Papa
aongeza matendo katika Rozari
l Atangaza Mwaka wa Rozari kwa
ajili ya familia na Amani
l Sasa itakuwa na mafumbo 20
BABA Mtakatifu Yohane Paulo wa
Pili, ameadhimisha mwaka wa 24 wa
upapa wake kwa kutangaza mwaka wa
Rozari, kuchapisha barua ya kitume kuhusu sala ya Rozari ya Bikira Maria na
kupendekeza ‘mafumbo ya nuru’ kuongezwa kwenye sala hiyo.
Papa alitia saini waraka huo na kuutoa katika moja ya
mikutano yake ya kila juma mbele ya mahujaji 17, 000 waliokusanyika kwenye
viwanja vya Kanisa Kuu la Mt. Petro, huko
alitumia wasaa huo kusisitiza tena
nia yake ya kuendelea kuwa Papa kadiri ya mapenzi ya Mungu ambapo alikabidhi
mikononi mwa Maria ‘uhai wa Kanisa na ubinadamu unaojaribiwa.’
“Kwake nakabidhi maisha yangu ya baadaye. Naweka kila kitu
mikononi mwake ili kwa upendo wa kimama, aendelee kuyapeleka kwa Mwanae”,
aliongeza.
Katika barua hiyo ya kitume inayoitwa Rosarium Virginis
Mariae (Rozari ya Bikira Maria), Papa anatoa Sala ya Maria kama ‘tafakari
juu ya mafumbo ya maisha na kazi ya Kristo iwapo itasaliwa ‘kwa uchaji na si
kwa midomo tu.
“Kwa kurudia mwito wa
Salamu Maria tunaweza kuakisi kikamilifu juu ya matukio muhimu ya Utume wa
Mwana wa Mungu duniani ambao umeletwa kwetu na Injili pamoja na Mapokeo,”
alieleza Papa.
Na kwa kuwa katika mafumbo 15 ambayo bado yanasaliwa hadi leo
matukio makubwa ya maisha ya Kristo hadharani hayakutafakariwa, katika barua
mpya ya kitume Papa anaongeza mafumbo matano anayoyaita ‘Mafumbo ya nuru’,
yanajumuisha maisha ya hadharani ya Kristo tangu ubatizo wake katika mto
Yordani yakihitimishwa na mateso yake.
Katika Sehemu ya Pili
ya Barua hiyo, Papa anatangaza ‘Mwaka wa Rozari’ kuanzia mwezi huu wa
Oktoba2002, hadi Oktoba 2003.
Baba Mtakatifu alielezea kuwa tangazo hilo la mwaka huu
linaadhimisha matukio matatu muhimu ambayo ni mwanzo wa mwaka wa 25 wa Upapa
wake, mwaka wa 120 wa Barua ya Baba Mtakatifu Leo wa Kumi na Tatu inayoitwa Supremi
Apostolatus Officio, iliyoanzisha mfululizo wa nyaraka juu ya Rozari,
na pia kufunga Mwaka Mtakatifu wa 2000.
Alisema katika historia ya Jubilei Kuu, desturi ilikuwa
kwamba baada ya mwaka wa Jubilei uliotolewa kwa Kristo na kwa kazi ya ukombozi
mwaka mmoja baada ya hapo, ulitangazwa ili kumuenzi Maria kama ishara ya kuomba
msaada wake ili kuzaa matunda kwa njia ya neema zilizopokelewa katika Jubilei.
Katika kuelezea uamuzi wake wa kuongeza mafumbo matano ya
nuru katika rozari ya sasa, Papa alisema kuwa Rozari ya Bikira Maria ni
Mpaka sasa mafumbo 15 ya Rozari yaani ya Furaha, ya Uchungu
na ya Utukufu yamekosa nyakati mahususi katika maisha ya Kristo hadharani,
alieleza Baba Mtakatifu.
Kwa sababu hiyo, Papa anapendekeza kuingiza “mafumbo ya
huduma ya Kristo ya hadharani kati ya Ubatizo wake na mateso yake.”
