Uamsho
ni Ulokole katika Ukatoliki?
l Karismatiki ilianzishwa na Walokole
l Sasa
Walokole hujichomeka katika Uamsho wa Kikatoliki
l ASKOFU: Chama cha kitume kinachodharau
kingine marufuku
ASKOFU Msaidizi wa Jimbo
Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Method Kilaini na Mratibu wa Karismatiki
Katoliki iliyopo Tanzania, Joseph Mshiri, wameweka wazi kuhusu kikundi cha
Wanauamsho baada ya watu kutokielewa na kukitazama
Novatus Magege, muumini wa
Parokia ya Kurasini, Jimbo Kuu la
Kuhusu tofauti zao na Waprotestanti (Walokole), alisema.
“Tofauti
Bw. Joseph Magabe, wa Parokia ya Kiagata, Jimbo Katoliki la
Musoma, yeye alipoulizwa kwa simu toka Musoma, alisema, “Kwa kweli hiyo
Karismatiki mimi ninaisikia tu, sijui ni nini. Ila, nasikia wanafanya mambo
Mmoja wa waamini waliokuwa katika Mkutano wa Injili wa hivi
karibuni uilofanyika katika Kanisa La Pentekoste Tanzania (KLPT), katika Parish
ya Keko,jijini
Katika kutafuta ufafanuzi juu ya jambo hili linaloonekana
kutoeleweka kwa jamii, kwa nyakati tofauti Gazeti la KIONGOZI lilikutana na
Mratibu wa Karismatiki Bw. Mshiri.
Mshiri alisema, “… Wakarismatiki sio Walokole. Unajua
wanaojiita Walokole sio dini wala dhehebu, hao ni watu wachache tu, wanaojiona
kuwa wao ni cream yaani
Wana karama ya Kuhubiri Injili kwa kutumia zawadi (karama) za
Roho Mtakatifu ambazo ndizo nyenzo maana Kristo anamuita kila mtu kumtumikia
kwa karama yake na katika nafasi yake.
Akaongeza kuwa, “ Hawa wana karama ya kuhubiri na kuombea
watu wengine hata wagonjwa.. .. hapa ni lazima kila mtu atambue ameitiwa nini
katika kutumikia Ukristo.”
Kuhusu suala la kunena kwa lugha, Bw.
Mshiri alikuwa na haya, ”Mtu anaanza mwenyewe kunena na wala sio kwamba anapata
mafunzo mahali popote na ni vema hata Wakarismatiki wanajua wazi kuwa wakati
mwingine, kunena kunaweza kuwakwaza watu wengine. Ndiyo maana hilo halifanyiki
kanisani.”
Hata hivyo, anaongeza kuwa, “Kwa bahati
mbaya ipo kasumba inayowanyemelea baadhi ya Wanakanisa kudhani kuwa Karismatiki
ndiyo safi kuliko wengine na wengine wanapotoka kwa kudhani kuwa, kama mtu
haneni kwa lugha, huyo eti hana Roho Mtakatifu. Hiyo si kweli. Hapo ndipo
linakuja tatizo la watu wengine wenye karama kujiona wa juu kuliko watu wengine
na hivyo, kuvunja umoja wa Kanisa.
Alisema kila Mkristo
Kuhusu kusali nje ya Kanisa, Bw. Mshiri
alisema, “…Hatuwezi kuwafikia watu wengine wakiwamo Waislamu na wale wa
madhehebu mengine kama hatutatoka nje ya kanisa kwa sababu, kanisani watu hawa
hawaingii.”
Kuhusu suala hilo, yafuatayo ni maneno halisi ya Mhashamu
Method Kilaini, Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, juu ya
Karismatiki Katoliki
“ILI kuelewa hili, kwanza tujue kwamba Kanisa
Katoliki ni pana; na Mungu ni mpana
ambaye kila wakati tunajifunza kitu kimoja na kingine kuona jinsi gani
kinaweza kuleta msisimko. Katika mafundisho ya Kanisa yapo mambo mengi sana, na
katika nyakati mbalimbali za kihistoria, mara unakuta kipengele fulani
kameshikwa, kipengele kingine kimeingizwa sana.
Vyote hivi ni vipengele tofauti vya Kanisa hilo hilo ambalo
linahamasisha Wakristo.
Unakuta wakati mwingine Moyo Mtakatifu
wa Yesu, uliingia sana. Moyo Mtakatifu wa Mama maria ukaingia sana, Mtakatifu
Anna na karama zake, ikaingia sana.
Katika kuelewa ukweli wa namna hiyo,
tunaweza tukaelewa na Karismatiki.Kwanini Karismatiki inakuja leo; likuwa wapi
na ilikuwa inafanya nini?
Karismatiki ni mojawapo ya vyama vya kitume ambavyo msisitizo wake unakuwa
juu ya karama zake Roho Mtakatifu. Hii ina mwanzo wake kwani tangu mwanzoni mwa
Kanisa, Wakristo wa mwanzo walisisitiza sana juu ya karama za Roho Mtakatifu.”
