KAULI
YETU
SERIKALI: Hivi Sekondari ya Shauritanga kuna nini?
MWISHONI mwa juma, Watanzania walikumbwa na
mshituko mwingine mkubwa baada ya vyombo vya habari kuripoti juu ya ajali ya moto
iliyotokea katika shule ya Sekondari ya Wasichana ya Shauritanga iliyopo Tarafa
ya Mashati, wilayani Rombo katika Mkoa wa Kilimanjaro.
Tukio hilo la Jumatano jioni, liliongeza simanzi
kwa Watanzania na kikubwa zaidi, kwa wanafunzi wa shule hiyo walionusurika kufa
kufuatia mabweni sita kuteketezwa katika ajali hiyo ya moto.
Tukio hili limekuja wakati hata machozi ya
Watanzania yaliyotokana na ajali nyingine kama hiyo iliyotokea katika shule
hiyohiyo mwaka 1994, hayajakauka.
Tunasema hivyo kwani, katika tukio hilo la mwaka
1994, wanafunzi 43 walifariki dunia.
Kwa mtazamo wa haraka, ni wazi kila mtu anaona
kuwa huenda ajali ya 1994, ilikuwa na wingu la utata kwani licha ya Serikali
kuunda tume ya kuchunguza tukio hilo, hadi sasa hakuna taarifa sahihi zilizotolewa
na hii inatia shaka.
Tunasema inatia shaka kwani licha ya miili
iliyogundulika kufa katika mabweni yaliyoteketea kwa moto katika tukio hilo
kuwa 43, bado wanafunzi wa shule hiyo
waliotambuliwa walikuwa 41; wawili hadi sasa bado ni kitendawili.
Tukio la wiki iliyopita lililowafanya wanafunzi
kukosa mahali pa kulala na kupoteza mali zao zikiwamo pesa, na kuwafanya wabaki
na nguo walizokuwa nazo wakati wa tukio walipokuwa katika masomo ya jioni.
Inasikitisha mno.
Tunasema linasikitisha mno kwani hivi sasa
wanafunzi hao wamehifadhiwa katika ukumbi wa mikutano wa shule hiyo
uliozinduliwa hivi karibuni na Rais Benjamin Mkapa huku wakiimba nyimbo za
kumsifu Mwenyezi Mungu kwa kuzinusuru roho zao.
Wanafunzi hao wanakesha na kushinda kwa nyimbo
hizo huku wakiwa wamevaa nguo pekee walizobaki nazo na ambazo ndizo pekee
walizokuwa wamevaa wakati janga hilo linatokea. Hii ni kusema kuwa sasa hawana
nguo hata moja ya kubadili.
Kinachotia wingu la utata katika tukio hilo, ni
taarifa ya Mkuu wa Shule hiyo aliyekaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa
ni vigumu kuamini kuwa tukio hilo limetokana na hitilafu ya umeme.
Mkuu huyo alisema kuwa kasi ya moto iliyokuwapo,
kutokuwapo kwa wanafunzi mabwenini wakati wa tukio, pamoja na mabweni kutokuwa
na swichi hata moja, ni mambo yanayoashiria kuwa tukio hilo sio la kawaida
kwani uwashaji na uzimaji wa taa hudhibitiwa katika ofisi ya mwalimu wa zamu.
Kama hivyo ndivyo, ni vigumu kufikiri kuwa pengine
kulikuwa na mwanafunzi aliyejaribu kufanya utundu wowote na hivyo, kugusa waya
au kusababisha hitilafu yoyote ya kiufundi.
Sisi tunasema, kama hivyo ndivyo, tatizo liko wapi
katika shule hiyo na habari za moto kuunguza mabweni ya Shauritanga, zitakoma
lini kusikika masikioni mwa Watanzania?
Huku tukimshukuru Mungu kwa kutumia nguvu na
mapenzi yake kuwaepusha wanafunzi wote kutoteketea hata mmoja katika moto huo,
tunasema, tunajua upo uwezekano wa Serikali kuunda tume nyingine kuchunguza
ajali hiyo, hatukatai lakini, wingi wa tume za uchunguzi zisizotoa taarifa
sahihi na njia za kukomesha majanga kama hayo, unawasaidije Watanzania?
Tunatoa wito kwa Serikali asasi mbalimbali za kidini, kibinafsi na
watu wote wenye mapenzi mema, kuwapa misaada mbalimbali vijana hao ambao sasa
wanaishi katika mazingira magumu. Kila mmoja ajue kuwa kutoa ni moyo na wala si
utajiri.
Pia, tunatoa wito kwa Serikali kuzingatia usemi
kuwa, dalili ya mvua, ni mawingu. Hii yaweza kuwa ni ishara za mwanzo za janga
kubwa zaidi kutokea katika shule hiyo.