Alisema anamuacha huru mtu mmojammoja, au na jumuiya zao
kuamua juu ya
Papa alieleza kwamba, anayaita mafumbo haya “Mafumbo ya Nuru”
kwa sababu Kristo katika maisha yake ya hadharani alijionesha
Katika Kifungu cha 21 cha barua hiyo,Baba Mtakatifu anatilia
mkazo Mafumbo ya Nuru yake matano ya maisha ya hadharani ya Yesu na kufafanua
fumbo ambalo Mkristo hutafakari katika kila Kifungu cha matini yafuatayo:
Ubatizo wa Yesu, Kujidhihirisha kwake katika Harusi ya Kana, Utangazaji wake wa
Ufalme wa Mungu, pamoja na mwito wake kwa uongofu, Kugeuka kwake sura, na
Kuweka Sakramenti ya Ekaristi kama kielelezo cha Fumbo la Pasaka.
“Ubatizo katika Yordani kwanza kabisa ni Fumbo la Nuru,” alisema. “Hapa Kristo anaposhuka
majini mtu asiye na hatia aliyefanyika ‘dhambi’ kwa ajili yetu (2Kor
Fumbo jingine la nuru ni ishara ya kwanza iliyotolewa kule
Kana (Yn. 2:1-12) wakati Kristo anapogeuza maji kuwa divai na
kuwafungua wafuasi wake mioyo
Fumbo jingine linahusu mahubiri ya Kristo wakati anapotangaza
kuja kwa Ufalme wa Mungu na kutoa wito kwa watu ili waongoke (Rej. Mk 2: 13,
Lk 7: 42-48) na anasamehe dhambi wote wanaomwendea Kristo kwa tumaini
nyenyekevHuduma hiyo inaendelea katika
Sakramenti ya Upatanaisho ambayo ililikabidhi Kanisa.(Rej. Yh.20: 22-23).
Fumbo la nne ni “fumbo la nuru hasa” ambalo ni Kugeuka sura
kwa Yesu tendo ambalo linatoa wito na mafundisho mengi na ya kufaa kwa Mkristo.
Fumbo la mwisho ni kuwekwa kwa Sakramenti ya Ekaristi
Takatifu ambamo Kristo anatoa mwili na damu yake kama chakula katika maumbo ya
mkate na divai na kushuhudia fumbo hilo ‘mpaka mwisho’ kwa sababu ya upendo
wake kwa wanadamu ambao kwa ajili ya wokovu wao atajitoa kuwa sadaka (Yn
13:1).
Kwa mujibu wa barua hiyo, Papa anapendekeza kuwa mafumbo hayo
ya Nuru yasaliwe siku ya Alhamisi ambapo mafumbo ya Furaha
yatasaliwa siku za Jumatatu na Jumamosi, mafumbo ya Uchungu yatasaliwa
Jumanne na Ijumaa na mafumbo ya Utukufu yatasaliwa siku ya Jumatano na
Jumapili.
Maaskofu
Ufaransa wapinga vita ya Iraq
PARIS,
Ufaransa
KAMPENI ya
Marekani na mshirika wake mkuu Uingereza kutaka kuishambulia kijeshi
Msimamo huo wa maaskofu dhidi ya kile ambacho
kinapingwa na watu wengi duniani ulitolewa katika tamko lao lililotolewa juma
lililopita.
“Mazingira ya vurugu ambamo mashambulizi ya
kijeshi katika sehemu mbalimbali za dunia hututumbukiza yanatuelekeza kurudia
na kusisitiza tena kwamba heshima ya kila uhai wa binadamu ni sharti la amani
ya kweli,” lilisema tamko
Miongoni mwa wale waliotia saini tamko
Pia yumo Askofu Mkuu wa jimbo kuu la
“Mkabala na
uwezekano wa operesheni ya kijeshi inayopigiwa upatu na Marekani dhidi ya Iraq,
ni sehemu ya utume wetu kukumbusha kwamba kutanzua tofauti miongoni mwa
mataifa, vita haiwezi kuchukuliwa kama njia miongoni mwa nyingine zinazoweza
kuchaguliwa kufuatana na kufikiria maslahi au fursa,” maaskofu hao wa Ufaransa
walieleza.
“Kwa Mkataba wa
Umoja wa Mataifa pamoja na maadili ya Kikatoliki, kuchagua matumizi ya silaha,
hata kama hatua hiyo ina lengo linalopendelewa na kwa ajili ya maslahi ya
pamoja, unahusisha uamuzi mkubwa vile kwamba huwezi kukimbilia njia ya vita
isipokuwa katika hali isiyoepukika na pale tu endapo masharti magumu kadhaa
yatakuwa yametimizwa, “ liliongeza tamko hilola maaskofu.