Anaendelea,”Kadri Kanisa lilipoanza liliweka mpango mmoja
baada ya mwingine ili kuweka msisitizo wa karama ya kujitoa, kumbe misisimko ya
haraka haraka ikapungua na kuwepo mipangilio ambayo inafanya vitu
vilivyopangwa; kwamba tunaposali tufanye hivi, tufanye vile, hapa tuinue
nikono, hapa tuiweke chini, ambapo sasa unaona katika Kanisa la mwanzo wakati
wanafanya ule msisimko wa Roho Mtakatifu, ilikuwa ni ile hisia. Walitumia
Na kadiri muda
ulivyokwenda hisia zilipungua na kukawepo na mipangilio ambayo
inaeleweka. Lakini mara nyingine kuna uhitaji, hivyo katika kipindi tulichoingia na hasa baada ya Mtaguso wa Pili, ikatokea
nafasi kwamba watu wenyewe vilevile waanze kuleta hisia zao katika namna
wanavyofundisha na wanavyotoa msimamo wa dini.
Na katika hisia zao, zikaja karama zake Roho Mtakatifu ambazo
ni kuhubiri; mtu akijisikia anahubiri, mtu anapoimba anaweza akaruka.
Zamani walikwambia hata mikono uifunge namna gani, na uifunge
kwa kiasi gani.
Haya ni mambo ya kihistoria kwa sababu haya ni mambo ya
binadamu anavyoitikia wito wa Mungu kufuatana na nyakati zake kufuatana na hali
yake.
Itaendelea Toleo lijalo
Wakazi
watatu wahukumiwa kunyongwa Tarime
l Wawili waliua wake zao
Na Mwandishi Wetu, Tarime
MAHAKAMA Kuu ya
Katika tukio la hivi
karibuni Mahakama hiyo iliyokutana katika ukumbi wa Mahakama ya Wilaya ya
Tarime, Oranda Nyakua (35), mkazi wa Utegi, wilayani hapa, alihukumiwa
kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mkewe, Pamela
Nyakua, kwa kumkata panga.
Akisoma hukumu hiyo katika Mahakama ya Wilaya
ya Tarime Jumatano iliyopita, Jaji John Mtolela, alisema Mahakama Kuu imetoa
hukumu hiyo chini ya Kifungu cha 197 cha Kanuni ya Adhabu Namba 322 cha Sheria
ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai, baada ya kuridhika na ushahidi wa upande wa
mashitaka uliotolewa mahakamani hapo.
Awali, Wanasheria wa Serikali, Feleshi Mbuki
na Deo Mgengeli, walidai mahakamani hapo kuwa, Oktoba 11, 1995, Saa 5:00
asubuhi, katika Kijiji cha Masike wilayani Tarime, mshitakiwa kwa makusudi
alimvizia kisimani na kumkata kwa panga kichwani na katika mkono wa kushoto,
mkewe, Pamela Nyakua, shambulio hilo lilisababisha kifo baada ya dakika chache.
Katika tukio jingine, Septemba 27, mwaka huu,
Mahakama Kuu hiyo ilitoa hukumu ya kumyonga hadi kufa, mkazi wa Kijiji cha
Nyamaharaga, Wilaya ya Kehancha katika nchi jirani ya
Ilidaiwa mahakamani hapo
na wanasheria hao wa Serikali kuwa, Februari 19, 1990 mchana, kwa kushirikiana
na nduguye, Sagore Buruna Sibare ambaye alitoroka, kwa kudhamiria walimkata kwa
panga mguu wa kushoto na mgongoni, mkazi wa kijiji cha Ketenga Wilayani Tarime,
Chacha Bisase na kumsababishia kifo saa mbili baadaye.
Katika tukio jingine,
Septamba 30 mwaka huu, Mahakama Kuu hiyo ilimhukumu kunyongwa hadi kufa, mkazi
wa Kijiji cha Tagota Wilayani Tarime, Lucas Kimito (69), baada ya kupatikana na
kosa la kumuua mkewe Wagesa Kimito.
Mbele ya Jaji Mtolela,
wanasheria wa Serikali waliimbia Mahakama Kuu kuwa, Machi 12, 1995 wakiwa
nyumbani, kwa makusudi mshitakiwa huyo alimshambulia kwa ngumi na fagio hadi
kumuua mkewe Wegesa Kimito baada ya kuzuka ugomvi wa kifamilia.
SINODI YA UCHAGUZI NA KATIBA:
Wamoravian hatima ya Kanisa lenu imo mikononi mwenu,
lioneeni huruma
lWachungaji
matumbo yawaka moto; Kitendawili cha nani atakuwa nani kigumu
Na Waandishi Wetu, Dar na Tukuyu
TANGU mwishoni
mwa juma, Kanisa la Moravian Tanzania (KMT), Jimbo la Kusini; mji wa Tukuyu
umekuwa na wageni mbalimbali wanaohudhuria Mkutano wa Sinodi ya Katiba na ile
ya Uchaguzi Katika Kituo cha Mikutano cha Rutengano mjini Tukuyu, inayofanyika
Oktoba 7 hadi 1 2, mwaka huu.