Ni vema uchunguzi wa kina ufanywe ili kubaini
asili ya ajali za moto katika shule hiyo. Uchunguzi ufanywe kuanzia kwa masuala
ya kiufundi na pia, uchunguzi wa kina wa kihistoria ufanywe ili kubaini
uhusiano wa shule hiyo na jamii nyingine tangu siku za nyuma.
Sisi tunasema, tukio hili lisipotoa fundisho
kubwa na kuifanya Serikali kuchambua toka matandu hadi makoko ya ukweli juu ya
shule hiyo, tujue kuwa hii ni rasharasha, masika inakuja.
Serikali ijiulize, kwanini Shauritanga iwe
kisima cha historia ya majanga ya moto katika shule za sekondari?
Hatusemi kuwa juhudi zielekezwe kwa shule hiyo
ya Shauritanga pekee katika kuchukua tahadhari, bali pia Watanzania wazingatie
kuwa mwenzio akinyolewa, wewe tia maji, hivyo shule nyingine zote nchini
zizinduke na kuwa macho zaidi.
Hata hivyo, tumshukuru Mungu kwa kuzinusuru roho
za vijana wetu ingawa bado tunaiuliza Serikali, HIVI SHAURITANGA KUNA NINI?
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
BARUA
FAT msitake kumnenepesha ng'ombe siku ya
mnada
Ndugu Mhariri,
Napenda kujitokeza
katika Gazeti lako, ambalo sasa linaibuka kwa kasi kuingia katika ushindani wa
kibiashara ili nilitumie kutoa maoni yangu.
Timu yetu ya Soka ya Taifa ya
Taifa Stars imepangwa katika kundi la tatu pamoja na
Mchezo wa Taifa Stars na
Katika mchezo huo, Taifa Stars ilifungwa na
Kutokana na kufungwa mabao 4-0, uongozi wa Chama cha Soka nchini (FAT)
ulikutana na Kocha Mkuu Salum Madadi ambaye aliongeza wachezaji kadhaa Taifa
Stars.
Kuna baadhi ya wachezaji ambao walipunguzwa na wengine kuongezwa na
kuifanya timu hiyo, sasa kuwa na wachezaji 29.
Timu hiyo imeweka kambi mjini Mwanza ikijiandaa na pambano
Wasiwasi wangu ni kwamba, maandalizi ya timu hiyo yamekuwa ya mashaka na
sijui
Ninasema hivyo kwani hadi sasa ninashangaa kuona kuwa, FAT imetangaza
kwamba timu hiyo itasafiri mpaka
Pambano
Hatuelewi kwa nini imekubali mwaliko huo bila kwanza kutafakari faida na
hasara ambazo zitapatikana kwa wachezaji kucheza mechi hiyo ya kirafiki ambayo
hatuamini
Ikumbukwe kuwa
Inashangaza kuona FAT imekubali haraka kwenda
Mimi ninasema mechi
Ninasema hivyo nikijua kuwa
ingawa siombei baya kwa timu yetu lakini, safari ni safari. Lolote laweza
kutokea wakati wowote ikiwa ni pamoja na kuchelewa kunakoweza kusababishwa na
tatizo la usafiri.
Kuna hatari ya kuwachosha wachezaji katika siku yenyewe hasa na kibaya
zaidi, hata
Ni vizuri kujiandaa kwa mazoezi
Ninashindwa kujua
Hivi kucheza mechi hiyo na
Lengo langu si kuipinga Taifa Stars kupata mechi za majaribio la hasha
isipokuwa, wasiwasi wangu ni muda wa mechi hiyo.
Tukumbuke kuwa ng’ombe hanenepi siku ya mnada, hivyo tulitakiwa tuanze
mapema zaidi?
Tuaamini kuwa kikosi kizuri cha Taifa Stars hakiwezi kujengwa kwa
kutegemea pambano la
Ninaomba wahusika kuwa makini na maamuzi wanayoyatoa katika kipindi
hiki.
Tinner Paul
S.L.P. 6202
TAFAKARI
YA WIKI
Walakini
kwa habari ya mtu maskini uwe mvumilivu, na kumwongezea siku kwa huruma.
Umsaidie
maskini kwa ajili ya amri; na kadiri ulivyo ukata wake usimfukuze mikono
mitupu.
Poteza
fedha zako kwa ajili ya ndugu yako na rafiki yako, zisiharibike kwa kutu chini
ya jiwe
Yoshua Bin Sira 29: 8-10.
Mambo
mema mbele ya kinywa kilichofumbwa ni
Yoshua
Bin Sira 30: 18
It is prepared by Miss. Christina Nyambo. Authorised
and run by Rev.
Fr. Revocatus Makonge, Exec. Sec. of
the Communications Department of TEC.
Please visit the TANZANIA
EPISCOPAL CONFERENCE WEB SITE