Miujiza
Kisiwani (3)
Na Peter Dominic
Siri hiyo iligundulika baada ya wazazi wa binti huyo kumtaka
anywe dawa ili aiharibu mimba hiyo aepukane na adhabu ya kifo ambacho
kingeliwaandama yeye na binamu yake baada ya kuvunja sheria.
Hata hivyo
kwa mshangao wa wazazi wake binti huyo aliwakatalia katakata na aliahidi kuwa
angaliweza kuilea mimba. Kinyume chake yupo tayari kupoteza maisha kuliko
kuitoa mimba hiyo.
Walikuwa
wamekubaliana na binamu yake kwamba kuliko kuitoa mimba basi bora wakabilianane
na adhabu ya kupigwa mawe. Labda waliamua kupeana ahadi hiyo kwa vile walikuwa
wadogo kiumri.
Ndiyo
kwanzahuyo binti alikuwa akiitwa Nyamwiza alikuwa na umri wa miaka 15 na
mwenzake alikuwa na umri wa miaka 17. Ni wazi kuwa adhabu ya kifo iliyoambatana
na kupigwa mawe walikuwa wakiisikia kwa hadithi.
Awali
wakati wazazi wa Nyamwiza wakimueleza yote katika nyumba yao ya msonge, ingawa
ilikuwa usiku walikuwa wamekosea maana pembezoni mwa nyumba yao alikuwapo mpelelezi
wa Mfalme akipeleleza kila kitu hivyo taarifa zilimfikia Mfalme siku ya pili
yake.
Nyamwiza
alikuwa mwepesi kutumwa na alikuwa makini tangu utotoni ndiyo maana alitokea
kupendwa sana na wazazi wake.
Aliaminiwa
na aliachwa huru kufanya mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuruhusiwa kwenda
kuteka maji peke yake na kuwatembelea majirani.
Lakini
wakati yeye yuko hivi ilikuwa ni tofauti sana na binamu yake aliyekuja kumpa
mimba ya aibu. Binamu yake Mugalula ni kujana ambaye alionekana kutokuwa
natabia njema tangu kukua kwake.
Wazazi
wake walijaribu kumuonya juu ya vitendo vyake lakini ilikuwa vigumu kubadilika.
Ni siku
moja Nyamwiza alipokwenda kuteka maji umbali wa mita mia mbili kutoka nyumbani
kwao. Hatua kidogo kabla ya kuufikia mto ule uliohudumia watu wa eneo hilo kwa
maji,alijikuta mikononi mwa binamu yake ambaye alimbaka akamsababishia maumivu
makali na kumuachia ujauzito.
Hata hivyo
kutokana na ujasiri wa binti huyo pamoja na maumivu aliyoyapata hakuwahi
kuwaeleza wazazi wake kilichopata hadi ilipogundulika kuwa tayari anao ujauzito
wa miezi mitatu na wiki tatu.
Tabia yake
ilibadilika ghafla, siku moja jioni bibi yake mzaa Baba alipomuhoji na kukagua
tumbo lake kwa viganja vyake vilivyozeeka, alimkagua karibu kila sehemu ya
mwili wake ndipo alipobaini kuwa alikuwa na ujauzito.
Nyamwiza
pia limweleza ukweli wa mambo bibi yake na kumuomba amfichie siri lakini bibi
yake alimweleza kuwa anaweza kuficha vingine lakini siyo mimba.
Nyamwiza
hakuelewa namna nyingine ya kuficha siri yake ilibidi kuwaeleza kila kitu
kilichomkuta.
Inagwa
ilikuwa mwiko mzazi kumshauri binti yakle kufanya jaribio la kuharibu mimba
lakini mapenzi ya wazazi wake, walimshauri anywe dawa za kuiharibu mimba ili
anusurike kifo cha kupigwa mawe.
Nyamwiza
alikubali mbele ya wazazi wake. Bibi yake akishirikiana na mama yake
walitayarisha dawa za kumpatia ili
aanze kuzitumia usiku ya pili
lakini
mchana wa siku ile aliruhusiwa kwenda kisimani ali apate kuoga na kufua nguo
zake.
Akiwa
kiimani alikutana na binamu yake aliyekuwa akitumikia adhabu kali ya kuchota
maji na kujaza mitungi kadhaaa kutokana na kitendo chake cha kumpachika mimba
binamu yake.