Sinodi hiyo inayofanyika nje kidogo ya mji wa Tukuyu
kuelekea Kyela inawahusisha wajumbe zaidi ya 310, wakiwa ni wachungaji wa
shirika zote za Jimbo zipatazo 155 wakiwa na mjumbe mmoja mmoja kutoka kila
ushirika.
Viongozi
wakuu wa KMT, Jimbo la Kusini yaani Askofu Lusekelo Mwakafwila, Mwenykiti wa
Jimbo, Mchungaji Angetile Musomba na Katibu Mkuu, Mchungaji Nelsen Mwaisango,
kwa nyakati tofauti mwaka huu, waliliambia KIONGOZI kuwa Sinodi ya Uchaguzi
hukutana kila baada ya miaka minne wakati ile ya marekebisho ya Katiba hukutana
kila baada ya miaka sita.
“Mwaka
huu Sinodi zote mbili zimeangukia pamoja, ila itaanza hii ya Katiba kisha
ifuate ya Uchaguzi,” alisema Mchungaji Musomba wakati akizungumza na KIONGOZI
katika Sikukuu ya Pasaka Mwaka huu.
“Huo
ni Mkutano mkubwa unaowachagua viongozi wote wa Jimbo, wakiwamo Wenyeviti wa
Wilaya,” alisema Askofu Mwakafwila alipozungumza jijini Dar es Salaam, miezi
michache iliyopita.
Naye
Katibu Mkuu, Mchungaji Mwaisango, alisema jijini kuwa, “Wanaochaguliwa katika
Sinodi ni Mwenyekiti wa Jimbo, Makamu Mwenyenyekiti, Katibu Mkuu na Wajumbe wa
Halmashauri Kuu ya Jimbo.”
Hadi
hivi sasa, kila mtu anajiuliza nani ataibuka kiongozi katika uchaguzi huo na
atachaguliwa kuongoza katika ngazi gani.
Kwa
mujibu wa taratibu za KMT, hakuna kugombea nafasi yoyote hususan Mwenyekiti wa
Jimbo au Wilaya, Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu.
Wajumbe
wa Mkutano kila mmoja huandika kwa siri jina la mchungaji anayemtaka kuongoza
kwa ngazi fulani na kisha huangaliwa wenye kura nyingi ambao hupigiwa tena kura
za siri hadi anapopatikana kiongozi.
Kutoka Tukuyu Mwandishi Wetu anajaribu kuelezea
mtazamo wake na kukumbusha kidogo historia muhimu ya KMT jimboni humo. Endelea.
HIVI
karibuni, jina la KMT, hususan Jimbo la Kusini, limekuwa likitajwa mara kwa
mara katika vyombo kadha vya habari.
Tunafurahi
kuona hivyo, hasa tunaposikia, kuona au kusoma habari hizo zikiwa zinalihusu Kanisa, zikielezea maendeleo na kutoa
changamoto zaidi kwa jamii ili kuimarisha maendeleo ya kiroho na kimwili.
Hata
hivyo, kwa upande mwingine wa shilingi, habari
hizo zimekuwa ni zile ambazo, yeyote mwenye nia njema na KMT, hatamani
kuendelea kuzisikia au kusoma.
Hii
haitokani na ukweli kuwa zimepotoshwa, bali kutokana na kile kinachoelezwa hasa
tuhuma za ukiukwaji wa maadili ya uongozi katika KMT, jimboni Kusini.
Mara
kwa mara vyombo hivyo, vimeripoti mapendekezo ya waamini wa KMT, jimboni
wakiwamo wachungaji wakimtaka Mwenyekiti wa Jimbo la Kusini, Mchungaji Angetile
Musomba, apumzike nafasi yake ya
Uongozi.
Katika
kutoa sababu za madai ya waamini hao, wanadai Mchungaji Musomba, akiwa
Mwenyekiti wa Jimbo (KMT), amekuwa akitoa nafasi za uwakilishi wa Jimbo katika
Mikutano ya nje ya nchi, kwa upendeleo, pamoja na mengine yanayopingana na
maadili ya Utumishi wa Mungu.
Katika
hili, mimi sio hakimu wa kutoa hukumu juu ya nani ana ukweli wote isipokuwa
pia, ninakumbuka dhahiri kuwa madai hayo, yalikanushwa na Askofu wa Jimbo hilo,
Lusekelo Mwakafwila, pamoja na Mwenyekiti mwenyewe.
Kama
hivyo ndivyo, wakati huyu anasema ndivyo, na huyu anasema sivyo, kuna
kuelewana? Kama hakuna kuelewana, matokeo yake ni nini kwa Kanisa? Linajengeka
au linabomoka? Lakini, kama linabomoka, Wamoravian hawaoni kuwa kuruhusu nyufa
katika Kanisa ni aibu kwa Wakristo?
