MICHUANO YA
KOMBE LA MATAIFA AFRIKA:
Taifa
Stars kigugumizi kikubwa kwa Wasudan
l
Na Lilian Timbuka
KIGUGUMIZI
bado kingali kikiwakabili wachezaji na makocha wa Timu ya Taifa kuhusiana na
pambano lao na Timu ya Taifa ya Sudan linalotarajiwa kufanyika nchini hapa
Oktoba 12, mwaka huu jijini Mwanza.
Baadhi
ya wachezaji waliozungumza na Gazeti hili kwa njia ya simu kutoka Mwanza ambako
timu hiyo imeweka kambi tayari kwa pambano
Wachezaji
hao walisema kuwa, maandalizi duni na ukosefu wa mechi kubwa za majaribio, ni
miongoni mwa matatizo makubwa yanayotatanisha klabu na kuifanya ishindwe
kujiamini kuwa itafanya vizuri.
“Mechi
ni ngumu na haitabiriki kabisa labda tusubiri kwani mpira ni dakika 90 kule
ndani ya Uwanja wa Kirumba. Suala la msingi washabiki na Watanzania kwa jumla,
nikukubaliana na matokeo ya mechi hiyo,” alisema Steven Mapunda ambaye pia ni
mchezaji wa Timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam.
Naye mshambuliaji machachari wa Timu ya Soka
ya Yanga ya Dar es Salaam, Edibily Jonath Lunyamila, aliyeongezwa hivi karibuni
katika kikosi cha Timu ya Taifa Stars, alisema ugumu uliopo ni kwamba Taifa
Stars haifahamu mbinu za uchezaji kutoka kwa wapinzni wao.
“Ni vigumu kutabiri au kulizungumzia pambano
Lunyamila alisema mchezo ni mashindano ambayo
yanatakiwa apatikane mshindi na mshindwa, “Tunaenda kushindana, hivyo lazima
awepo mtu atakayetoka akicheka na mwingine akiwa amenuna, kwa kufungwa au
kufunga. Hali hiyo kwa upande wa Watanzania hatuwezi kuitabiri kutokana na
maandalizi tuliyonayo,” alisema Lunyamila.
Mechi
hiyo ambayo ni ya kusaka nafasi ya kushiriki mashindano ya kuwania Kombe la
Mataifa ya Afrika Mwaka 2004, katika michuano itakayofanyika nchini
Naye Dalphina Rubyema anaripoti kuwa; Timu
ya Taifa ya
Akizungumza na KIONGOZi jijini Dar es Salaam
hivi karibuni, Katibu Mkuu wa Chama cha Soka nchini (FAT), Michael Wambura,
alisema kuwa baada ya kuwasili jijini Da es Salaam, Timu hiyo ya Sudan
itaondoka kesho yake kuelekea jijini Mwanza ambapo itaungana na timu ya Taifa
Stars iliyoko Mwanza kwa takribani wiki mbili sasa.
Taifa
Stars iko chini ya Kocha Mkuu, Salum Madadu na Msaidizi wake, Hafidh Badru.
Taifa Stars ambayo bado inakumbuka kipigo cha kutisha kutoka kwa timu ya Taifa
ya
Taifa
Stars katika kundi lake, inaungana na timu za
Mechi hizo zinaendeshwa kwa mtindo wa
ligi na timu inayoongoza katika kundi
Nafasi ya pili inachukuliwa na Timu ya
Wachezaji wa zamani wataka washirikishwe katika
michezo
Na Thadeo Malashala, DSJ
VIONGOZI wa Vyama vya Michezo mbalimbali nchini wameshauriwa kuwashirikisha
wachezaji wa zamani katika kutoa maoni juu ya namna bora ya kuendeleza michezo
hiyo.
Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na Kocha wa zamani wa timu ya Yanga ,
Mkwavi Majimengi, wakati akizungumza na KIONGOZI jijini
Majimengi ambaye pia aliwahi kuichezea timu ya Mkoa wa Dar es Salaam na
Tanga, alisema kuwa, kuwashirikisha wachezaji wa zamani katika masuala
mbalimbali, ni sehemu ya kuwaenzi wachezaji hao na kupata mchango wao katika
kuboresha michezo nchini.
“Mimi ningoeomba Serikali iliweke wazi suala hili
Alizitaja timu hizo kuwa ni Tanzania Legands,
itakayomenyana na Timu ya Ijumaa Sports Club.
Majimengi aliyataja majina ya maveterani
watakaoshiriki mechi hiyo ya kirafika kuwa ni Maulidi Dilunga, Rasuendee,
Maulidi Abedi, Fundi Magota, Lukas Nkondoa, Sunday Juma,
James Kisaka na Rajabu Rashidi.
Wengine
ni Said Mwamba Kizota, Sebastian Nkoma, Mhidin Siso, Yasin Napili, Jumanne
Shengo, Malota Soma, Abubakari Salum,
Juma Mkambi, Makumbi Juma, Omary Hussein na Ramadhani Nkumba.
