wa biashara katika Chuo Kikuu hicho, alisema kwamba ilikuwa muhimu kwa
Wapalestina kuonyesha uungaji mkono wao kwa Arafat kwa sababu ya matendo mema
aliyofanya kiongozi huyo kwa watu wake siku zilizopita.
Karismatiki walenga Uamsho wa Ulaya
MKUTANO wa Karismatiki uliomalizika hivi karibuni
ulilenga pamoja na mambo mengine kuchunguza “kile ambacho Roho Mtakatifu
aliambia Kanisa la Ulaya.”
Mkutano
wa Viongozi wa Karismatiki Katoliki wa Ulaya kwa ajili ya huduma za kimataifa
ulikuwa na mada kuu: “Ulaya, Tweka Mpaka Klindini” uliishia kwenye sehemu ya
hija huko
Mkutano
huo ulilenga na kujadili kile ambacho Mungu anajaribu kusema kadiri Ulaya
inavyozidi kuendelea kuungana kisiasa na kiuchumi, na “kutambua mpango wa Mungu
na mwito wa Ulaya kuanza upya tena,” taarifa hiyo ilisema.
Mkutano
huo wa kimataifa ulifungwa kwa ibada ya misa takatifu iliyoongozwa na Mhashamu
Askofu Mkuu Stanislaw Nowak wa jimbo kuu la
Washiriki
wa mkutano huo walifanya hija huko
Habari
zaidi juu ya Uamsho wa Karismatiki Katoliki Kimataifa zinapatikana kwenye
tovuti (mtandao wa kompyuta) ambayo ni: www.iccrs.org.
Rozari ni silaha ya amani – Papa
VATICAN CITY
Siku ya Septemba 29 baba Mtakatifu alizungumzia
Rozari kama Silaha ya Amani, ifuatayo ni hotuba yake aliyoitoa kabla ya kusali
sala ya Malaika wa Bwana pamoja na waamini na mahujaji kwenye makazi yake ya
majira ya kiangazi ya Castel Gandolfo.
Wapendwa Kaka na Dada!
Tayari tuko kwenye mlango wa mwezi wa Oktoba, ambao huwa
na Kumbukumbu ya kiliturujia ya Bikira Maria wa Rozari Takatifu, mwezi huu
unatusukuma kugundua tena mapokeo haya ya sala, ambayo ni rahisi lakini ya
kina.
Rozari ni mwono wa kitaamuli wa sura ya Kristo, tunaweza kusema
unaofanyika, kupitia macho ya Maria. Kwa hiyo, ni sala ambayo iko moyoni mwa
Injili na iko katika amani kamili na wazo la Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vaticano
na sana katika kueneda sambamba na yale niliyoonesha katika barua yangu ya
kitume, “Novo Millennio Ineunte”: (Tuingie Milenia Mpya). Ni lazima
kwamba Kanisa “litweke hadi Kilindini” mwa milenia mpya tukianzia na taamuli
(tafakuri) kuhusu sura ya Kristo.
Kwa hiyo, ningependa kupendekeza kwa watu mmojammoja, familia na kwa
Jumuiya Ndogondogo za Kikristo. Kulipa umuhimu ombi hili. Pia naandaa waraka
ambao utawasaidia kugundua tena uzuri na undani wa sala hii.
Ningependa kukabidhi kwa mara nyingine tena njia kuu za amani kwa sala ya
rozari. Tunakabiliwa na hali ya kimataifa iliyojaa mivutano, na sura za mapigano.
Katika baadhi ya sehemu za ulimwengu, ambapo makabiliano ni ya nguvu sana –
hapa ninafikiria hasa Nchi Takatifu ya Kristo – tunaweza kuona ubora wa njia
hiyo ya Rozali. ingawa ni za
muhimu juhudi za kisiasa zinafaa kidogo iwapo roho zinabakia katika hali mbaya
na hakuna uwezekano wa kuonyesha nia ya moyo kuamsha tena njia ya mazungumzo.
Lakini, ni nani anaweza
kutuingizia hisia za namna hiyo
Ninafikiria mataifa, lakini
pia familia: ni amani kiasi gani ingehakikishwa katika uhusiano wa kifamilia,
iwapo rozari takatifu ingesaliwa na familia!
[Baba Mtakatifu aliwasalimu
mahujaji katika lugha saba za Kifaranza, Kiingereza, Kijerumani, Kihispania,
Kireno, Kipolandi na Kiitaliano. Katika Kiingereza alisema:]
"Ninawasalimu
[Mwishoni kwa Kiitaliano,
Papa alisema:]
Sala ambayo tunakaribia
kuisali, inaanza kwa kukumbuka tangazo la Malaika Mkuu Gabriel kwa Bikira
Maria. Kwa kweli, leo ni sherehe ya malaika wakuu Mikael, Gabriel na Raphael:
Ninaomba wahudumu hawa wakuu wa Mungu watusaidie kupelekeana daima upendo
mkarimu kwa mapenzi yake.
Itakuwa vigumu kuhalalisha
shambulizi dhidi ya
WASHINGTON, D.C., Marekani
AKISISISTIZA
tena msimamo wa wa Baraza la Maaskofu Katoliki wa Marekani, Askofu Mkuu wa
Washington, Kardinali Theodore McCarrick aliwashauri watunga sheria kuepuka vita
na Iraq isipokuwa uhai wa Marekani kama umo katika hatari ya mara moja.
“Sasa
hivi tungesema vita ya kujilinda iwapo hali fulani ingeruhusu,” alisema Askofu
huyo Mkuu wa Washington wakati akiongea na radio ya WTOP, kwa mujibu wa gazeti
la Catholic Standard.
“Unapoiangalia
Iraq, ninahisi iwapo Rais angekuwa na habari za aina hiyo kwamba tupo katika
hatari ya kweli mara moja, kutoka Iraq hapo tungeweza kuwa na kesi,” alisema
kardinali.
“Sidhani
kama maaskofu wanahisi kesi ya namna hiyo imeishafanywa,” aliongeza “Ndiyo
maana tunasema tafadhali nenda taratibu, tafadhali jaribu kuona kwa hakika
jinsi hali ilivyo kabla ya kufanya jambo fulani ambalo tungesema lisingekuwa la
maadili.”
Askofu
huyo mkuu alikuwa katika kipindi maalumu cha “Muulize Kardinali” ambapo maswali
mengi yalijikita juu ya Iraq, kashfa za ngono kwa maklero, utafiti juu ya seli
shina za viinitete na uhaba wa mapadre.
Kardinali
huyo alisema kuwa hata katika vita ya kujilinda, nchi husika inapaswa kufuata
sheria za ulinganifu wa njia zitakazotumika na kuepuka madhara kwa raia wema.
Aliongeza kuwa shambulizi la kwanza dhidi ya Iraq litakuwa vigumu sana kulihalalisha, bila kuwepo ushahidi wa wazi juu ya kuwepo kwa silaha za kibayolojia nchini humo.
“Nadhani kile maaskofu wanachotumaini
ni kwamba kadiri Rais na Bunge la Congress wanavyozungumzia jambo hili,
tunaweza kuwa na fursa ya kupima tunu za kimaadili, kitu ambacho watakifikiria
pia,” alisema Kardinali McCarrick.
It is prepared by Miss. Christina Nyambo. Authorised
and run by Rev.
Fr. Revocatus Makonge, Exec. Sec. of
the Communications Department of TEC.
Please visit the TANZANIA
EPISCOPAL CONFERENCE WEB SITE