Hivi
kwa nini Wamoravian wote; walalamikaji na walalamikiwa, wasilionee huruma
Kanisa wakatii ukweli, kwa manufaa ya Kanisa na Ukristo kwa jumla?
Labda
kabla hatujaenda mbali, tukumbushane japo kwa ufupi tu, historia ya KMT
jimboni, wakati tishio la kuwepo kwa nyufa lilipoanza kujitokeza.
Hii
ilikuwa mwaka 1988, ilipojitokeza migogoro kadhaa wakati KMT Jimbo la Kusini
likiwa chini ya uongozi wa Mwenyekiti, Mchungaji Musomba na Makamu akiwa
Mchungaji Samweli Mwakijambile; Katibu Mkuu, alikuwa Mchungaji Nelsen
Mwaisango.
Ni
dhahiri kuwa migogoro hiyo ilitokana na tuhuma za matumizi mabaya ya pato la
ofisi miongoni mwa viongozi.
Ni
wazi kuwa hali hiyo, ilifanya kuwepo picha fulani ya kuwindana miongoni mwa
viongozi ingawa hali hiyo haikuwekwa wazi na wahusika ambao wote ni wana Kamati
ya Utendaji. Sakata moja wapo lilikuwa la mashine ya mbao, ambayo ilitoweka
katika mazingira ya utata.
Sakata
hilo, lilikuwa limemkalia vibaya Mwenyekiti. Kutokana na hali hiyo, ikabidi
aliyekuwa Makamu, akalie kiti hicho katika kulishughulikia suala hilo.
Hata
hivyo, ilitia faraja kwani baada ya mazungumzo ya busara kutumika, msamaha ndio
ulioafikiwa na kuacha mambo yalivyo. Hii ilipangwa kuwa siri ingawa baadaye
haikuwa siri tena.
Ukapita
muda, janga la kutoeleweka vizuri katika mapato na matumizi ya pesa,
likamgeukia Makamu. Safari hii aliyekalia kiti katika kushughulikia suala hilo,
akawa Mwenyekiti wa Jimbo.
Katika
kuyamaliza hayo, Makamu akakubali kubeba msalaba huo, Mwenyekiti hakukubaliana.
Kutokana
na ama ujanja wa bahati mbaya au wa makusudi, suala la Makamu Mwenyekiti
likawekwa wazi kuwa anatuhumiwa kwa ubadhilifu wa shilingi laki moja na nusu
(150,000/=). Hali hii ikazua uelewano dhaifu katika Kanisa. Na hali ilikuwa ya
kutisha.
Katika
suala hili, kulikuwa na mgawanyiko. Wapo waliosema Makamu Mwenyekiti huyo alipe
pesa hiyo ili aendelee na kazi, wapo waliosema aondoke kabisa. Pia,
hawakukosekana waliotaka viongozi hao wote; Mwenyekiti na Makamu wake, waondoke
katika nyadhifa zao.
Ikumbukwe
kuwa ipo dhana ambayo kwa mtazamo wangu binafsi, ninaiona si nzuri ndani ya
Kanisa na ni sumu katika umoja wa Kristo.
Hii
ni dhana ya mapokeo kwamba, kati ya Mwenyekiti wa Jimbo, Makamu, na Katibu
Mkuu, mmoja akitoka Kyela, Mwingine atoke Ileje na mwingine atoke Tukuyu.
Kwa
mantiki hiyo, Mchungaji Musomba (Mwenyekiti), alikuwa mwakilishi wa Wandali
(Ileje), Mchungaji Mwakijambile (Makamu), aliwakilisha Wanyakyusa wa Kyela;
wakati Mchungaji Mwaisango (Katibu Mkuu), aliwakilisha Wanyakyusa wa Tukuyu.
Mimi
ninadhani dhana na mapokeo ya uwakilishi wa namna hiyo si nzuri kwani ina
hatari ya kumuweka kiongozi asiye na uwezo na kuwaacha wenye uwezo wa kuongoza
katika nafasi husika, ili mradi tu, kuna mbegu hiyo mbaya ya ukabila.
Wamoravin wanapaswa kujua kuwa Yesu anahimiza
umoja katika Kanisa sio ukabila katika Kanisa.
Ieleweke
kuwa Jimbo la Kusini, linazo wilaya nne (kwa mujibu wa KMT). Hizo ni Wilaya ya
Kusini (Kyela), Wilaya ya Magharibi (Tukuyu), Wilaya ya Kati (Ileje) na Wilaya
ya Mashariki (Dar es Salaam, Morogoro na Pwani).
Pia,
dhana ya uwakilishi wa namna hii ni hatari kwa sababu, ipo hatari upande mmoja
ukamfanya mtu mmoja ajione kama mungu-mtu ndani ya Kanisa na hata kuamini kuwa
hakuna mwingine kama yeye.
Ninasema
hali hiyo inadumaza Kanisa kimanedeleo kwani licha ya kumfanya mtu ajisahau,
alale usingizi, pia haitoi mwanya wa kutosha kwa waamini wengine kutumia vipawa
vyao kulitumikia Kanisa la Mungu.