“Kwa sasa, taarifa
zilizopo haziwezi kuruhusu uhalalishaji wa kwamba masharti kama yalivyofupishwa
katika Katekisimu ya Kanisa Katoliki (Na. 2309) yametimizwa. Tunashiriki maoni
ya namna hii na ya baraza la maaskofu ambayo wameyaeleza juu ya suala hili
pamoja na mwangalizi wa Vatican katika Umoja wa Mataifa,” walisisitiza maaskofu
hao.
“Hivi utawala wa
Iraq, pamoja na kwamba unalaaniwa kwa ukiakaji wake wa haki za watu katika Iraq
na kwa sheria ya kimataifa, unahusisha kitisho cha haraka na cha mara moja,
jambo ambalo linaweza kuwa kesi halali ya ulinzi? “ walihoji. Na kuongeza
“iwapo utawala huo una kitisho cha kweli, haipasi njia zote kutumika kwanza
badala ya kukimbilia njia za kijeshi kuuondoa? “
“Matokeo
ya ‘hatua hii ya bila kurudi nyuma’ ambayo ni hoja kuhusu kila vita, ni
usumbufu kwa maoni ya umma,” waliendele kusema maaskofu hao.
“Mkabiliano kati ya taifa la Kiarabu na
Marekani utaimarisha hoja ya itikadi ya Uislamu wa siasa kali kuibua uhasama wa
makundi yasiyolindwa na yasiyoharifiwa dhidi ya ‘Magharibi’ walisema.
“Vita itapanua pengo ambalo tayari limechimbwa
kati ya watu wetu na watu wa Ukanda wa Mashariki ya Kati, ambapo, zaidi ya hayo
tunaweza kutaja kaka zetu wengi katika Kristo, pengo ambalo linasababisha hisia
kali kwamba mataifa makubwa ‘hutumia vipimo viwili tofauti’ katika kutekeleza
maazimio ya Umoja wa Mataifa,” walilalama Maaskofu hao wa Kifaransa.
“Sasa hivi zaidi ya wakati mwingine wowote,
haki ni msingi na sharti la amani,” lilihitimisha tamko
Waganda
wawili, Wamisionari wanne watangazwa wenye heri
l Asema utakatifu ndiyo ushuhuda bora wa kutangaza Injili
BABA Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili aliadhimisha Jumapili ya Missioni
Ulimwenguni kwa kuwatangaza wenyeheri vijana makatekista wawili kutoka
Katika ibada
hiyo iliyofanyika kwenye viwanja vya Kanisa la Mt. Petro papa aliwasifu
wamisionari wake kwa waume kwa kujitoa bila ubinafsi ili kutangaza Injili.
“Niko nanyi
kila siku,” alisema Baba Mtakatifu. “Niko pamoja na wewe. Yesu analimbia kanisa
lililoko safarini ulimwenguni. Niko pamoja nanyi, jumuiya ndogo za kikanisa
katika nchi za misioni. Msiogope kujihusha katika mazungumzo na watu wote.
Peleka ujumbe wa wokovu kwa kila mmoja. Muwe wajasiri!”
baba Mtakatifu alisema kuwa huu ulikuwa
ni ushuhuda ulioachwa na Daudi Okelo pamoja na Jildo Irwa, makatekista wa
Picha za vijana
hao wa Kiganda zilitundikwa katika ya sehemu ya mbele ya Kanisa la Mt. Petro,
mara baada ya Papa kutamka kanuni kuu ya uenye heri.
“Wanatolewa kwa
jumuiya nzima ya Kikristo kama mfano wa utakatifu na fadhila, na kama vielelezo
na waombezi kwa makatekista ulimwenguni kote, na hasa wale walio katika sehemu
zile ambapo makatekista bado wanateseka kwa sababu ya imani yao, na wakati
mwingine kukabiliwa na kutengwa kijamii na hata hatari kubwa,” alisema papa
katika mahubiri yake.