Serikali yatakiwa
iendeleze soka si kuitelekeza
Na Godwin Kaijage, DSJ
IMEELEZWA kuwa moja ya sababu zinazochangia kufungwa
kwa Timu ya Soka ya Taifa (Taifa Satars,) katika michuano ya Kimataifa,ni
maandalizi hafifu.
Kauli hiyo ilitolewa mwishoni
mwa juma na mchezaji wa zamani wa soka nchini, Omari Pazi wakati akizungumza na
Mwandishi wa habari hizi jijini
Pazi alisema kuwa timu ya
Taifa inapaswa kuandaliwa katika kipindi kirefu kabla ya mashindano na si
vingine kwani kinume na hivyo, ndipo hutokea hatari ya kufungiwa rundo la
magoli.
“Si kama inavyoendeshwa hivi
sasa ambapo timu hupewa maandalizi ya muda mfupi ya wiki mbili tu, hali aliyosema inasababisha jahazi la soka
kuzama,” alisema.
Vile vile, alitoa changamoto
kwa Serikali kulivalia njuga suala la kuunua mchezo wa kambumbu badala ya
kuutelekeza. “Kwanini jamani hata sisi
Aliongeza, “Angalia soka
linalochezwa na wachezaji wa Afrika ya
Alisema hivi sasa kuna vilabu vingi tofauti na zamani ambapo mtu
kupata nafasi ya kuchezea timu fulani, ilitakiwa mchezaji huyo afanye kazi
ngumu kweli kweli, lakini akasema pamoja na wingi wa vilabu hivyo, bado soka
linazidi kushuka kila kukicha.
“Zamani ili upate kuichezea
timu ya Simba ama Yanga, ilibidi ufanye kazi ya ziada tofauti na wakati huu
ambapo timu ni nyigi na viongozi wa soka hutembelea katika viwanja mbalimbali na pale wanapovutiwa na
wachezaji hao huwasajili moja kwa mojakatika timu zao,” alisema.
Pazi katika mchango wa kuleta maendeleo ya soka nchini, alifundisha timu za Mogo na
Black People zilizoko Ukonga jijini Dar
es Salaam.
Matumizi
mabaya ya fedha, chanzo cha wadhamini kutodhamini michezo-Rais Yanga
MATUMIZI
mabaya ya fedha za wadhamini ni moja ya vikwazo vya wadhamini kukwepa udhamini
wa vilabu vya michezo nchini, anaripoti
Lilian Timbuka.
Rais
wa Klabu ya Yanga ya jijini Dar es Salaam, Abbas Tarimba, alisema wakati
akizungumza na Mwandishi wa habari yalipo Makao Makuu ya Yanga, Jangwani jijin
Alisema
imekuwa kawaida kwa viongozi wa vilabu mbalimbali vya michezo na vyama vya
michezo, kutumia vibaya fedha wanazopewa na wafadhili wanaojitokeza kudhamini
michezo.
“Viongozi
waliopo madarakani wanapungukiwa na sifa za kuwa viongozi kwa sababu wanavunja
mikataba ya awali, kwa mfano hivi sasa FAT tayari wamekiuka na tayari
wamekwisha tumia pesa za vilabu kwa ajili ya nauli kwa matumizi mengine ambayo
yako nje ya mkataba na VODACOM,” alisema.
Alisema
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) ambayo awali ilidhamini Ligi Kuu Tanzania Bara,
iliamua kuvunja mkataba huo baada ya FAT kushindwa kutimiza masharti ya mkataba
katika Ligi Kuu mwaka jana ya Hatua ya Sita Bora, ambapo FAT iliongeza timu 8
badala ya sita bila kuwaarifu wadhamini hao.
“FAT
walipewa fedha na wadhamini wa ligi hiyo ambao ni VODACOM kwa mujibu wa
mkataba, lakini wao wamezitumia fedha hizo kinyume,” alisema.
Alisema
katika hali
“Mimi
naungana na Waziri Mkuu kuwa viongozi wetu wana ubinafsi na wanaopenda
kugonganisha vilabu na wadhamini,” alisema Rais huyo ya Yanga.
Hivi karibuni FAT ilikiri kutumia pesa za nauli
za vilabu zilizotolewa na VODACOM kwa matumizi mengine ambayo hayakubainishwa
na Chama hicho, ambapo Katibu Mkuu wa chama hicho, Michael Wambura aliahidi
kuzirejesha pesa hizo kwa vilabu shiriki kabla ya Ligi hiyo kuendelea tena hapo
Oktoba 16.
Kwa hivi sasa Ligi hiyo imesimamishwa
kutokana na kuipa nafasi Timu ya Taifa ambayo inakabiliwa na mechi ya Kimataifa
inayotarajiwa kufanyika Oktoba 12, dhidi ya timu ya Taifa ya Sudan.
It is prepared by Miss. Christina Nyambo. Authorised
and run by Rev.
Fr. Revocatus Makonge, Exec. Sec. of
the Communications Department of TEC.
Please visit the TANZANIA
EPISCOPAL CONFERENCE WEB SITE