Ni
vema jamii ya Wamoravian wa Jimbo la Kusini, itambue kuwa, katika milenia hii
ya tatu, miongoni mwa mambo yanayoweza kuhatarisha umoja, mshikamo na udugu katika
Kanisa, ni upatikanaji wa viongozi kwa vigezo vya umaarufu wa kabila au ukoo.
Hivi
umaarufu wa ukoo na mambo ya Mungu, wapi na wapi?
Sasa,
itasikitisha zaidi kama waamini wa Moravian Jimbo la Kusini, wataendelea
kuruhusu kuwapo tena kwa migogoro ndani ya Kanisa lao na wakasahau kuwa Mungu
alisimama pamoja na Kanisa hadi likafika lilipo.
Inasikitisha
kuwa licha ya neema hizo za Mungu, joto na fukuto la chuki, ukabila na mgawanyo
linaanza kulinyemelea Kanisa huku waamini wapo; tena pengine wanashiriki kwa
kuwa chanzo kwa namna moja ama nyingine; aibu.
Hivi
Wamoravian kwa ujumla wenu, mnalitakia
nini Kanisa lenu; kwanini msilionee huruma na kulinusuru lisianguke kwenye
janga la migogoro?
Hata
hivyo, namna nzuri ya kulinusuru Kanisa, ni kuona kuwa, waamini wanakuwa
wakweli. Penye kustahili pongezi, wampongeze Mwenyekiti (Mchungaji Musomba)
kwani ni ukweli ulio wazi kuwa licha ya kumtuhumu kwa hili na lile, yapo mengi
mazuri aliyayofanya ndani ya Kanisa.
Uamuzi
wa busara na unaojenga heshima ya kiongozi husika, na Kanisa kwa jumla.
Umefika
wakati sasa, chuki zisizo na maana, zikaepukwa na kila mmoja hasa viongozi wawe
mfano bora wa kuonesha na kulinda heshima ya Kanisa, kila mmoja ajue kuwa ukabila,
ni sumu ndani ya Kanisa, ubinafsi, kwa kila mmoja awe muumini au kiongozi ni
hatari.
Hata
zama za kupuuza suala la watumishi wa Mungu kujiendeleza na hatimaye kuonekana
kama anasa, zimepitwa na wakati.
Anayeona
hakubaliki ndani ya Kanisa kiuongozi, aache wengine wajaribu kulisukuma
gurudumu la maendeleo ya jamii kiroho na kimwili.
Pia,
ni vema msamaha wa kweli utawale na aina yoyote ya ubaguzi iondolewe.
Kila
mmoja ajue kuwa hatima ya Kanisa la leo na la kesho, ipo mikononi mwa waamini.
Kila
mmoja ajue kuwa majungu kamwe hayajengi na ubinafsi unaolenga kujinufaisha au
kunufaisha kikundi fulani cha watu kwa kutumia dhamana aliyonayo mtu, iepukwe
sasa. Uchaguzi huu utumiwe kulijenga Kanisa sio kuliangamiza.
Wamoravian
wajue kuwa, kosa lolote watakalolifanya sasa, linaweza kuwaliza kwa miaka minne
ijayo na hata zaidi.
Wachungaji
wa zamani nao watambue kuwa, mbele ya Mungu na mbele ya jamii, wanao wajibu
mkubwa kutoa ushirikiano wa dhati baina yao na wachungaji vijana wa sasa,
wasigeuze Kanisa kuwa uwanja wa ushabiki na upinzani wa kidini, kikabila na
kiukoo.
Watoe ushauri kwa
viongozi na wachungaji wengine wakilenga kulinufaisha Kanisa sio kumnufaisha
wala kumpendeza mtu mmoja mmoja. Wasitoe ushauri wa kuliangamiza Kanisa na
kuifanya jamii vikiwamo vizazi vijavyo, viwalilie.
Wamoravian wajue kuwa
wametumwa ili wawe watumishi waaminifu shambani mwa Bwana; walihurumie Kanisa.
Sinodi ya Uchaguzi
jimboni humo, iwe chachu ya kujenga upendo, ushirikiano na umoja ndani ya
Kanisa. Itumike kumpata kiongozi ambaye ataliongoza vizuri Kanisa hata
Wamoravian Jimbo la
Kusini hawana budi kujua kuwa kosa watakalolifanya katika Uchaguzi huu,
litakuwa gharama ya mahangaiko
CHAGUENI
VIONGOZI WATAKAOLISAIDIA KANISA NA UKRISTO KWA JUMLA NA WENYE DHANA YA
MAENDELEO.
Fanyeni hivyo mkijua kuwa mkikosea katika
Sinodi hii ya Uchaguzi, msimlaumu mtu; mjilaumu wenyewe.
lWote hakuna hata mmoja aliyekamilika
Na Joseph Sabinus
MIGONGANO baina ya watu hutokea
kwa kuwa tu, kila mmoja hataki kukubali kuwa yeye ni tofauti na kila mtu, kwa
sura, jina, tabia, malezi, mzingira ya kuzaliwa na kukulia namna ya kupokea na
kukabili taarifa na hata kuichambua.