Aidha Baba
Mtakatifu aliuelezea mfano wa makatekista hao kama unaoweza kuvuvia maisha ya
“wanaume na wanawake wengi – katika Uganda, katika Afrika, na mahali popote –
kujibu kwa ukarimu wito wa kuwa katekista, kwa kuleta maarifa juu ya Kristo kwa
wengine na kuimarisha imani ya jumuiya zile ambazo ni hivi karibuni tu
zimepokea Injili ya wokovu.”
Wakati wa misa
ya kuwatangaza wenyeheri makatekista hao, nyimbo za utamaduni wa Kiafrika
ziliimbwa na ujumbe mkubwa wa kutoka Uganda uliohudhuria misa hiyo ukiongozwa
na Makamu wa Rais wa Uganda, Dk. Speciosa Wandira Kazibwe, ambapo Waafrika wengi
walivalia nguo zao za kijadi.
Wakati wa misa
hiyo pia kulikuwa na nyimbo katika lugha ya ki-Tamil, ili kumkumbuka mwingine
wa waliotangazwa kuwa wenyeheri, Mary wa Mateso.
Mwenyeheri huyo
aliyezaliwa(1839-1904) katika Ufaransa
Hélčne Marie de Chappotin de Neuville , alianzisha Shirika la kitawa la
Wamisionari wa Maria katika India, mwaka 1874. Leo shirika hilo lina watawa
8,000 katika nchi 77.
Pia katika misa
hiyo Baba Mtakatifu alimtangaza kuwa mwenyeheri Mwitaliano Liduina Maneguzzi
(1901-1941), mhubiri wa Injili katika Ethiopia, ambaye alikuwa mtawa wa kwanza
katika Shirika la Masista wa Mt. Francis de Sales. Kazi yake ya umisionari
ilifupishwa katika umri wa miaka 40 kwa ugonjwa wa kansa.
Mmoja wa wale
waliohudhuria misa hiyo, Mwitaliano Giacomo Colombo, 52, alikuwa miongoni mwa
wale waliohudhuria sherehe za uenyeheri. Colombo aliponywa katika mwaka 1976
kutokana na majeruhi ya ajali mbaya ya gari baada ya familia yake kumwombea
apone kupitia maombezi ya Liduina.
Watumishi wa
Mungu wengine wawili waliotangazwa kuwa wenyeheri ni Waitaliano Andrea Giacinto
Longhin (1863-1936) aliyekuwa mtawa wa Kikapuchin na kwa miaka 32 kama Askofu
wa Treviso, ambapo alikuwa mfano kwa kuishi umaskini na kwa unyenyekevu.
Alikuwa akijulikana kama “askofu wa kanisa.”
Mwingine ni
Mwitaliano Marcantonio Durando (1801-1880), padre wa Shirika la Kitume ambaye
pia alikuwa mwanzilishi wa Shirika la Masista wa Nazarene. Kama Mt. Vincent wa
Paulo, “alijua namna ya kutambua katika ubinadamu wa Kristo kielelezo kikubwa
cha upendo wa Mungu kwa kila mtu,” alisema Baba Mtakatifu.
Kutangazwa
wenyeheri kwa Wakristo hawa sita “kunatukumbusha kuwa huduma ya kwanza ambayo
tunapaswa kutoa kwa utume ni utafutaji wa kweli na endelevu wa utakatifu,”
alisisitiza Baba Mtakatifu. “Hatuwezi kutoa ushuhuda kwa Injili kikamilifu kama
hatuiishi kwanza kiaminifu.”
Mwishoni mwa
sherehe hizo, kabla ya kusali sala ya Malaika wa Bwana, Papa aliwasifu
“wamisionari wake kwa waume – mapadre, watawa wa kike na kiume, pamoja na walei
– waliotumia nguvu zao katika utumishi wa mstari wa mbele kwa Kristo, na kwa
nyakati nyingine hata kutoa ushuhuda kwa damu yao.”
Kwa mujibu wa
Shirika la Vatican la Uinjilishaji wa Watu, mwaka jana tu wamisionari
Wakatoliki 33 waliuawa katika Asia, Afrika na Amerika ya Kusini wakati
wakihubiri Injili.
Habari zaidi
kutoka Vatican zinasema kuwa, hadi sasa Baba Mtakatifu yohane Paulo wa Pili
ametangaza wenyeheri 1,303 katika miaka 24 ya upapa wake.