Majonzi
yaligubika Baraza la Maaskofu
q
Lapoteza
'nyota' ya matumaini
Na
Mwandishi Wetu
JUMANNE asubuhi, kila
mmoja katika Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), alionekana mwenye
baridi, amejikunyata, hali yake si nzuri na wala si mbaya. Hakuna mgonjwa.
Lakini, nini kimewasibu wasinyae na kugubikwa na majonzi huku wakionekana
upweke namna hiyo?
Katika hali isiyo ya kawaida, mchana wa
siku hiyo simu kutoka ofisi ya Katibu
Mkuu wa TEC, zinapigwa katika ofisi mbalimbali ya Baraza hili zikimtaka kila mfanyakazi
aende kanisani.
Bila kujua hili wala lile, wafanyakazi
wote walielekea kanisani, si wafanyakazi peke yao bali hata watu kutoka majimbo
mbalimbali ya Kanisa Katoliki ambao walikuwa wanashiriki Mkutano wa Idara ya
Uchungaji, nao pia waliunganika.
Kila mmoja akiwa ametulia kanisani humo,
Katibu Mkuu wa TEC, Padre Pius Rutechura, akainuka na kutaka kusema kitu
lakini, kabla hajafanya hivyo, akakumbwa na kigugumizi asichokuwa nacho siku
zote.
Uso wa Padre Rutechura ambao siku zote
huwa ni wenye furaha na matumaini awapo mbele ya wanaTEC wenzake, siku hiyo
ukaonekana kinyume kabisa.
Kila mtu akawa na hamu ya kupata ujumbe
kutoka kwa Padre Rutechura, ili ajue amekumbwa na masaibu gani.
Akasema kuwa, kipenzi cha wengi, Padre
mcheshi, Padre mwenye huruma, Padre asiye mbinafsi, Padre mkarimu kwa watu
wote, Padre mtaalamu wa mambo mengi yakiwamo mawasiliano na mambo muhimu ya
kiroho, NORBERT KIJA, sasa eti ni MAREHEMU. Eti amefariki dunia. Huzuni na
majonzi tupu.
Ni nani anayemfahamu Padre Kija ambaye
hakulengwalengwa na machozi baada ya taarifa hiyo iliyotolewa katika kanisa la
TEC?
Kisha, Katibu wa Idara ya Liturjia wa
TEC, Padre Julian Kangalawe, akaongoza sala kumuombea Marehemu kipenzi cha
watu, Padre Kija.
"Mungu akulaze Mahali Pema Father
Kija. Lakini Father, tutakuona lini katika dunia hii? Huzuni tupu, majonzi na
upweke.
Gazeti la KIONGOZI, Idara ya Mawasiliano,
TEC, Tanzania na Kanisa kwa jumla, wanaamini kuwa ingawa kimwili umewatoka,
lakini kiroho uko pamoja nao na wana matumaini mtakutana katika Ufalme wa Mungu
kwa kuwa maombi yao kwako ni makubwa, vilio vyao ni vingi na hasahasa wanakiri
kuwa ulimtumikia vema Mwenyezi Mungu.
Hivi ni nani hakumjua alivyo kuwa na
utani kwa watu wengi? Ukiwa nae unajisikia umekaa pamoja na baba yako, umekaa
na ndugu katika Yesu na hasahasa umekaa na Mkristo mwenzako?
Jumatano katika ibaada maalumu ya
kumuombea kanisani hapo, kwa huzuni kabisa Padre Lucas Mzuanda akasema kuwa ni
wazi hakuna ajuae kifo kitampata wapi na hivyo kila mmoja ajiandae wakati
wowote kuingia mbinguni huku akiishi maisha mema na kudumu katika sala.
Kifo cha Padre Norbert Kija, aliyekuwa
Katibu Mtendaji wa Idara ya Mawasiliano wa TEC, na Mkurugenzi Mtendaji wa
gazeti hili la KIONGOZI, kimetokea Septemba 19, mwaka huu baada ya kuugua akiwa
jimboni kwake Shinyanga.