Hivyo, marekebisho na
uvumilivu mwingi huhitajika katika jamii kwani tofauti hizo husababisha
migongano na kutoelewana hasa katika sehemu za kazi na makazini.
Hii ni kutokana na ukweli
kuwa, kadiri watu wanavyotofautiana kitabia, ndivyo kunavyokuwa na uwezekano
mkubwa wa kupata migongano.
Ni muhimu kila mtu
akatambua na kukubali kuwa namna alivyo ni tofauti kabisa na alivyo rafiki,
mkewe au mmewe, wazazi na watu wengine kwani hata mapacha wanataofautiana kwa
hili ama lile mradi tu, hawafanani kwa kila kitu.
Ni wazi kuwa ili kuishi
na kushirikiana vema katika jamii ya
watu wanaokuzunguka, ni muhimu kwanza kabisa, kujua tabia yako mwenyewe ili
uweze pia kujua namna ya kuwaongoza na kushirikiana na wengine katika jambo lolote
hata kama wana tabia tofauti na yako.
Ujuzi wa tabia yako na za
wengine utakupa wigo mpana wa kushughulikia jambo au kushirikiana na watu
wengine wenye tabia tofauti kwa ufanisi na kwa amani.
Maarifa haya,
yatakuwezesha hata kuchagua rafiki, mume au mke mshauri mzuri katika masuala ya
kimaisha au kikazi ambaye tabia yake na
yako zinashabihiana au zinaweza kujirekebisha na kufanana kwa urahisi.
Marekebisho haya
yatafanya pia watu hao waepuke
kufarakana kwa kuwa watafanya marekebisho yanayohitajika. Wakifahamu tofauti
hizo, wanaweza kuishi ama kufanya kazi kwa amani zaidi.
Maarifa ya tabia za
watu mbalimbali ni muhimu katika
uchaguzi wa kazi fulani zinazohitaji watu fulani. Kwa viongozi ni muhimu kujua
tabia za unaowaongoza ili kujua namna ya kuwapangia kazi za kudumu kutokana na
tabia zao.
Kwa mfano, mtu asiye na
mpangilio mzuri wa mambo ni vugumu kufanya kazi za uhazili au uhasibu au hata kuongoza vyombo
Mtu ambaye ni mwepesi wa
kuogopa hatari anaweza asifae kabisa kazi za uokoaji, upelelezi, uandishi wa
habari, urubani au hata kuongoza jeshi katika vita.
Kadhalika, mtu asiyependa
kutabasamu hafai kabisa katika kazi
Pia, mtu asiyependa
kuzungumza mbele za watu anaweza asifae kabisa katika kazi za uhakimu, uhubiri,
upelelezi na uendesha mashtaka.
Ni muhimu kujua watu hao
kwa kuwa baadhi hupenda kutumia nguvu
na madaraka na wengine hushawishi wanapohitaji kitu au jambo fulani.
Wengine ni wasemaji
Ni dhahiri kuwa ni watu
wachache wenye moyo wa huruma na wapenda haki wenye utu na wengine ni wale
wenye msimamo
Watu wengine hupendelea
kuuliza maswali mengi kabla ya kufanya
jambo na wengine hukubali kwa urahisi bila hata kuuliza swali. Hao ni rahisi
kubadili msimamo.
Wengine mambo na sauti zao ni polepole wakati mwingine ni
wepesi wa kutenda mambo bila
hata uvumilivu wala uchunguzi na tafakari ya kutosha.
Tofauti hizo za watu
zinatokana na tofauti za tabia zao.
Mtaalamu mmoja wa
Kigiriki wa tabia za watu Bw.
Hipprocratus katika kitabu chake cha Hippocratus, alitenganisha
na kujaribu kuzipanga tabia za binadamu katika makundi manne yaani, “choleric” kama mtu
mwepesi wa hasira; wakati “sunguine” alielezwa kama mtu mwenye
furaha kwa wakati mwingi, mwenye kutumaini na kutazamia wema tu.
Anapenda
watu na ni mwenye bidii.
Mtaalamu
huyo alimtaja ‘Philegmatic’ kama mtu mtulivu, thabiti na
asiyeshtuka na mwisho akamuelezea ‘Melancholy’ kuwa ni mtu ambaye
ana tabia ya kuhuzunika, uchungu, mwepesi wa kukata tamaa na mzito wa
kufanya jambo.
Mtaalamu
mwingine wa Kiingereza yeye aliziweka tabia za watu katika makundi kama hao ila
kwa majina tofauti. ‘Dominance’ alitajwa kama mtu mwenye tabia ya
kupenda kutawala wengine na kutumia nguvu huyo alifananishwa na ‘Choleric’
kama alivyotajwa na mtaalamu wa tabia za watu wa Kigiriki.
‘Influencing’ yeye alitajwa kuwa ni yule mtu mwenye tabia ya kupenda
kuongoza wengine huku akiwashawishi kwa kutumia mvuto wake.