Kinyume na
matarajio yake binamu yake alipiga magoti na kumuomba msamaha huku machozi
yakimtiririka.
Nyamwiza ambaye alisimama na kumuangalia asijue la
kumfanya alimshika mkono na kumuinua. “Mimi nimekusamahe, lakini ni vipi
tutakavyopigwa mawe hadi kufa!” alisema na kuanza kububujikwa na machozi.
“Mimi
nimesabababisha haya yote, sina budi kukutetea na kufanya kila linalowezekana
ili ikibidi basi tunusuru maisha ya mtoto aliyepo tumboni.” binamu yake alimpa
moyo.
“Nimesikia
Liwali mmoja akimweleza Mfalme kuwa katika ukoo wenu kuna watu waliopeana
mimba! Mfalme aliamulu uchunguzi wa kina ufanyike ikibidi wahusika wafikishwe
kwake kukabiliana na adhabu ya kifo.” Ni kauli iliyoka kwa kijakazi wa Mfalme
pindi alipokutana na Nyamwiza.
Baada ya
kusema hivyo Nyamwiza na binamu yake wote waliuliza kwa hamaki “ ni kweli wewe
dada?”
Kisha yeye
aliendelea kusema. “Ni kweli, hivi ni nani huko kwenu?
Lakini
nimesikia wanasema ni binti mdogo na kijana mdogo au ni ninyi!?, aliuliza kwa
mshangao.
Baada ya
kusema hivyo Nyamwiza aliangua kilio na mwenzake alianza kumbembeleza. “Mimi
nimewaabieni msije mkanisema wataniua.
Naomba msinisema kwenu jamani” aliwaarifu yule mfanyakazi kisha alitoweka
kuelekea alikotumwa.
Binamu
yake Nyamwiza alimbebeleza mwenzake kisha walikaa na kupanga namna ya kufanya
ili kuhepukana na kifo cha kupigwa mawe ama adhabu ya kukatwa kichwa.
Wote kwa
pamoja waliafikiana watoroke kabla habari sahihi hazijamfikia Mfalme. Suala
hilo halikuhitaji kupoteza muda, “Hizi ni habari mbaya kwetu tukiendelea kukaa
hapa, tutapoteza maisha tutoroke tuelekee Mashariki. Nadhani tutaweza kufikia
vijiji vingine ambavyo watu wanaishi, nadhani watatupokea” alisema binamu yake
Nyamwiza.
“Lakini
itakuwaje tukifika huko!…ina maana watatatupokea na wakitupokea tutawaambije?
sisi ni nani?… Wewe ni nani wangu na
huu ujauzito nilionao je?” aliuliza Nyamwiza.
Mwenzake
alimpa matumaini kuwa hilo lisingelikuwa tatizo. Waliafikiana na kutokomea
msituni kuelekea Mashariki ya mbali.
Nyumbani
kwa akina Nyamwiza na kwa binamu yake mambo hayakuwa shwari.
Wapelelezi wa Mfalme waliwasili muda mfupi ili waweze kuwakamata Nyamwiza na
binamu yake wafikishwe mbele ya Baraza kujibu tuhuma za kupeana mimba kabla ya
kufunga ndoa na ikithibitika basi wakabiliwe na adhabu ya kupigwa mawe hadi
kufa au kukatwa vichwa.
Wazazi wao
ambao walikuwa katika hekaheka za kuwatafuta, walijikuta mikononi mwa nguvu za
dola la Mfalme Kitakwete. Kwakuwa
vijana wao ndiyo hasa watuhumiwa, wao walikamwatwa na kufikishwa mbele ya
Baraza la wazee.
Walihojiwa
kwa masaa kadhaa lakini baadae waliachiwa. Kuachiwa kwao kulitokana na wao
kukataa kuhusika na tuhuma hizo. Waliishinda kesi hiyo kwakuwa hakukuwa na
ushahidi wa yote yaliyosemwa kwakuwa watuhumiwa hawakuwepo mahali hapo.
It is prepared by Miss. Christina Nyambo. Authorised
and run by Rev.
Fr. Revocatus Makonge, Exec. Sec. of
the Communications Department of TEC.
Please visit the TANZANIA
EPISCOPAL CONFERENCE WEB SITE