Ni
mtu mwenye furaha mara kwa mara na hupenda watu. Huyo ni sawa na ‘Sunguine’.
‘Compliance’ huyu ni mtu mwenye tabia ya kupenda kukubali kufuata,
kutii na kuridhika. Anapenda kuwaacha wengine wafanye wanavyopenda ana tabia ya
kuogopa kuingia kwenye migongano na hivyo, huogopa asikatae jambo
analoambiwa ; ni sawa na ‘Melancholy’.
‘Steadness’ ambaye alifananishwa na ‘Philegmatic’
yeye ni mtu mwenye tabia ya uthibiti, uadilifu, uaminifu na utaratibu.
Ni mwenye tabia ya kupenda mambo yaende sawa ingawa kwa kawaida huwa hapendi
kuongoza.
Ufafanuzi
zaidi wa kila kundi la tabia za binadamu.
‘Choleric au Dominance’ huyo ni
mtawala jasiri. Anapenda kuongoza na kushawishi wengine ili kufanya malengo
yaliyopo yatimie.
Msigeuze mabinti zenu
kuwa mitaji- Askofu Balina
Na Charles Hilila,
ShinyangaASKOFU
wa Jimbo Katoliki la Shinyanga, Mhashamu Aloysius Balina, amekemea tabia ya baadhi ya wazazi kuwatumia watoto wa kike kama mitaji yao
huku wakiwanyima elimu ambayo ni paji la Roho Mtakatifu.
Mhashamu Balina alisema katika Ibada ya Sakramenti ya
Kipaimara katika Parokia ya Bugisi jimboni kwake hivi karibuni kuwa, uduni wa
elimu hususan kwa watoto wa kike mkoani Shinyanga, kwa kiasi kikubwa unatokana
na wazazi kutowajibika vema kwa watoto hao kama wazazi wanavyowajibika kwa
watoto wa kiume.
“Wazazi
wengi wanawaonea
Alisema
tamaa ya kupata
Alisema
tamaa ya kupata
Mhashamu
Balina aliwahimiza wazazi katika Parokia ya Bugisi, kuitumia shule ya sekondari
iliyojengwa katika Parokia hiyo, badala ya kuiacha nafasi hiyo kutumiwa na
wengine wanaotoka nje ya mkoa huo.
“Unaona
sasa, Jimbo limejenga sekondari hapa, lakini ni watoto wangapi wanaosoma pale
wanatoka katika Parokia hii…Kwani wazazi wa hapa hamzai; mbona hakuna watoto
wenu hapa?” Alihoji.
Ili
kuimarisha elimu Jimboni hapa na kupambana na ujinga, Jimbo limeweka mikakati
mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuweka mpango wa Askofu Balina kuzungumza na
wazazi wa watoto katika Parokia zote za Jimbo na kuwaeleza haki ya mtoto
kupata elimu bora katika mazingira
bora, pamoja na manufaa ya elimu na madhara ya ujinga.
Katika
Misa hiyo, Askofu Balina alitoa Sakramenti ya Kipaimara kwa waamini 195 wa
Parokia ya Bugisi. Ilihudhuriwa na mamia ya waamini.
Askofu Ngalalekumtwa ataka waamini
wasiwe bubu, vipofu kukemea uovu
Na Getrude Madembwe, Iringa
ASKOFU wa Jimbo Katoliki la Iringa, Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa,
ameitaka jamii kuepuka tabia ya kufanya maigizo kuwa wao ni viziwi na mabubu,
na hivyo hawaoni maovu yanayotendeka na kuwataka wayakemee.
Aliyasema hayo katikati ya juma lililopita wakati akihubiri katika
sherehe za Wanashirika wa Shirika la Teresia wa Mtoto Yesu zilizofanyika katika
Parokia ya Tosamaganga na kuhudhuriwa na mapadre na masista wa mashirika
mbalimbali, watawa wakiume na wakike pamoja na walei kutoka katika parokia
mbalimbali jimboni humo.
Oktoba Mosi, kila mwaka, huwa ni maadhimisho ya Sikukuu ya Mtakatifu
Teresia wa Mtoto Yesu ambaye ni Somo wa Shirika
Alisema watu wengi wakiwamo waamini, wamekuwa na tabia isiyo nzuri ya
kuona maovu yakitendeka katika jamii, lakini wanayafumbua macho kwa kujifanya
vipofu ama viziwi wasioyaona au kuyasikia.
“Ni heri mtu kipofu wa kweli
asiyeona au kiziwi wa kweli kweli kwa kuwa yeye hasikii, kuliko anayejifanya
kipofu au kiziwi ili asikemee mambo yanayokwenda kinyume na mapenzi ya Mungu,”
alisema Mhashamu Ngalalekumtwa.
Akaongeza, “Mwenye macho haambiwi tazama; sasa kwanini wewe ujifanye
kuwa huoni mpaka uambiwe kuwa tazama?”
Mhashamu Ngalalekumtwa alisema kuwa, katika mazingira hayo ya kiburi cha
kujua na kufumbia makosa, wanadamu wanahitaji msaada wa Mtakatifu Teresia wa
Mtoto Yesu ili wapate kuponywa na kwamba, wanaagizwa kuboresha maisha
Wanashirika hao pia
wametakiwa kuwa na kiu na njaa ya kutimiza matakwa ya Mungu ambayo ni kuwa na
moyo wa huruma, sera, katiba, kanuni inayohitaji kutumika kwa wanashirika.
Maendeleo sahihi
yajali watu sio vitu- Sumaye
Na Eric Samba
MAENDELEO
ya kweli na endelevu, ni lazima yawe maendeleo ya wanadamu badala ya vitu,
amesema Waziri Mkuu, Fredrick Sumaye.
Sumaye
aliyasema hayo juma lililopita katika hafla ya kuchangia Mfuko wa Tume ya
Kikristo ya Huduma za Jamii (CSSC), iliyofanyika katika ukumbi wa AMECEA uliopo
Kurasini jijini
Alisema
maendeleo ya kweli na halisi ni mchakato wa kudumu usio kuwa na mwisho.
“Maendeleo
ni ya kudumu hakuna hatua inayoweza kufikiwa na kusema kuwa sasa tunapumzika.
Hata zile nchi tunazosema zimeendelea, bado hazijapumzika kutafuta maendeleo
zaidi,” alisema.
Aliongeza,
“
Alisema
kwa kutambua
Alisema
Dira ya Taifa ya Maendeleo ya Mwaka 2025, ni mkakati wa makusudi unaolenga
kupunguza umaskini kufikia 2010 na kuuondoa kabisa hadi mwaka 2025
Aidha,
aliwataka Watanzania kujitahidi kusimamia maendeleo
Alisema
itakuwa ni kosa kubwa kwa Watanzania wakifikiri kwamba huko nje kuna waamini na
watu fulani wanaosubiri kuwapa misaada yote wanayohitaji.
Waziri
Mkuu alisema, njia nzuri ya kujitegemea ni kufanya kazi kwa bidii na ubora
unaotakiwa. Alisema mbaya zaidi ni kwamba, Watanzania wengi hawafanyi kazi kwa
bidii, ubora na kujituma.
Aliwashukuru
Maaskofu kwa kukutana na viongozi wa serikali za Mitaa katika kanda mbalimbali
ili kujadili maendeleo bila kujali tofauti zao.
Awali
akimkaribisha Waziri Mkuu, Makamu Rais wa Tume hiyo ambaye pia ni Rais wa
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Severine NiweMugizi, alisema
Tume hiyo iliundwa miaka kumi iliyopita ikiwa na malengo kadhaa ambayo ni
pamoja na kuchangia maendeleo ya wanadamu kimwili na kiroho pamoja na kupanua
na kuboresha huduma za elimu na afya kupitia miradi mbalimbali.
Alisema
Tume yake imeamua kuandaa hafla ya kuchangia kutokana na wafadhili kupunguza
misaada yake kwa taasisi za tume hiyo kwa asilimia 20, ambapo bajeti ya Tume
hiyo ilikuwa ikitegemea wafadhili kwa alisimia 100.
Alisisitiza
kuwa, ili kuziba pengo
Aidha,
alisema kuwa ni muhimu kuchangia huduma hizo kwani wapo Watanzania wengi
wanaotegemea huduma za hospitali na shule zilizo chini ya uratibu wa Tume hiyo.
Alisema
hadi sasa, Tume inakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwa ni pamoja na kuendeleza
huduma za jamii katika hospitali, kuinua kiwango cha elimu ambacho
kimeporomoka, kuongezeka kwa yatima kutokana na ugonjwa hatari wa UKIMWI na
kuongezeka kwa umaskini.
Alisema
Tume hiyo inayoundwa na Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) na Baraza la
Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), inahudumia asasi za afya zipatazo 712 ambapo
kati ya hizo kuna hospitali 81, vituo vya afya 631, hospitali teule za wilaya
18 na hospitali za rufaa mbili.
Aidha,
Mhashamu NiweMugizi alisema kuwa asasi za afya za makanisa zinavyo vitanda
12021 sawa na asilimia 40.5.
Kuhusu
elimu, Mhashamu NiweMugizi alisema kuwa chini ya Tume hiyo, zipo asasi 402
ambapo kati ya hizo, shule za msingi ni 40, shule za sekondari 200, vyuo vya
ufundi 54, vyuo vya elimu sita na vyuo vikuu viwili.
Zaidi
ya shilingi milioni 29 zilipatikana katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na watu
mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini, serikali na wafanyabishara ambapo Waziri
Mkuu Sumaye alichangia shilingi milioni moja.
It is prepared by Miss. Christina Nyambo. Authorised
and run by Rev.
Fr. Revocatus Makonge, Exec. Sec. of
the Communications Department of TEC.
Please visit the TANZANIA
EPISCOPAL CONFERENCE WEB SITE